MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TEA Yaweka Mikakati Madhubuti Kukuza Mafunzo ya Amali Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TEA Yaweka Mikakati Madhubuti Kukuza Mafunzo ya Amali Nchini
Habari

TEA Yaweka Mikakati Madhubuti Kukuza Mafunzo ya Amali Nchini

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) imeweka mikakati thabiti ya kutekeleza miradi ya ujenzi na uboreshaji wa mazingira ya kujifunzia kwa vitendo katika shule na vyuo vya mafunzo ya amali nchini.
Mikakati inayolenga kuboresha elimu ya amali na kuwawezesha vijana kujiajiri.
Mwenyekiti wa Bodi TEA, Dkt. Leonard Akwilapo amesema hayo katika Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yajulikanayo kama Saba Saba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.
Amesema Mamlaka hiyo imepewa fedha za kutosha ili kutekeleza miradi hiyo muhimu katika shule teule zinazotoa mafunzo ya amali.
“Tumepewa fedha za kutosha kwa ajili ya kutekeleza miradi katika shule teule zinazotoa mafunzo ya amali,” amesema Dkt. Akwilapo.
Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuiwezesha TEA kupitia Mfuko wa Elimu wa Taifa  ambao umekuwa kichocheo kikuu cha mageuzi katika sekta ya elimu nchini, hususan katika kukuza ujuzi na uwezo wa kujitegemea kwa vijana.
Mamlaka hiyo inatekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya elimu ya amali kama vile karakana, madarasa ya vitendo, mabweni na vifaa vya kisasa vya kujifunzia, sambamba na kutoa ufadhili wa mafunzo kupitia Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF).
Hadi sasa, maelfu ya vijana wamenufaika na mafunzo hayo na wameweza kujiajiri katika sekta mbalimbali ikiwemo useremala, umeme, uashi, ushonaji na ICT.
Katika maonyesho hayo ya kimataifa, TEA inalenga kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kupanua wigo wa huduma zake na kusambaza elimu kwa umma kuhusu mipango ya kukuza elimu ya amali nchini.
Kupitia ushiriki wake katika Maonyesho ya Saba Saba, TEA inasisitiza dhamira yake ya kuandaa mazingira bora ya elimu ya vitendo ili kuhakikisha Tanzania inazalisha nguvu kazi yenye ujuzi wa kutosha kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

You Might Also Like

Ridhiwan Kikwete Apongeza Halmashauri Ya Tunduma

Walimu Wanaofundisha Lugha Ya Kichina Tanzania Wakutana

Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati

TEA Yakabidhi Miradi Iliyokamilika Wilayani Mtama, Masasi

Rais Samia awasili Zimbabwe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article BRELA Yatwaa Tuzo Sabasaba
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

BRELA Yatwaa Tuzo Sabasaba
Habari July 11, 2025
UDSM  Yakamilisha Utafiti Wa Dawa Ya Kusafisha Sumu Kwenye Maji
Habari July 11, 2025
Rafiki Planter’Teknolojia Rahisi, Tija Kubwa”
Habari July 11, 2025
Wazalishaji, Waagizaji Mbolea Watakiwa Kuzingatia Afya ya Udongo kwa Tija ya Kilimo
Habari July 11, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?