MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wakulima Waomba Watafiti Wa  AGRISPAK, Kuwatafutia Mbinu Kukabili Nzi Weupe
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wakulima Waomba Watafiti Wa  AGRISPAK, Kuwatafutia Mbinu Kukabili Nzi Weupe
Habari

Wakulima Waomba Watafiti Wa  AGRISPAK, Kuwatafutia Mbinu Kukabili Nzi Weupe

Author
By Author
Share
5 Min Read
Na Mwandishi Wetu
WAKULIMA  wamewaomba watafiti wa Mradi wa Mbinu Shirikishi za Wanafunzi na Wakulima katika Uvumbuzi na Uhaulishaji wa Maarifa na Teknolojia za Kilimo  (AGRISPAK), kuwatafutia mbinu za kukabiliana na wadudu aina ya Nzi weupe ambao wanaathiri mazao yao na kusababisha upotevu wa zaidi ya asilimia 70 hadi 80.
Wakulima hao wa Kata ya Nyandira Wilayani Mvomero Mkoani Morogoro, wameomba hayo katika Mradi wa AGRISPARK unaotekelezwa na watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).
Ombi hilo limetolewa na wakulima hao wakati Watafiti kutoka SUA walipokutana nao, kutambua changamoto na mahitaji yao ya maarifa.
Katika kutoa changamoto zao itawasaidia  watafiti kuandaa machapisho kwa lugha ya Kiswahili ambayo yatawaongezea maarifa hivyo kuwasaidia kuboresha kilimo chao na kuinua kipato cha kaya hizo zilizo kwenye eneo la mradi huo wa utafiti wa AGRISPARK.
Akizungumza na watafiti hao Mkulima Peregrin Adam kwa niaba ya wakulima wenzake, amesema  wadudu hao hivi sasa wamekuwa tishio kwa wakulima shambani na hakuna dawa ambayo kwa sasa inaweza kuwaangamiza kwa kuwa wamekuwa wengi.
Amesema wanapopuliza dawa wanaruka ikiisha wanarudi na kuendelea kushambulia mazao.
“Tumefurahi sana kuwaona watafiti kutoka SUA kuja kututembelea na kujua changamoto zinazotukabili,
“Kusema ukweli kwa sasa changamoto kubwa kwenye Kata hii yote ni hawa wadudu weupe huku tunawaita “Masister” kutokana na weupe wao, hakuna dawa tena inayoweza kuwaua wadudu hawa na wamejaa mashambani,
” Wanashambulia zaidi zao la maharage ambalo ndilo zao letu kubwa la biashara kwenye Kata yetu” amesema  Peregrini.
Amesema, “Kiukweli kwa sasa kilimo kimekuwa kigumu sana maana wanashambulia karibu mazao yote ya mbogamboga ambayo ndio tegemeo letu kwa kipato kwa wakulima wote kwenye Kata hii, na wanatupa hasara kati ya asilimia 70 hadi 80 ya mazao yanapotea kutokana na mashambulizi yao”.
Mkulima Adam wa Nyandira ameiomba SUA kupitia kwa watafiti wake kuwasaidia kupata ufumbuzi wa tatizo hilo, ikiwezekana kufikisha kilio hicho kwa serikali na wizara ya Kilimo kuwatafutia ufumbuzi wa wadudu hao ambao wanawapa umasikini wakulima wengi kwa sasa.
“Mkiangalia kwa mazingira yetu huku tunalima mbogamboga msimu wote na tunategemewa sana kwa kuzalisha maharage hasa mabichi kwenda mikoa mbalimbali hasa Dar es salaam na Dodoma lakini kwa sasa uzalishaji wetu umepungua mno kutokana na kuongezeka kwa wadudu hawa hatari wasiosikia dawa ,” amesema.
  Kwa upande wake Mtafiti Mkuu mwenza wa mradi wa AGRISPARK Dkt. Nicholous  Mwalukasa amesema lengo la kuwatembelea wakulima hao ni kutaka kujua changamoto wanazokabiliana nazo katika kilimo ili waweze kutumia uwepo wa machapisho mbalimbali ya kisayansi yaliyopo kuandaa vitabu vidogo.
Vitabu hivyo vitakuwa na mada mbalimbali  ili kutoa elimu ya namna ya kukabiliana na changamoto zao ili kuongeza uzalishaji.
“ Hivi sasa tupo kwenye hatua ya tatu ya mradi ambapo tumekuja kupata maelezo na changamoto zenu ili twende kuwatafutia ufumbuzi wake kupitia tafiti mbalimbali zilizofanyika duniani kote na kwa kutumia wataalamu wa SUA na taasisi zingine na baadae tutatayarisha kwa lugha rahisi ambayo mtaweza kuelewa na kutumia elimu hiyo kutatua changamoto hizi.
“Kwanza niwape pole kwa changamoto mnayokutana nayo kwa wadudu hawa na sisi tumelichukua na tunakwenda kuwatafutia majibu sahihi na ya namna ya kuwakabili wadudu hawa pamoja na changamoto zingine mlizoziainisha,
“Tutaziandaa katika nakala ngumu na nakala laini na kuwaletea ili muweze kupata maarifa hivyo kuendelea kulima kilimo chenye tija na kujikwamua kujipatia maendeleo kupitia kilimo cha mbogamboga mnachokifanya zaidi katika eneo hili,” amesema.
Watafiti hao kutoka SUA kupitia mradi wa AGRISPARK wanatembelea  Kata zilizo ndani ya mradi huo kwenye Wilaya ya Mvomero, Manispaa ya Morogoro pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro vijijini kwa ajili ya kukutana na wakulima na wafugaji kutambua mahitaji yao ya maarifa yanayoweza kusaidia kuinua uzalishaji kupitia kilimo na mifugo katika mnyororo mzima wa thamni wa mazao na mifugo yao.
Mradi wa AGRISPARK unafadhiliwa na Serikali  kupitia SUA, kama maono mapana ya uongozi wa chuo wa kutenga fedha za ndani kwa ajili ya kuwawezesha watafiti wake kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

You Might Also Like

Rais TUCTA Apongeza Mfuko Wa NSSF Kwa Ongezeko La Thamani Hadi Trilioni 9

Biashara kidijitali inawezekana soko huru la Afrika

Wasilisheni Migogoro Yenu Tume ya Usuluhishi na Uamuzi – Massawe

Elimu Ya Fedha Yafika Makanya Same

NCCR-MAGEUZI Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Watafiti Mradi Wa  AGRISPAK kutoka SUA Waanza Uandaaji Wa Vitabu Vidogo
Next Article Timu Ya Watanzania Ikiongozwa Na Profesa Ndunguru, Yakutana Na Balozi Zambia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?