MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tume Ya Mipango Yaelekeza Waandishi Wa Habari Kutoa Elimu Ya Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tume Ya Mipango Yaelekeza Waandishi Wa Habari Kutoa Elimu Ya Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050
Habari

Tume Ya Mipango Yaelekeza Waandishi Wa Habari Kutoa Elimu Ya Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
TUME ya Taifa ya Mipango imewataka waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 ili kuhakikisha wananchi wote wanaitambua, wanaielewa na kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.
Wito huo umetolewa Jijini Dar es salaam mapema Agosti 19,2025 na Naibu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo anayeshughulikia Mipango ya Kitaifa
Dkt Mursali Milazi wakati akifungua mafunzo kwa waandishi wa habari yalioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu Duniani (UNFPA) kwa kushirikiana na Tume hiyo.
Amesema Vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata uelewa sahihi kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
“Utekelezaji  wa Dira hii utaanza rasmi katika mwaka wa fedha 2026/2027…
kutekeleza Dira ni hatua moja, lakini kuwaandaa wananchi na wadau mbalimbali kuelewa na kushiriki utekelezaji wake ni hatua muhimu zaidi.”amesema Dkt Milazi
Habari Picha 9062
Amesisitiza  kuwa serikali imejipanga kikamilifu kwa ajili ya utekelezaji wa Dira hiyo kwa kuandaa mifumo ya usimamizi na uwajibikaji, ambayo itasimamiwa na Tume ya Mipango ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati.
“Dira hii ni ya kwetu sote, hivyo kila Mtanzania anatakiwa aweze kuelewa kwa undani. Mwananchi wa kawaida akiulizwa, mahali popote alipo, awe na majibu ya msingi kuhusu malengo na mwelekeo wa nchi yetu hadi 2050,” ameongeza Dkt  Milazi.
Kwa upande wake Msimamizi wa Kitengo cha Idadi ya watu na Maendeleo kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Idadi ya watu Duniani (UNFPA) Samweli Msokwa amesema  kuwa ushiriki wa vijana, wanawake na makundi maalumu ni muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050, ambayo imeandaliwa kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Mipango.
Amesema shirika hilo limekuwa likishirikiana kwa karibu na Serikali katika nyanja mbalimbali, ikiwemo usimamizi wa uzalishaji wa takwimu na data muhimu za maendeleo na kuzisambaza kwa jamii kwa matumizi sahihi ya sera na mipango.
“Katika  hatua za awali za maandalizi ya Dira hii, UNFPA ilishirikiana na Serikali kufikisha maudhui ya dira kwa makundi mbalimbali, ikiwemo waandishi wa habari ili kusaidia kufikisha elimu kwa wananchi.”amesema
Na kuongeza kuwa
“Waandishi wa habari ni kundi muhimu katika kuwaelimisha wananchi kuhusu Dira hii. Wananchi ndio watekelezaji wakuu, hivyo elimu yao ni msingi wa mafanikio ya Dira,” amesema Msokwa
Aidha, alisisitiza kuwa vijana wanapaswa kuielewa vyema Dira ya 2050 ili waweze kutambua fursa zilizopo, kujifunza na kuwa sehemu ya mabadiliko ya maendeleo nchini.
Habari Picha 9071

You Might Also Like

Ushirikiano Wa Nchi Za Kiafrika Uthibitike Kwa Vitendo -Dkt. Biteko

 Rais Samia aipongeza REA

Trump Amteua Mtendaji Mkuu White House, Safari Ya Kuunda Timu Yake

Miradi Ufungaji Mifumo Ya Umeme Jua 20,000 Mbioni Kuanza

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Umeme Jua Kuchoche Uchumi Maeneo Ya Vijijini
Next Article Warsha Ya Luban Yaleta Mapinduzi Ya Elimu Ya Ufundi Nchini Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?