MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UNFPA,Wadau Washauri Kuimarisha Usalama Wa Kidigitali Kukabiliana na Ukatili Wa Jinsia Mtandaoni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UNFPA,Wadau Washauri Kuimarisha Usalama Wa Kidigitali Kukabiliana na Ukatili Wa Jinsia Mtandaoni
Habari

UNFPA,Wadau Washauri Kuimarisha Usalama Wa Kidigitali Kukabiliana na Ukatili Wa Jinsia Mtandaoni

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
SERIKALI imesema  ukatili wa kijinsia unaendelea kuwa moja ya changamoto kubwa za haki za binadamu nchini, huku takwimu za kitaifa zikionesha kuwa asilimia 39.5 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 wamewahi kukumbwa na ukatili wa aina mbalimbali ikiwemo wa kimwili, kihisia na kingono kutoka kwa wenza wao.
Aidha wadau wameshauri kuimarisha Kwa usalama wa kidigitali na kushuhulikia  ukatili wa kijinsia kupitia teknolojia ( TFGBV) Ili kuruhusu wanawake na wasichana kushiriki kikamilifu katika elimu,fursa za kiuchumi,uongozi ma Maisha ya kiraia.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watu wenye Ulemavu Zanzibar, Abeda Rashid Abdallah  amesema hayo Dar es Salaam wakati akizungumza katika mkutano wa kitaifa kuhusu viashiria vya ukatili wa kijinsia vinavyofanyika kupitia teknolojia (TFGBV).
Habari Picha 11588
 Mkutano huo umeandaliwa na Shirika la kimataifa linaloshughulika na idadi ya watu (UNFPA )kwa kushirikiana na  Shirika la C-Sema, ukilenga kuimarisha hatua za Tanzania katika kukabiliana na ongezeko la ukatili wa kidijitali dhidi ya wanawake na watoto.
Akifafanua zaidi, Abeda amesema kuwa ukatili wa kijinsia unaowezeshwa na teknolojia ni tatizo linalokua kwa kasi, likijumuisha vitendo kama usambazaji wa picha za faragha bila ridhaa, unyanyasaji wa kingono mtandaoni, vitisho vya kidijitali, lugha za chuki na matusi.
Habari Picha 11589
Amesisitiza kuwa vitendo hivyo vinaathiri kwa kiasi kikubwa ustawi wa kisaikolojia na kijamii wa waathirika, hususan wanawake na wasichana.
Aidha, ameongeza kuwa zaidi ya nusu ya wanawake vijana wamewahi kukumbana na unyanyasaji mtandaoni, hali inayotia wasiwasi mkubwa katika kipindi hiki ambacho matumizi ya teknolojia yanaongezeka kwa kasi nchini.
Mwakilishi Mkazi wa UNFPA nchini Tanzania, Melissa Barrett ameeleza kuwa teknolojia inapaswa kuwa chombo cha kuwawezesha watu badala ya kuwa jukwaa la kuumiza huku akisisitiza kuwa kadri upatikanaji wa intaneti unavyozidi kuongezeka, ni lazima kuwepo na hatua madhubuti za kuhakikisha wanawake na wasichana wanatumia nafasi za kidijitali kwa usalama bila hofu ya kunyanyaswa.
“Ni muhimu ubunifu wa  Kidigitali kuchangia usawa wa kijinsia na ulinzi wa haki za binadamu,”amesema Mellissa.
Kwa upande wake, Balozi wa Finland nchini Tanzania, Theresa Zitting amesema kupitia ushirikiano uliopo kati ya serikali ya Finland, UNFPA na serikali ya Tanzania, wamejizatiti kushiriki utaalamu wa kimataifa katika maeneo ya utawala wa kidijitali, usalama wa mtandao na matumizi ya teknolojia yenye kuzingatia maadili ambapo juhudi hizo zinalenga kuhakikisha maendeleo ya teknolojia yanachangia kukuza usawa wa kijinsia badala ya kuongeza pengo la ukatili.
Kwa upande wake Ofisa program za jinsia kutoka UNFPA Ally Ahmad amesema mkutano huo una umuhimu mkubwa katika kuleta uelewa wa pamoja kuhusu changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia unaochochewa na matumizi ya teknolojia nchini Tanzania.
 Kupitia majadiliano ya wadau mbalimbali, ikiwemo serikali, taasisi za kimataifa kama UNFPA, wataalamu wa teknolojia na wanajamii

You Might Also Like

Taska Mbogo Aitaka Serikali Kurejesha Viwanda, Kuimarisha Kilimo

Ridhiwani Aiagiza CMA Kushughulikia Migogoro Kwa Haraka, Ufanisi

FAJ Yataka Wahamiaji Wa Kazi Wa Afrka, Wanaokwenda Maeneo Mengine Walindwe

Kamishna TFS Aongoza Kikao Cha Viongozi Wa Kamisheni ya Misitu Afrika

Kamati Ya Bunge  Yaridhishwa Na Ujenzi Wa Jengo La Kituo Cha Zimamoto, Mtumba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TPHPA Yapeleka Wadudu 4,252 Ziwa Victoria Kudhibiti Gugu la Kariba
Next Article PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii
Habari March 28, 2026
Italia Yahimiza Ubunifu Wa Bidhaa Za  Sanaa Za Vioo
Habari March 28, 2026
Randama Ya Maji 2026/27 Yaidhinishwa
Habari March 27, 2026
PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini
Habari March 26, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?