Na Lucy Lyatuu, Dodoma
KATIKA kuadhimisha siku ya mashine za nukta nundu(Breli), serikali imesema watu wenye ulemavu nchini wanakadiriwa kufikia mil 5.3 huku idadi kubwa wakiwa ni wenye ulemavu wa kuona.
Naibu Waziri Wa Nchi, Ofisi Ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge, Uratibu na Wenye Ulema) Ummy Nderiananga amesema hayo leo jijini hapa wakati akizungumzia maadhimisho ya Kimataifa ya Breli ambapo kitaifa kwa Tanzania yatafanyika leo Februari 12 2026 katika mkoa wa Tanga.
Nderianaga amesema hayo wakati akimwakilisha Waziri wa Ofisi hiyo,William Lukuvi na kuongeza kuwa pamoja na idadi hiyo ya wenye ulemavu tofautitofauti lakini wale wasioona serikali imewamefikia kwa kiwango kikubwa kwa kuwapa vifaa na vitendea kazi mbalimbali hususani waliopo shuleni.

“Kwa wasio shuleni serikali imeweza kuwafikia kwa huduma mbalimbali kupitia program nyingine ikiwemo za TASaF, ” Amesema Waziri huyo na kuongeza kuwa mashine za Breli zimekuwa zikiwafkia watoto kuanzia ngazi ya chini ili wajue kutumia vifaa hivyo kupitia ngazi mbalimbali zo hayo amesema yatahusisha shughuli mbalimbali ikiwemoikiwhsho ya teknolojia na kazi za wasioona, upimaji wa elimu na ujuzi wa wasioona.
Amesema Kongamano la wadau na jamii ya wasioona, Shughuli za burudani na hotuba za viongozi wa Serikali na wadau zitatolewa.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Teknolojia ya Breli Husaidia Kuchochea Maendeleo kwa Wasioona na Ujenzi wa Taifa”. ambapo Kauli mbiu hiyo inamaanisha kwamba teknolojia ya Breli inawawezesha Watu wasioona kushiriki kikamilifu katika nyanja zote za maisha (kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia), na hivyo kuchangia maendeleo yao binafsi na ya taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake, Katibu Wa Chama Cha Wasioona, Mkoa wa Dodoma, Enock Mbawa amesema ushiriki wa kundi hilo katika nyanja mbalimbali husaidia kufikisha sauti zao.
Aidha ameiomba serikali kuwashirikisha katika program mbalimbali lakini pia wasisahaulike katika kupata vifaa vitakavyowawezesha kufanikisha majukumu yao ya kila siku.
Kadhalika aliishauri jamii kuwapeleka shule watoto wenye ulemavu
Kwa kuwa vifaa vya kujifunzia vipo.
.

