MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TUGHE: Wafanyakazi wapewe haki ya kujiunga vyama vya wafanyakazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TUGHE: Wafanyakazi wapewe haki ya kujiunga vyama vya wafanyakazi
Habari

TUGHE: Wafanyakazi wapewe haki ya kujiunga vyama vya wafanyakazi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Yunge Kanuda
WAAJIRI wametakiwa kuwapa wafanyakazi wao haki ya kujiunga na Vyama Vya wafanyakazi kwa ajili ya kuleta tija katika maeneo ya kazi.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE), Hery Mkunda amesema hayo wakati wa ufunguzi wa semina ya Waajiri na Viongozi wa matawi wa chama hicho Jijini Arusha.
Mkunda amewataka waajiri kufanya hivyo kwa kuwa vyama vya wafanyakazi ni wadau muhimu katika kuchangia maendeleo ya Taasisi.
Amesema tokea mwaka 2018, chama hicho kimekuwa  na utaratibu wa kuandaa na kuratibu mafunzo ya pamoja yanayojumuisha washiriki toka Viongozi wa Matawi ya Chama na Mamlaka za Ajira au wawakilishi wao.
“Kwa niaba ya TUGHE niwashukuru sana Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE kwa kukubali kuwezesha na kushiriki mafunzo haya ambapo tayari matunda ya uwepo wa mafunzo haya ya kila mwaka yameanza kuonekana.
“Yameonekana kwa kuwa  migogoro baina ya Watumishi na Waajiri imepungua sana na pale ilipojitokeza imekuwa ikipata utatuzi kwa njia ya majadiliano mahala pa kazi,” amesema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TUGHE Taifa ambaye alikuwa ni mgeni rasmi, Joel Kaminyonge amesisitiza umuhimu wa kuhubiri wajibu na haki sehemu za kazi.
Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania ( ATE,), Suzanne Ndomba-Doran amesema mada ya haki za msingi za vyama vya wafanyakazi ni elimu muhimu kwa wanachama kwani wanapaswa kufahamu wajibu kwasababu hakuna haki bila wajibu.
Amesema vyama vya wafanyakazi vina wajibu mkubwa wa kuleta utulivu, ufanisi na ukuaji wa tija sehemu za kazi na kuboresha mazingira na mahusiano mazuri baina ya mwajiri na mfanyakazi.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi ( OSHA), amesema nchi inahitaji kuwa na nguvukazi yenye afya njema ili kuleta tija katika maeneo ya kazi hivyo nsuala la Afya na Usalama ni muhimu kuwa agenda endelevu .
Mafunzo hayo ya siku nne yamewakutanisha washiriki kutoka sehemu mbalimbali za kazi zikiwemo Wizara, Idara, Taasisi, Wakala wa Serikali, Mamlaka za Serikali, Bunge, Mahakama, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi za Afya za Serikali na zile za binafasi.
Mafunzo hayo yatahitimishwa kwa Washiriki kufanya utalii wa ndani kwa kupata fursa ya kutembelea hifadhi ya  Taifa Ngorongoro.

You Might Also Like

WDC Kuboresha Miradi Yake Ya Majengo

Tumeridhika na kazi za TTCL – Mwanaisha

Washauriwa Kutumia Mbegu Zinazokabiliana Na Mabadiliko Ya Tabia Nchi

BRELA Yazindua Baraza La Wafanyakazi

Si ruhusa kufuga, kuchunga, kuvua maeneo ya umwagiliaji

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article CPC chatambua juhudi za Rais Samia
Next Article Asilimia 86.2 ya Wanawake  wanajishughulisha na shughuli za madini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?