MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TUCTA: Vijana Ni Nguvu Kazi Ya Taifa, Watumie Fursa Kujijenga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TUCTA: Vijana Ni Nguvu Kazi Ya Taifa, Watumie Fursa Kujijenga
Habari

TUCTA: Vijana Ni Nguvu Kazi Ya Taifa, Watumie Fursa Kujijenga

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) limewataka vijana nchini kutambua nafasi yao kama nguvu kazi muhimu kwa maendeleo ya taifa, kuhakikisha wanazitumia fursa zilizopo kwa manufaa yao binafsi na kwa taifa kwa ujumla.
Naibu Katibu Mkuu wa TUCTA,  Rehema Ludanga, amesema hayo katika Kongamano la Siku ya Wafanyakazi Vijana ikiwa  ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Vijana na kuelekea kilele cha Mwenge wa Uhuru Lililofanyika Leo Oktoba 11, 2025 jijini Mbeya.
Amesema vijana wanapaswa kuwa na uelewa mpana kuhusu fursa zinazowazunguka.
“Ni lazima vijana wawe na uwezo wa kutathmini mazingira yao na kutambua fursa mbalimbali ambazo zinaweza kuwa chachu ya maendeleo kwao na kwa taifa. Sisi tunawategemea kuziba mianya ya ajira na nafasi zilizoachwa wazi ili kujenga kesho iliyo bora,” amesema Ludanga.
Ameongeza kuwa moja ya changamoto kubwa zinazolikabili taifa kwa sasa ni mabadiliko ya tabianchi, ambayo yanaathiri sekta muhimu kama kilimo na madini.
Habari Picha 9909
Hali hiyo, amesema, inaweza kusababisha kupotea kwa baadhi ya ajira, hivyo vijana wanapaswa kujiandaa kwa kujifunza ujuzi mbadala.
“Katika kipindi hiki cha mpito, ni muhimu vijana kutumia muda wao mwingi kujifunza kazi na ujuzi mbadala zitakazowawezesha kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi,” amesema.
Aidha, ameeleza kuwa kongamano hilo lililolenga kuwakutanisha vijana lilikuwa na dhamira ya kuwakumbusha walikotoka, walipo na wanakotaka kuelekea, sambamba na kuweka mikakati ya kujijenga kwa faida yao, familia na taifa.
Habari Picha 9908
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Benno Malisa, amewahimiza vijana kutumia muda wao kwa kujitathmini na kujiuliza serikali inafanya nini kuwawezesha kujitegemea.
“Leo hii mnapigania marupurupu na mishahara kuongezeka. Sawa, lakini mnapoyapata mnapanga vipi matumizi yenu? Je, yanawatosheleza na kuwajenga au yanawabomoa?” amehoji Malisa.
Habari Picha 9912
Maadhimisho ya Wiki ya Vijana hufanyika kila mwaka yakilenga kutoa elimu, kuhamasisha ushiriki wa vijana katika maendeleo na kuwajengea uwezo wa kutumia fursa zilizopo kwa manufaa ya taifa.

You Might Also Like

COSOTA Yapokea Migogoro 136 Ndani Ya Miaka Minne

Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika

Miradi iliyokamilika ianze kutoa huduma- Nyamoga

Kassim Majaliwa Mgeni Rasmi Miaka 30 VETA

Polisi Dar Wakamata Magari 15  Yasiyo na Usajili Rasmi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TTCL Kuboresha Mifumo Kwa Kutumia Teknolojia Za Kisasa
Next Article Serikali Yajipanga Kuinua Maisha ya Vijana, Yaahidi Mabadiliko Kupitia Sera, Sheria
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?