MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yaleta Mapinduzi ya Kilimo na Biashara Kupitia Bunifu –  Profesa Nombo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yaleta Mapinduzi ya Kilimo na Biashara Kupitia Bunifu –  Profesa Nombo
Habari

VETA Yaleta Mapinduzi ya Kilimo na Biashara Kupitia Bunifu –  Profesa Nombo

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo, amesema Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), imeanza kuchukua nafasi muhimu katika kubadilisha sekta za kilimo, uchumi na biashara kupitia ubunifu unaolenga kutatua changamoto zinazowakabili Watanzania katika maeneo mbalimbali ya maisha.
Profesa Nombo amesema hayo alipotembelea banda la VETA katika maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nanenane leo Agosti nane, 2025 mkoani Dodoma.
Amesema taasisi hiyo sasa imejikita katika kutoa mafunzo yenye uhalisia wa mahitaji ya sasa, huku ikileta suluhisho kwa changamoto kama ajira, tija kwenye kilimo na ujasiriamali mdogo na wa kati.
“VETA si mahali pa kujifunza tu ni eneo mahsusi la kupata ujuzi kwa mtu yeyote anayetaka kuboresha maisha yake.
“Mafunzo haya yanawajengea Watanzania uwezo wa kujiajiri, hivyo kupunguza utegemezi wa ajira za Serikali,” amesema.
Amesema kuwekeza katika ujuzi ni hatua madhubuti ya kuwawezesha wananchi kuongeza kipato na kuchangia kwa vitendo katika maendeleo ya taifa.
Amewataka Watanzania kutumia fursa ya mafunzo ya VETA kama njia ya kujiendeleza na kuvuka mipaka ya kifikra kuhusu ajira.
Katika hatua nyingine, Nombo amepongeza Bodi ya VETA kwa juhudi zao za kuendeleza bunifu zenye tija ambazo zinajibu moja kwa moja mahitaji ya jamii.
Amesema ubunifu wa VETA una mchango mkubwa katika kujenga taifa lenye watu wabunifu, wenye ujuzi, na wenye uwezo wa kutatua matatizo kwa njia endelevu.
Kwa sasa, VETA inaendelea kuonesha mwelekeo mpya wa elimu ya ujuzi nchini, ikiweka msingi wa uchumi wa viwanda na maendeleo ya kijamii yanayojengwa juu ya maarifa na ubunifu wa ndani.

You Might Also Like

Ujenzi Jengo la Sayansi, Teknolojia, Ubunifu Kuanza Kesho Dodoma

TSB yaanzisha ‘special’ Mkonge BBT

Ridhiwani Ashiriki Mazishi Ya Mwenyekiti SHIVYAWATA

Rafiki Mkubwa wa Trump, Elon Musk atanufaika vipi baada ya kumuunga mkono?  

Serikali  Kuja Na Mradi  Wa Kuimarisha Upatikanaji Umeme Vitongojini- Kapinga 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Profesa Nombo Atembelea Banda la UDSM, 88 Dodoma
Next Article Tanzania Kujenga Kiwanda Kikubwa cha Mbolea kwa Ushirikiano na Zambia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Dodoma Yang’ara Katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani
Habari August 8, 2025
Samia, Nchimbi Kuchukua Fomu Ya Urais Kesho
Habari August 8, 2025
Mgombea Udiwani Manyoni Adhalilishwa, Rushwa Yadaiwa Kuvuruga Kura Za Maoni
Habari August 8, 2025
TOSCI: Mbegu Bora Ni Ajira, Biashara
Habari August 8, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?