MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TSB Yatangaza Fursa Za Kilimo, Uwekezaji Wa Mkonge
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TSB Yatangaza Fursa Za Kilimo, Uwekezaji Wa Mkonge
Habari

TSB Yatangaza Fursa Za Kilimo, Uwekezaji Wa Mkonge

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
Katika Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) imeelezea fursa zilizopo katika tasnia ya mkonge.
Akizungumza katika maonyesho hayo, Mkuu wa Sehemu ya Masoko na Uhamasishaji kutoka Bodi ya Mkonge Tanzania, David Magali amesema lengo la ushiriki wao ni kutoa elimu kwa wadau wa mkonge pamoja na kutangaza fursa zilizopo katika mnyororo mzima wa thamani wa mkonge.
“Tuko hapa kuwahamasisha Watanzania kujiingiza kwenye kilimo cha mkonge, uzalishaji wa mbegu, uchakataji wa mkonge pamoja na utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na mkonge.
“Tunaelimisha namna ya kuzalisha mkonge unaokidhi soko la ndani na la kimataifa,” amesema Magali.
Amesema tofauti na mazao mengine, mkonge hauhitaji uangalizi mkubwa, na kwa sasa soko lake ni la uhakika kutokana na mahitaji ya kimataifa kuongezeka.
“Fursa ipo wazi kwa vijana, wanawake na wawekezaji kuingia kwenye kilimo cha mkonge. Ni zao lisilo na changamoto nyingi, lakini lina tija kubwa,” amesema.
Ofisa Kilimo Mwandamizi kutoka Bodi ya Mkonge, Emanuel Lutego amesema ongezeko la wakulima wanaojihusisha na mkonge limechochea hitaji kubwa la mbegu bora.
“Hii ni fursa ya wazi kwa watu binafsi na mashirika kuwekeza kwenye uzalishaji wa mbegu za mkonge ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka kila siku,.
“Tunawakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza kwenye mashine za kuchakata mkonge. Lengo letu ni kuongeza uzalishaji wa mkonge hadi kufikia tani 120,000 kwa mwaka, na hilo linawezekana tu tukiongeza uwezo wa uchakataji,” amesema.
Amesema tasnia ya mkonge haimalizii tu kwenye uzalishaji wa nyuzi kwani kuna fursa pana ya kutengeneza bidhaa mbalimbali zitokanazo na mkonge, kama vile mikoba, kamba, mazuria, viatu na hata vipodozi vinavyotumia malighafi ya mkonge.
TSB kupitia vituo vyake vya ubunifu vilivyopo Tanga na Zanzibar, inakaribisha wabunifu na wakufunzi kushiriki katika kutoa mafunzo na kuanzisha viwanda vidogo vya bidhaa zitokanazo na mkonge.
 “Hii ni fursa ya kipekee kwa wale wenye mawazo bunifu. Tuna mazingira mazuri ya kuwasaidia kubuni na kutengeneza bidhaa bora kwa soko la ndani na nje,” amesena.
Bodi ya Mkonge inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha elimu ya uzalishaji bora, ufugaji wa mbegu, na uendelezaji wa viwanda inawafikia walengwa kwa ufanisi.

You Might Also Like

Samia Kukagua Barabara Ya Mzunguko, Uwanja Wa Ndege Msalato Kesho

Washauri Somo la Astronomia Kurudishwa Mashuleni, Kukuza Utalii Anga

Matumizi Holela Ya Vilevi Hatari Kwa Watumiaji

Mpogolo Aipongeza Halmashauri Maandalizi Mikopo Asilimia 10

Profesa Ndunguru: Teknolojia ya Vinasaba Yafungua Ukurasa Mpya Katika Kilimo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Elimu Ya Dawa Za Kulevya Kutolewa Kwa Wanafunzi
Next Article Waendelezaji Majengo 103 Kesi Ziko Mahakamani, -AQRB
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?