MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Habari

TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
BODI ya Mkonge Tanzania (TSB) imesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika uchakataji wa mkonge ili kuongeza tija na kufikia lengo la taifa la kuzalisha zaidi ya tani 120,000 kwa mwaka.
 Ofisa Udhibiti Ubora  Emmanuel Lutego, amesema hayo katika maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama sabasaba yanayoendelea Dar es Salaam.
Amesema Serikali kupitia bajeti yake ya mwaka uliopita imesambaza zaidi ya miche milioni mbili kwa wakulima, na sasa tatizo lililopo ni uhaba wa mashine za kuchakata mkonge,.
Ameongeza kuwa katika mwaka huu wa fedha, serikali inatarajia kusambaza mashine 10 za uchakataji katika maeneo mbalimbali ili kupunguza changamoto hiyo na kuongeza uzalishaji wa mkonge bora, unaokubalika katika soko la dunia.
Mbali na nyuzi, Lutego amebainisha kuwa mabaki ya mkonge hutumika pia kuzalisha bidhaa nyingine zikiwemo mbolea, chakula cha mifugo, uyoga, na nyuzi chuma, hivyo kuongeza thamani ya zao hilo kwa namna nyingi.
Tanzania inatajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazozalisha mkonge bora duniani, na juhudi za Bodi ya Mkonge ni kuhakikisha sifa hiyo inalindwa na kuendelezwa kwa kutumia teknolojia na kuzingatia viwango vya ubora
Mkuu wa Sehemu ya Masoko na Uhamasishaji, David Maghali amesema TSB imetumia Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam  maarufu kama Sabasaba kwa kuwataka Watanzania kuchangamkia kilimo  Cha mkonge kwani kina  tija na soko la uhakika la  kimataifa.
  Amesema uwepo wao kwenye maonesho hayo ni kwa ajili ya kuwaelimisha wadau kuhusu fursa za kilimo na biashara ya mkonge, pamoja na kuhamasisha ushiriki mpana zaidi wa Watanzania katika sekta hiyo.
Amesema wanatoka  elimu juu ya uzalishaji bora wa mkonge ili kuhakikisha kinachozalishwa kinakidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.
“Lengo letu ni kuona wakulima wanazalisha bidhaa zenye ubora ambazo zinanunulika moja kwa moja sokoni,” amesema.
Amesema Tanzania imejaliwa kuwa na ardhi bora kwa kilimo cha mkonge, hivyo ni muhimu kwa wananchi kuitumia fursa hiyo kwa kuwekeza kwenye kilimo hicho ambacho hakina changamoto nyingi na kina soko la uhakika duniani.
“Fursa nyingine ni katika uzalishaji wa mbegu za mkonge, kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya miche miongoni mwa wakulima ambayo ni nafasi ya Watanzania kuanza kuzalisha mbegu kwa ajili ya biashara,” amesema.
Aidha, ametaja uanzishaji wa vituo vya uchakataji kuwa ni fursa muhimu, akisema kwa sasa mkonge hauuziwi kama majani bali kwa mfumo wa nyuzi, hivyo ni muhimu kwa wawekezaji kuwekeza kwenye mashine za kuchakata mkonge ili kuongeza thamani ya zao hilo.
Amesema jambo kubwa wanalofanya  ni kuhakikisha uzalishaji unalingana na mahitaji ya soko.
“Tuna kituo cha atamizi Tanga kinachotoa mafunzo ya utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na mkonge kama mikoba, mikeka na bidhaa za ufumaji,” amefafanua.
.

You Might Also Like

Samia: Sera Iliyozinduliwa, Somo La Ujasiriamali Ni Lazima

Tanzania Kushirikiana na Finland Uboreshaji Mbegu za Miti

Kampeni ya Mama Samia imewafikia zaidi ya watu 4000 mikoa saba

Watanzania Washauriwa Kula Senene, Kumbikumbi, Msusa, Ngogwe Kuepuka Udumavu

Mipango Zaidi Msiba Wa Cleopa Msuya Kutolewa Na Serikali

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi
Next Article Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Habari July 10, 2025
eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi
Habari July 10, 2025
July 10, 2025
Habari July 10, 2025
Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa
Habari July 10, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?