MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe
Habari

Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WAFUGAJI wasio waaminifu wamekuwa wakiongeza unga, mkojo wa ng’ombe, magadi, mafuta ama maji kwenye maziwa jambo ambalo sio sawa kwa kuwa maziwa huharibika upesi.

Ofisa Jinsia na Lishe kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Ruth Mkope amesema hayo alipokuwa akitoa mada kuhusu maziwa katika semina ya Waandishi wa Habari katika kuelekea kilele cha siku  ya Kimataifa ya Maziwa Juni Mosi mwaka huu mkoani Morogoro.

Ruth amesema wafugaji hao wamekuwa wakiongeza vitu hivyo kwenye maziwa wengine wakiongeza maji ili yawe mengi, mafuta ili yaonekane ng’ombe wake ana maziwa mazuri ama unga ili yaonekana mazito jambo ambalo halikubaliki katika tasnia hiyo ya maziwa.

Amesema uongezaji wa vitu hivyo ni kuchocheo cha maziwa kuharibika kwa haraka, ndio maana wananchi wanahamasishwa kutumia maziwa yaliyosindikwa ili kuepuka kuuziwa yaliyochakachuliwa.

Amesema mambo mengine yanayochangia maziwa kuharibika haraka ni pamoja na kiwele cha ng’ombe kuwa kichafu, ama ugonjwa wa kiwele, mkamuaji kuwa mchafu au ana magonjwa ya kuhara, kukohoa, kifua kikuu, kucha ndefu, nywele ndefu, uvutaji sigara pamoja na mazingira yanayomzunguka kuwa machafu.

Ili maziwa yasiharibike haraka amesema mkamuaji anapaswa kuwa msafi, asiyekuwa na vidonda, kukohoa, kupiga chafya au magonjwa ya kuambizwa.

Ili wananchi wapate maziwa salama ambayo hayajachakachuliwa watumie yaliyosindikwa.

Katika hatua nyingine amesema, unywaji wa maziwa unapaswa kupewa msukumo kwa watoto wa shule wenyewe bila kutegemea wafadhili.

“Hii itasaida kuongeza unywaji wa maziwa hivyo kufanya hali ya lishe ya watoto hawa kuwa nzuri na pia kuongeza ari ya wafugaji katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa,” amesema.

Akizungumzia Mchango wa benki hiyo kwa wakulima, Mratibu wa Mradi T13P TADB, Joseph Mabula amesema benki hiyo ilianzishwa kwa ajili ya kuchagiza maendeleo ya sekta ya kilimo nchini katika eneo la mazao, mifugo, uvuvi na misitu.

Pia kuwasaidia wakulima wadogo kuondokana na kilimo cha kujikimu na kuzalisha ziada.

“Majukumu yake ni kuchagiza ukuaji wa sekta ya kilimo, kutoa mikopo katika miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwa ni pamoja na kutoa fedha za gharama nafuu,” amesema.

Semina hiyo ya kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari, imeandaliwa na Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) kwa kushirikiana na benki hiyo ya TADB.

 

You Might Also Like

Benjamini Mkapa Yapandikiza Mimba 21, Watano Waongezewa Nguvu Za Kiume

Wananchi Wahimizwa Kulinda Maeneo Yaliyohifadhiwa  Kisheria- Kamishna  Wakulyamba

Mikataba ya zaidi ya bilioni 50 kuhamasisha nishati salama

Mafunzo Yatolewa Katika Kongamano La Jotoardhi

TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa
Next Article Tanzania Na Namibia Kuongeza Juhudi Kukuza Ushirikiano Wa Kiuchumi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tanzania Na Namibia Kuongeza Juhudi Kukuza Ushirikiano Wa Kiuchumi
Habari May 21, 2025
TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa
Habari May 21, 2025
Dkt. Ndumbaro : Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Imefanikiwa 
Habari May 20, 2025
Senyamule Ahamasisha Ushiriki Wa Vijana Katika Uchaguzi
Habari May 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?