MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wizara Ya Kilimo Yajipanga Vema Maonesho ya Kimataifa Ya Biashara
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wizara Ya Kilimo Yajipanga Vema Maonesho ya Kimataifa Ya Biashara
Habari

Wizara Ya Kilimo Yajipanga Vema Maonesho ya Kimataifa Ya Biashara

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WIZARA ya Kilimo imeshiriki kwa mafanikio makubwa katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba, kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu fursa na teknolojia mbalimbali za kilimo,

Aidha kuwajulisha wananchi juhudi za serikali katika kuhakikisha usalama wa chakula na lishe kwa Watanzania wote.

Akizungumza katika maonesho hayo, Ofisa Kilimo Mkuu wa Wizara hiyo, Magreth Natai, amesema lengo kuu la ushiriki wao ni kutoa elimu kwa watanzania kuhusu wizara na taasisi zake zinavyohakikisha nchi inakuwa na utoshelevu wa chakula.

“Tumejipanga vyema kuhakikisha tunafikia malengo ya usalama wa chakula na lishe kwa kuwa na dira na mikakati mbalimbali kama vile kuongeza tija katika uzalishaji, kudhibiti upotevu wa mazao kupitia kilimo cha umwagiliaji na ujenzi wa maghala ya kisasa,” amesema.

Amesema Wizara imeweka mkazo mkubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya kilimo, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa maghala katika ngazi ya halmashauri na kaya.

Amesema hatua hizo zimechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza upotevu wa mazao ya chakula kutoka asilimia 30-40 hadi chini ya asilimia 20, huku lengo likiwa ni kufikia asilimia tano.

Katika banda la wizara hiyo, wananchi wamekuwa wakipata elimu juu ya matumizi ya mbegu bora, matumizi ya zana za kisasa za kilimo, mifumo ya taarifa za bidhaa, pamoja na mbinu bora za kuhifadhi chakula ili kukabiliana na sumukuvu na upotevu wakati wa mavuno.

“Tumekuwa na mafanikio makubwa. Kwa zaidi ya miaka 10 sasa, nchi yetu imekuwa ikijitosheleza kwa chakula kwa zaidi ya asilimia 100.

“Mwaka huu pekee tunakadiria kuwa na utoshelevu wa chakula kwa asilimia 128,” amesema.

Amewataka wananchi kufika kwenye mabanda ya wizara na taasisi zake ili kujifunza kwa kina kuhusu fursa zilizopo katika kilimo, pamoja na kupata majibu ya maswali kuhusu mbegu bora, pembejeo na teknolojia mpya zinazosaidia wakulima kuongeza tija na kipato.

Ametaja Taasisi na bodi zilizopo chini ya wizara ya kilimo ni Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), Taasisi ya Udhibiti wa Mbegu Tanzania (TOSCI) na Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA),

Pia Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Tengeru (MATI Tengeru), Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Ukiriguru (MATI Ukiriguru), Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Igurusi (MATI Igurusi),
Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Ilonga (MATI Ilonga), Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Mtwara (MATI Mtwara), na
Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Nyegezi (MATI Nyegezi).

Bodi ya Mazao Mchanganyiko, Bodi ya Sukari Tanzania , Bodi ya Kahawa Tanzania, Bodi ya Chai Tanzania, Bodi ya Korosho Tanzania na Bodi ya Pamba Tanzania.

Vile vile Bodi ya Tumbaku Tanzania, Bodi ya Mazao ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko na Bodi ya Pareto Tanzania.

You Might Also Like

Dar Yaidhinishiwa Bil. 68 Ukarabati, Matengenezo Ya Barabara

Rais Samia Akabidhi Tuzo Kwa NSSF Ya Usimamizi,  Uratibu Wa Hifadhi Ya Jamii Kw Sekta Binafsi

August 10, 2024

WMA Yajivunia Kuongezeka Kwa Wafanyakzai

Mikoa mitatu kuanzishwa vituo vya gesi asilia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TARI Yabadilisha Kilimo kwa Teknolojia Mpya, Za Kisasa
Next Article Maabara Ya Mkemia Mkuu Yashauri Wajasiriamali Wa Kemikali
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mashine Kusaidia Uuzaji Vinywaji Bila Muuzaji
Habari July 8, 2025
Tanzania Yafungua Milango Ya Biashara Na Jumuiya Ya Ulaya
Habari July 8, 2025
Rais Mwinyi Ajionea Mifumo Mbalimbali Banda La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba
Habari July 7, 2025
Maabara Ya Mkemia Mkuu Yashauri Wajasiriamali Wa Kemikali
Habari July 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?