MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wafanyabiashara: Tupo Tayari Kushirikiana na Serikali
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wafanyabiashara: Tupo Tayari Kushirikiana na Serikali
Habari

Wafanyabiashara: Tupo Tayari Kushirikiana na Serikali

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
ARUSHA:  WAFANYABIASHARA wa jengo la biashara la Shirikisho la Vyama vya Wafanyajazi Tanzania (TUCTA), lililopo Arusha wameishukuru serikali kwa kufanikisha uzinduzi wa jengo hilo.
Habari Picha 8991
Aidha wamemtakia afya njema na mafanikio, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete, katika safari zake za kiuongozi.
Pongezi hizo zimetolewa na wafanyabiashara wa jengo hilo, kupitia mwakilishi wao, Emmanuel Saevie, wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo hilo lililozinduliwa na Ridhiwani, kwa kusema ujio wa waziri huyo ni ishara ya kuthamini juhudi za wafanyabiashara na mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa nchi.
Pia Saevie amelipongeza shirikisho hilo,  kwa maamuzi ya kubadili matumizi ya awali ya jengo hilo na kuligeuza kuwa jengo la kisasa la biashara, jambo ambalo limefungua fursa kwa wafanyabiashara wengi kupata maeneo ya kufanyia shughuli zao kwa tija.
Habari Picha 8993
“Tunatoa pongezi za dhati kwa uongozi wa TUCTA kwa uamuzi wao wa kulikarabati jengo hili na kulitumia kwa manufaa ya uchumi. Ni hatua ya mfano kwa taasisi nyingine,” amesema Saevie.
Katika hatua nyingine, Meneja Mkuu wa Wakala wa Uwekezaji wa TUCTA (WDC), Muchunguzi Kabonaki, amepongezwa kwa usimamizi madhubuti uliowezesha jengo hilo kukarabatiwa hadi kuwa na mwonekano mzuri na wa kuvutia.
Habari Picha 8995
“Bila upendeleo wowote, tunampongeza meneja Kabonaki kwa moyo wake wa kizalendo na ufuatiliaji wa karibu. Amefanya kazi kubwa kwa kushirikiana na timu nzima kuhakikisha jengo hili linakuwa la kisasa,” amesema.
Aidha, Saevie ametoa salamu za pongezi kwa wananchi wa Jimbo la Chalinze kwa kumpa ridhaa Ridhiwani Kikwete kugombea ubunge bila kupingwa, akisisitiza kuwa ni ishara ya imani kubwa waliyo nayo kwake.
“Tunamtakia kila la heri katika uchaguzi ujao. Ikiwa itampendeza Mheshimiwa Rais, tunaomba aendelee kumteua Ridhiwani kuendelea na nafasi hiyo ili arudi na kuendeleza yale aliyoanzisha, pindi uchaguzi utakapokamilika” amesema.
Habari Picha 8996
Katika hatua nyingine, Wafanyabiashara waliopata nafasi ya kufungua biashara zao katika jengo hilo wametoa ahadi ya kushirikiana kikamilifu na mamlaka za serikali katika kulipa kodi, kufuata taratibu, na kushiriki kwenye maendeleo ya taifa.
“Tumepewa nafasi, sasa ni zamu yetu kuonyesha mfano bora wa uaminifu na ushirikiano na serikali yetu,” amesema Saevie.

You Might Also Like

TPHPA Yanunua Ndege Kudhibiti Visumbufu Vya Mazao

Bashungwa Asema Wafungwa Kupewa Mafunzo Ya Ufundi Stadi

Bodi Ya  Bima Ya Amana Yapata Mkurugenzi  Mkuu

Mkongo Wa Mawasiliano Unalenga Kuleta Tija Kwa Wananchi

Samia akisalimiana na Rais wa China

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mpango Awaalika SADC Kutuma Timu ya Uangalizi wa Uchaguzi
Next Article Waomba Kuondolewa Vikwazo Vya Biashara Ya Mazao Ya Kilimo Ikolojia Mipakani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?