MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ulega : Nimeridhisha Na Hatua Iliyofikiwa, Ongezeni Kasi Zaidi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ulega : Nimeridhisha Na Hatua Iliyofikiwa, Ongezeni Kasi Zaidi
Habari

Ulega : Nimeridhisha Na Hatua Iliyofikiwa, Ongezeni Kasi Zaidi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: WAZIRI  wa Ujenzi Abdallah Ulega, ameridhishwa na ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Jiji la Dodoma yenye kilomita  112.3, ambayo utekelezaji wake umefikia  zaidi ya asilimia 85.
Ulega amesema hayo wakati akikagua mradi huo ambapo  amewaagiza wataalam wa Wakala wa Barabara (TANROADS) kuhakikisha wanawasimamia Makandarasi wa mradi huo kukamilisha kwa wakati na ubora.
“Nimekagua na nimeridhishwa na hatua zilizofikiwa katika awamu zote mbili na malengo ya Serikali ni kuwa mradi huu ukamilike kwa wakati na nimeelekeza wataalam kutoka TANROADS hadi kufikia mwezi Juni wawe wamefika asilimia 90,” amesema.
Pia amesema serikali inatarajia kujenga barabara ya njia nne na sita kuanzia Chamwino Ikulu hadi katikati ya jiji hilo  ambapo kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za manunuzi za kumpata mkandarasi.
Katika eneo la Ihumwa amesema serikali ina mpango wa kujenga barabara ya kisasa ya njia za kupishana, ili kuruhusu magari kupita katika mji wa Serikali wa Magufuli na yaendayo mjini bila kuwa na kizuizi chochote.
Vilevile, Waziri Ulega amezungumzia umuhimu wa Taasisi za TANROADS, Shirika la Reli Tanzania  (TRC ) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuwezesha mradi huo wa kimkakati kukamilika kwa wakati.
Katika hatua nyingine amesema ujenzi wa miundombinu ya barabara  za juu maeneo ya Morocco na Mwenge jijini Dar es salaam, upo  kwenye mpango mzuri, Wizara inaendelea kukamilisha taratibu za kitaalam ili kuendelea na utekelezaji wa miradi hiyo.
“Nitumie fursa hii kuwaambia watanzania kwamba bado Serikali inayo mpango wa kuzijenga Flyover za Mwenge na Morocco na hatua iliyopo wataalam wameniambia wanakamilisha taratibu na wafadhili wa mradi JICA hadi kufikia mwezi Julai fedha za mkopo zitakuwa zishasainiwa,” amesema.
Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi,  Aloyce Matei amesema hadi kufikia Julai mwaka huu, matarajio yao ni kwamba fedha za mradi wa ujenzi wa barabara za juu za  Morocco na Mwenge zitasainiwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.
Naye, Mkurugenzi wa Miradi kutoka TANROADS, Japheson  Nnko amemhakikishia Waziri Ulega kuwa watasimamia Makandarasi hao kuhakikisha mradi wa mzunguko wa nje wa jiji la Dodoma unakamilika kwa ubora na wakati kama ilivyosainiwa kwenye mkataba.
Amebainisha  kuwa  mradi huo umegawanywa sehemu mbili ambapo Mkandarasi China Civil Engineering  Construction Corporation (CCECC) anayejenga sehemu ya Nala-Veyula-Mtumba-Ihumwa bandari kavu (km 52.3) anatarajiwa kukamilisha ifikapo mwezi Julai, 2025.
 Na Mkandarasi Avic International anayejenga sehemu ya Ihumwa bandari kavu-Matumbulu-Nala (km 60) anatarajiwa kukamilisha ifikapo  Agosti, 2025.

You Might Also Like

Mdau wa Maendeleo Goryo Ashinda Tuzo Ya Mlipa Kodi Bora

Mkurugezi Mkuu LATRA, Kamanda Ng’anzi Wafanya Ukaguzi Wa Kushtukiza Stendi Ya Magufuli

Dkt. Komba: Mfumo wa kidijitali utaleta tija kwa mkulima

Tunatekeleza Azma YA Rais Samia Kuwafikia Wananchi Waliojiajiri

Wastaafu Epukeni Matapeli Kwenye Mafao-PSSSF

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article UVCCM Yazindua Kampeni Ya Kutetea Ukweli, kutokomesha Upotoshaji, Uongo
Next Article Kilimo Yaomba Trilioni 1.24 Mwaka Wa Fedha 2025/26
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ushiriki Wa Tanzania Jukwaa La Dunia Waongeza Fursa Za Kimataifa Kukabiliana Na Maafa-Dk Yonaz
Habari June 3, 2025
Shinyanga Kunufaika Na Miradi Ya REA,Wauziwa Mitungi 13,000 Kwa Ruzuku
Habari June 2, 2025
SUA Chatumia Ngamia Mafunzo Ya Vitendo Kwa Wanafunzi
Habari June 2, 2025
Mama Mchumgaji TAG Zinga, Asheherekea Siku Ya Kuzaliwa Na Watoto Yatima, Mazingira Magumu
Habari June 2, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?