MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia
Habari

Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: ZAIDI ya wanawake 1,000 kutoka mkoa wa Mbeya wamehitimu mafunzo ya muda mfupi ya ujuzi kupitia programu maalum ya ‘Wanawake na Samia’ iliyoanzishwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kuwawezesha wanawake kiuchumi na kijamii.
Akizungumza wakati wa mahafali hayo, Mkuu wa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Mbeya, Hassan Kalima, amesema zaidi ya wanawake 1,184 walijiandikisha kwa hiari katika mpango huo, ambapo 1,063 kati yao waliweza kuhitimu kwa mafanikio makubwa.
Kalima amesema mafunzo hayo yaliyoanza rasmi Julai 15 Julai 2025 na kukamilika Septemba tisa, mwaka huu 2025, yalitolewa katika Chuo cha VETA Mbeya, yakihusisha kozi mbalimbali.
Ametaja kozi hizo kuwa ni ushonaji nguo, ujasiriamali wa utengenezaji sabuni, batiki, vitafunwa, mapishi, udereva, ufundi magari, ujenzi na zaidi ya kozi 40 fupi zinazotolewa na chuo hicho.
 “Tulitarajia idadi ndogo, labda wanawake 200 hadi 300, lakini mwitikio ulikuwa mkubwa sana. Hii inaonesha ni jinsi gani wanawake wanathamini nafasi ya kujifunza ujuzi utakao wasaidia kujitegemea,” amesema Kalima.
Amesema wahitimu walionyesha furaha na shukrani kwa kupatiwa nafasi hiyo adhimu, ambapo kama ishara ya kutambua mchango wa serikali, walimshonea mgeni rasmi vazi la heshima la kitenge kama zawadi.
Habari Picha 9864
Kwa upande wake, Hamida Mbogo, Katibu wa kikundi cha ‘Wanawake na Samia’ mkoa wa Mbeya na mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo, amesema,
“Tunamshukuru sana Rais wetu Mama Samia kwa moyo wake wa kuwapigania wanawake. Kupitia VETA, wanawake wengi sasa wana matumaini mapya ya kuinuka kiuchumi na kubadili maisha yao.”
Pia amewahamasisha wanawake wote nchini kuchangamkia fursa hiyo akisisitiza kuwa VETA ipo kila kona ya nchi na inatoa mafunzo bora na ya vitendo yanayobadili maisha.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa VETA Tanzania, Anthony Kasore, amesema kuwa awali mpango huo ulilenga kuwafikia wanawake 3000, lakini kutokana na hamasa kubwa na mafanikio yaliyoshuhudiwa, sasa lengo limeongezwa hadi kufikia wanawake 15,000 nchi nzima.
“Tutafungua milango kwa wananchi wote kuja kutueleza wanahitaji mafunzo gani. Sisi tupo tayari kutoa mafunzo kulingana na mahitaji ya jamii,” amesema Kasore.
Mafunzo hayo yanatoa ujuzi wa moja kwa moja unaoweza kutumika mara moja katika soko la ajira au kuanzisha biashara binafsi. Wanawake waliokuwa hawajui namna ya kuoka keki au kushona nguo sasa wanaweza kufanya hivyo kwa ubora wa hali ya juu, na hivyo kuongeza kipato cha familia na kupunguza utegemezi.

You Might Also Like

Rais Wa CWT Suleiman Ikomba Sasa Ni Daktari

Mpogolo Aipongeza Halmashauri Maandalizi Mikopo Asilimia 10

TPHPA yafundisha namna sahihi ya utumiaji wa viuatilifu

Rafiki Planter’Teknolojia Rahisi, Tija Kubwa”

Waziri Mkuu Ashiriki Kumuombea Baba Wa Taifa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa: Serikali Yaanzisha Program Ya Uanagenzi Kwa Vijana
Next Article Majaliwa Afurahishwa Na Ustadi Wa Vijana Wenye Ulemavu Veta
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?