MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii
Habari

Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Lucy Ngowi
DODOMA: WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano ya Kazi), Deus Sangu, amesema kuna upungufu mkubwa wa maofisa katika dawati la jinsia nchini, ambapo kwa sasa wapo maofisa wanne tu.
Akizungumza katika Kongamano na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Tanzania (TASWO), Sangu amesema serikali inaendelea kukabiliana na changamoto ya upungufu wa wataalamu hao, hususan katika sekta ya elimu.
Aidha, amewataka wataalamu wa ustawi wa jamii kuzingatia maadili ya taaluma yao, akisisitiza kuwa wao ni tegemeo muhimu kwa makundi yenye uhitaji maalum, yakiwemo watoto waliofanyiwa ukatili pamoja na familia zenye migogoro.
Amesisitiza pia umuhimu wa kuimarisha maadili hayo sambamba na kuhakikisha kunakuwa na usambazaji sawa wa wataalamu wa ustawi wa jamii nchini.
Sangu ameeleza kuwa changamoto hiyo inahitaji ushirikiano wa wizara mbalimbali, ikiwemo Wizara ya Elimu pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto.
Vilevile, amewahimiza wataalamu hao kutumia mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha ukusanyaji na usimamizi wa taarifa.
Amebainisha kuwa hadi kufikia mwisho wa mwaka 2025, serikali ilikuwa imeajiri maofisa ustawi wa jamii 1,724, hatua iliyosaidia kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi hadi ngazi ya kata na vituo vya afya.
Hata hivyo, ameeleza kuwepo kwa changamoto ya usambazaji usio sawa wa wataalamu hao, ambapo asilimia 34 wamejikita katika makao makuu, huku zahanati zikiwa na asilimia 4.29 pekee.
Kwa upande mwingine, amesema serikali inaendelea na mchakato wa kuandaa Sheria ya Taaluma ya Ustawi wa Jamii, ambayo inalenga kulinda hadhi ya taaluma hiyo pamoja na kuboresha mazingira ya kazi na maslahi ya wataalamu wake.
Ameongeza kuwa ajira zitaendelea kutolewa kulingana na uwezo wa bajeti, zikilenga zaidi maeneo yenye upungufu mkubwa kama zahanati na kata.
Sangu amewataka wataalamu wa ustawi wa jamii kuimarisha mahusiano ndani ya jamii ili kudumisha amani na utulivu.

You Might Also Like

Salum Mwalim: Hakuna Mtu, Taasisi Inayoweza Kuzuia Uchaguzi

Rais Samia Afungua Barabara Ya Mbinga-Mbamba Bay Yenye Km 66-Ruvuma

Ridhiwan Atembelewa Na Watendaji NMB

Waziri Mkuu Asisitiza Elimu ya Bima ya Afya kwa Wote Vijijini

Majaliwa Amwakilisha Rais Samia Kwenye Kilele Cha Siku Ya Utumishi Wa Umma

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Italia Yahimiza Ubunifu Wa Bidhaa Za  Sanaa Za Vioo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Italia Yahimiza Ubunifu Wa Bidhaa Za  Sanaa Za Vioo
Habari March 28, 2026
Randama Ya Maji 2026/27 Yaidhinishwa
Habari March 27, 2026
PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini
Habari March 26, 2026
UNFPA,Wadau Washauri Kuimarisha Usalama Wa Kidigitali Kukabiliana na Ukatili Wa Jinsia Mtandaoni
Habari March 26, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?