MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99
Habari

Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: MKUU wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego ametoa wito kwa Watanzania kuanza kutumia vumbi la nyuki kutokana na faida zake lukuki kiafya, akibainisha kuwa linahusisha virutubisho 99 kwa wakati mmoja, na ni salama kwa matumizi ya binadamu wa rika zote.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, Dendego alieleza kuwa mkoa wa Singida umeendelea kuimarika katika uzalishaji wa mazao ya nyuki, ikiwemo asali na nta, na sasa umeongeza zao jipya la vumbi la nyuki lenye thamani kubwa kiafya.
“Mwanzoni ilionekana linafaa kwa wanaume pekee, lakini sasa wataalamu wamebaini linawafaa watu wote – watoto, vijana na wazee,” amesemaDendego.
Ameongeza kuwa vumbi hilo linapatikana katika Kijiji cha Nyuki mkoani Singida, na kwamba serikali ya mkoa inaendelea kutoa elimu juu ya matumizi yake ili kuhakikisha linawanufaisha wananchi kiuchumi na kiafya.
Katika taarifa hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa pia aligusia mafanikio ya sekta ya afya ndani ya kipindi cha miaka minne, akisema Singida sasa ina vituo vya afya na hospitali za kisasa zenye vifaa vya hali ya juu.
 “Kwa sasa hatulazimiki tena kuwapeleka wagonjwa Dodoma, Mwanza au Dar es Salaam kwa matibabu ya kibingwa. Tuna vifaa na tunaendelea kuwajengea uwezo wataalamu wetu ili wavitumie ipasavyo,” amesema.
Mkoa wa Singida unatajwa kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa uzalishaji wa mazao ya nyuki nchini, na sasa kupitia ubunifu na utafiti wa ndani, umeanza kuvuna faida zaidi kupitia zao jipya la vumbi la nyuki – hatua inayolifanya kuwa kitovu kipya cha tiba asilia nchini.

You Might Also Like

SGR Kipande Cha Saba Na Nane kuanza kujengwa

Mtanda Akagua Maendeleo Ya Mradi YA Hoteli Ya Nyota Tano Ya NSSF

Kamati YA Siasa Yaendelea Kukagua Miradi Ya Maendeleo Temeke

Mwenyekiti TCCIA Geita Gabriel Ahamasisha Watanzania Kutumia Bidhaa Za Ndani

TASU yaiomba serikali inunue meli kutoa ajira kwa mabaharia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi
Next Article Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?