MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ujenzi Kiwanda cha Chumvi Waanza Lindi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ujenzi Kiwanda cha Chumvi Waanza Lindi
Habari

Ujenzi Kiwanda cha Chumvi Waanza Lindi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na mwandishi wetu Kilwa Lindi
WAZIRI wa Madini Anthony Mavunde amesema Ujenzi wa kiwanda cha kusafisha madini ya chumvi kinachojengwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) katika eneo la Lingaula Wilayani Kilwa ni utekelezaji wa ahadi ya serikali kwa wakulima wa chumvi.
Mavunde amesema kwa kueleza kuwa Rais Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara Mkoani Lindi alisema hayo, hivyo utekelezaji wake umeanza.
Ameyasema hayo alipotembelea eneo litakapojengwa kiwanda hicho ikiwa ni pamoja na kupokea rasmi Hati ya umiliki wa ardhi wa eneo hilo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
“Ninamshukuru Rais Samia kwa kusikia kilio cha wakulima wa chumvi juu ya ukosefu wa masoko ya uhakika, hatua iliyosababisha kutupa maelekezo ya kuhakikisha tunasimamia ujenzi wa kiwanda hiki haraka ili kutatua kero hiyo ya muda mrefu kwa wakulima wa chumvi  wa maeneo mengi nchini ikiwemo wa Mkoa wa Lindi.
“Rais alipokuja kwenye ziara yake katika Mkoa huu, moja kati ya mambo aliyoyasikia na kupokea ni kilio cha wazalishaji wa madini ya Chumvi, hivo ameagiza kiwanda cha chumvi kijengwe hapa,.
“Na niwaambie Rais anafuatilia suala hili la wazalishaji wa chumvi na hatua hii ni utekelezaji wa ahadi yake kwenu baada ya kusikia kilio chenu”
“Rais wetu anayodhamira kwa dhati ya kuwanyanyua wazalishaji wa madini ya chumvi ili waweze kupiga hatua, kama ilivyo kwa wachimbaji wa madini mengine nchini,” amesema.
Pia Waziri Mavunde ameiagiza STAMICO kufanya nafunzo ya namna bora ya kulima chumvi ili wazalishe yenye ubora unaofaa kabla ya Disemba mwaka huu.
Sambamba na hilo, Waziri Mavunde ameitaka STAMICO kuangalia uwezekano wa kuingia mikataba ya utatu kati yake, wazalishaji hao wa chumvi pamoja na mabenki ili wazalishaji wawezeshwe kupata mikopo nafuu hatimaye wazalishe chumvi ya kutosheleza uhitaji.
Awali, akitoa taarifa fupi kuhusu mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO DKt. Venance Mwasse amesema kuwa Chimbuko la Mradi huo ni Maendeleo ya utekelezaji wa mipango ya Shirika pamoja na Maagizo ya Rais Suluhu Hassan aliyeagiza kusaidia wachimbaji wadogo wakiwemo wa chumvi.
Dkt. Mwasse amesema mbali na Kiwanda hicho kuchenjua madini ya chumvi, pia kitakuwa kinatoa Shamba darasa kwa wakulima wa chumvi ili kuwajengea uwezo wa kuzalisha chumvi yenye ubora zaidi.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya STAMICO, Meja Jenerali Mstaafu Michael Isamuhyo alieleza kwamba mradi wa ujenzi wa kiwanda hicho unataraji kukamilika na kuanza uzalishaji Aprili, mwakani.
Amesema mtambo  umeshaagizwa kutoka nchini India na kulipiwa asilimia 50 ya gharama, na unatarajiwa kuwasili Mwezi Oktoba, 2024.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa Lindi, Zainab Telack amesema kuwa kukamilika kwa kiwanda hicho kutasaidia kufungua fursa sio tu kwa wakulima wa chumvi, bali kwa wananchi wa mkoa huo.

You Might Also Like

Tuwaombe Rais Samia, Mwinyi – Sheikh Swed

Masauni Akabidhi Polisi Magari 77

Apongeza watumishi kwa kutoa huduma bora kwa walimu

Watuhumiwa 25 Wa Makosa Ya Mtandao Wakamatwa Na Polisi

Rais Samia awasili Zimbabwe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Yonaz akabidhi boti ya doria kukabili vitendo vya kiuhalifu
Next Article Trilioni 11.5 Zimetumika Miradi Ya Maendeleo Kigoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?