MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99
Habari

Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: MKUU wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego ametoa wito kwa Watanzania kuanza kutumia vumbi la nyuki kutokana na faida zake lukuki kiafya, akibainisha kuwa linahusisha virutubisho 99 kwa wakati mmoja, na ni salama kwa matumizi ya binadamu wa rika zote.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, Dendego alieleza kuwa mkoa wa Singida umeendelea kuimarika katika uzalishaji wa mazao ya nyuki, ikiwemo asali na nta, na sasa umeongeza zao jipya la vumbi la nyuki lenye thamani kubwa kiafya.
“Mwanzoni ilionekana linafaa kwa wanaume pekee, lakini sasa wataalamu wamebaini linawafaa watu wote – watoto, vijana na wazee,” amesemaDendego.
Ameongeza kuwa vumbi hilo linapatikana katika Kijiji cha Nyuki mkoani Singida, na kwamba serikali ya mkoa inaendelea kutoa elimu juu ya matumizi yake ili kuhakikisha linawanufaisha wananchi kiuchumi na kiafya.
Katika taarifa hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa pia aligusia mafanikio ya sekta ya afya ndani ya kipindi cha miaka minne, akisema Singida sasa ina vituo vya afya na hospitali za kisasa zenye vifaa vya hali ya juu.
 “Kwa sasa hatulazimiki tena kuwapeleka wagonjwa Dodoma, Mwanza au Dar es Salaam kwa matibabu ya kibingwa. Tuna vifaa na tunaendelea kuwajengea uwezo wataalamu wetu ili wavitumie ipasavyo,” amesema.
Mkoa wa Singida unatajwa kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa uzalishaji wa mazao ya nyuki nchini, na sasa kupitia ubunifu na utafiti wa ndani, umeanza kuvuna faida zaidi kupitia zao jipya la vumbi la nyuki – hatua inayolifanya kuwa kitovu kipya cha tiba asilia nchini.

You Might Also Like

Wajumbe IPA Zanzibar Wafanya Ziara TEA

Profesa Mkenda Aitaka TAEC Kusomesha Watumishi

Ujenzi Miundombinu ya Kuongeza Udahili kipaumbele Cha Serikali

Dkt. Biteko ashiriki kilele cha miaka 60 JWTZ

Polisi Kuimarisha Ulinzi Nyumba Za Ibada Krismasi, Mwaka Mpya

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi
Next Article Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchengerwa Apongeza Shule Ya Sekondari Kibaha Kwa Ufaulu Wa Hali Ya Juu
Habari July 9, 2025
NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani
Habari July 9, 2025
Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi
Habari July 9, 2025
Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi
Habari July 9, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?