MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wagombea Wa CCM Dodoma Mjini Waanza Kujinadi kwa Wajumbe
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wagombea Wa CCM Dodoma Mjini Waanza Kujinadi kwa Wajumbe
Habari

Wagombea Wa CCM Dodoma Mjini Waanza Kujinadi kwa Wajumbe

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: MBIO za kuwania nafasi ya ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimeanza rasmi leo, baada ya kutangazwa kwa majina ya wagombea nane waliopitishwa na Kamati Kuu ya chama hicho.
Wagombea hao wameanza kujinadi mbele ya wajumbe wa CCM katika kata mbalimbali za jimbo hilo, leo Julai 30,2025 wakiainisha dira na mikakati yao ya kuleta maendeleo endapo watapata ridhaa.
Wagombea waliopitishwa ni Samwel Malecela, Rashid Mashaka, Pascal Chinyele, Samwel Kisaro, Fatuma Waziri, Robert Mwinje, Rosemary Jairo, na Abdulhabibu Mwanyemba.
Kampeni za ndani zimeanza leo Julai 30, 2025 majira ya saa tatu asubuhi katika Kata ya Chigongwe, ambapo Samwel Malecela aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Wazazi wa CCM Mkoa wa Dodoma na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa aliongoza kwa kujinadi mbele ya wajumbe.
Katika hotuba yake kwa wajumbe, Malecela ameainisha vipaumbele vyake vinavyolenga kutatua kero za msingi zinazowakabili wananchi wa jimbo hilo, akisisitiza dhamira ya utumishi uliotukuka na ushirikishwaji wa jamii katika maamuzi ya maendeleo.
Licha ya kuonekana kuwa na ushindani mkali, baadhi ya wagombea wamekutana na changamoto kadhaa kutoka kwa wajumbe. Samwel Kisaro, mmoja wa wagombea, amejikuta katika hali ya kujitetea baada ya kuulizwa swali na mjumbe wa Kata, Amos Ndubaha, kuhusu ushiriki wake katika migogoro ya ardhi.
Ndubaha ametaka kufahamu ni kwa namna gani Kisaro ataweza kutatua matatizo ya ardhi ilhali anaendesha kampuni inayojihusisha na upimaji, ununuzi, na uuzaji wa viwanja shughuli ambazo zimewahi kuzua mgogoro katika maeneo mbalimbali ya Dodoma.
Kisaro amekana madai hayo akisema si mhusika wa moja kwa moja katika shughuli hizo, na huenda amechanganywa na mtu mwingine mwenye jina linalofanana.
Jimbo la Dodoma Mjini limekuwa na historia ya kubadilisha wabunge mara kwa mara kila baada ya muhula mmoja. Tangu mwaka 1995, wabunge waliowahi kuliongoza jimbo hilo ni pamoja na Ashimu Sagafu (1995–2005), Ephraim Madeje (2005–2010), David Malole (2010–2015), na Anthony Mavunde (2015–2025), ambaye sasa amehamia katika Jimbo la Mtumba.

You Might Also Like

Tume Ya Kurekebisha Sheria Tanzania Kuipitia Sheria Ya Takwimu

VETA Kihonda Waja Na Mashine Ya Kusaga Chumvi Sabasaba

Vijana 26 Kwenda Kujifunza Mafunzo Ya Vitendo Nje Ya Nchi

Wafanyakazi fahamuni vihatarishi sehemu za kazi

Erio atoa elimu ya bidhaa bandia kwenye mabanda nanenane

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Zabibu Ya Makutupora Nyekundu Yatajwa Kuwa Ya Kipekee Duniani
Next Article Dkt Yonaz Awaasa Watumishi Ofisi Ya Waziri Mkuu  Kuongeza Bidii Katika Kutekeleza Majukumu Yao
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Chinyeli Aahidi Chakula Bure kwa Wazee, Mwanyemba Kupambana Kutafuta Maendeleo
Habari July 31, 2025
Ajira kwa Vijana na Afya kwa Wazee: Ajenda Kuu za Wagombea Jimbo la Dodoma Mjini
Habari July 30, 2025
Dkt Yonaz Awaasa Watumishi Ofisi Ya Waziri Mkuu  Kuongeza Bidii Katika Kutekeleza Majukumu Yao
Habari July 30, 2025
Zabibu Ya Makutupora Nyekundu Yatajwa Kuwa Ya Kipekee Duniani
Habari July 30, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?