MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TPHPA Tuna Mchango Mkubwa Katika Utoshelevu Wa Chakula – Ndunguru
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TPHPA Tuna Mchango Mkubwa Katika Utoshelevu Wa Chakula – Ndunguru
Habari

TPHPA Tuna Mchango Mkubwa Katika Utoshelevu Wa Chakula – Ndunguru

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), ina mchango mkubwa katika utoshelevu wa chakula kwa asilimia 128 kwa kudhibiti visumbufu vya mazao ambavyo vingeweza kuathiri uzalishaji wa mazao hayo.

Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Profesa Joseph Ndunguru amesema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya ya Mimea Mei 12, mwaka huu 2025 katika Viwanja vya Makumbusho ya Azimio La Arusha mkoani Arusha.

Ametolea mfano wa jinsi mamlaka hiyo ilivyofanikiwa kudhibiti baa la panya katika mikoa 16, wilaya 54, kata 540 na kuokoa jumla ya ekari 358,895 za mazao ikiwemo mahindi.

“Hadi kufikia Aprili 2025 TPHPA imefanya udhibiti wa ndege aina ya kwelea kwelea milioni 200.7 katika hekta 220,163 za halmashauri 18 na kuokoa zaidi ya tani 1,463,445, ikiwemo mpunga, uwele na mtama.

“Kudhibiti viwavi jeshi katika hekta 83,180 na kuokoa zaidi ya tani 332,732 za mazao ya nafaka ikiwemo mahindi katika mashamba mbalimbali.

“Kudhibiti Nzige ekari 1340 waliovamia wilaya ya Mpwapwa mkoa wa Dodoma, pamoja na nzige wekundu milioni 36 waliovamia ekari 405 wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida,” amesema.

Pia amesema mamlaka hiyo imewezesha ufunguaji wa Masoko Mapya ya mazao ya kilimo Nje Ya Nchi.

“Mamlaka imewezesha ufikiaji wa masoko kwa mazao tisa ya kipaumbele katika nchi 14. Kati ya Mazao tisa yaliyohusika katika ufunguzi wa masoko Kimataifa, na Nchi husika yanakosafirishwa,” amesema.

Ametaja mazao hayo kuwa ni Vanilla yanasafirishwa China, Indonesia na India. Parachichi yanasafirishwa Canada, Malaysia, Afrika Kusini, India, China na Umoja wa Ulaya, Israel.

Pia ndizi zinasafirishwa Afrika Kusini, Viazi mviringo nchini Zambia,Kahawa na soya nchini China, Nanasi China, India, uturuki na Brazil.

Vile vile Karafuu Indonesia na Singapore, Pilipili Manga nchini Canada, Kakao nchini Marekani, Tumbaku nchini Iraki na Pakistan.

Pia TPHPA imefanikiwa kufungua masoko mapya ya parachichi nchini Afrika Kusini, India na China, Soya nchini China, Mashudu, Pamba na Alizeti nchini China na mahindi ya njano nchini Misri.

Amesema biashara hiyo ya mazao ikifanyika itaingizia Tanzania kiasi cha dola za kimarekani bilioni 3.5 kwa mwaka.

You Might Also Like

China Inaongoza Sekta ya Miundombinu na Ujenzi Tanzania

Faru Weusi, Simba, Tembo Waongezeka Ngorongoro

Waziri wa Vijana akutana na Mwita wa Zanzibar

BUWSSA Yapewa Bilioni 28 Kutatua Tatizo La Maji

Serikali Yaweka Mkazo Kukuza Tasnia Ya Ufugaji Wa Kuku

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Profesa Ndunguru: Tumewezesha Usafirishaji wa Mazao Mbalimbali Yenye Thamani ya Trilioni 15.6
Next Article TPHPA Yaelezea Vipaumbele Vyake
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Bodi Ya Wadhamini Ya NSSF Yaridhishwa Na Uwekezaji Wa Ubia Na Jeshi La Magereza
Habari May 14, 2025
TPHPA Yaelezea Vipaumbele Vyake
Habari May 14, 2025
Profesa Ndunguru: Tumewezesha Usafirishaji wa Mazao Mbalimbali Yenye Thamani ya Trilioni 15.6
Habari May 14, 2025
Daraja La Magufuli Laimarisha Uhusiano Wa Jumuiya Ya China,Tanzania Yenye Mustakabali Wa Pamoja
Makala May 14, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?