MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TARI Yabadilisha Kilimo kwa Teknolojia Mpya, Za Kisasa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TARI Yabadilisha Kilimo kwa Teknolojia Mpya, Za Kisasa
Habari

TARI Yabadilisha Kilimo kwa Teknolojia Mpya, Za Kisasa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: KATIKA Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yajulikanayo kama Sabasaba, Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) imeonyesha jinsi teknolojia na uvumbuzi vinaweza kubadilisha maisha ya wakulima na kuchochea maendeleo ya kilimo kwa ujumla.
Akizungumza na Mfanyakazi Tanzania katika banda la TARI, Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Dkt. Thomas Bwana amesema maonyesho hayo ni jukwaa muhimu la kukutana na wadau mbalimbali, hasa wakulima, wajasiriamali, na wafanyabiashara, kwa ajili ya kuonesha teknolojia mpya zinazotatua changamoto za sekta ya kilimo.
“Wajibu wetu mkubwa ni kuhakikisha tunaibua na kuendeleza teknolojia zitakazosaidia wakulima kuongeza tija, kupunguza gharama na kuongeza kipato,” amesema.
Amesema miongoni mwa uvumbuzi uliovutia wananchi  ni mashine ya ‘Rafiki Planter’, inayotumika kupanda mbegu za pamba kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa.
“Kwa kawaida, hekta moja ya pamba hupandwa na watu 10 hadi 16 ndani ya saa nane, lakini kwa mashine hiyo, kazi hiyo hufanyika kwa saa moja tu na mtu mmoja.
“Hii inamaanisha wakulima wanaweza kuwahi mvua, kupunguza gharama za kazi na kuongeza uzalishaji,” amesema.
Amesema kupitia tafiti za TARI, nafasi za upandaji wa pamba zimeboreshwa kutoka sentimita 90×40 hadi 60×30. Mabadiliko haya yameongeza idadi ya mimea kutoka 22,000 hadi zaidi ya 44,000 kwa hekta moja, na kuongeza mavuno kutoka kilo 1,200 hadi kati ya kilo 2,400 na 2,700 kwa hekta.
“Tija imeongezeka, na mara moja fedha zimeanza kuingia mfukoni mwa mkulima,” amesema.
Amesema taasisi hiyo pia ipo na mbegu bora za migomba zinazozalisha mikungu yenye hadi kilo 94, ikilinganishwa na wastani wa kilo 30 za migomba ya kawaida. Kwa upande wa mihogo, mbegu aina ya TARICASS 4 imeongeza uzalishaji karibu mara tano zaidi ya mihogo ya kawaida.
Amesena Katika eneo la kuongeza thamani, TARI imeonyesha matumizi mbadala ya mihogo, mtama, uwele na korosho.
“Mihogo sasa inaweza kutumika kutengeneza tambi, biskuti, mikate, na hata unga wa biashara badala ya kutegemea ngano pekee.
“Kwa korosho na karanga, taasisi imeonyesha teknolojia za kuongeza thamani kwa kutengeneza siagi, unga wa korosho, na bidhaa zilizoimarishwa kwa virutubisho.
“Mabibo ya korosho ambayo hapo awali yalionekana kuwa taka, sasa hutumika kutengeneza juisi, divai na hata ethanol kwa ajili ya vitakasa mikono,” amesema.
Amesema katika mazao ya nafaka kama mtama na ulezi, TARI imefanikiwa kutengeneza bidhaa kama maandazi, hatua inayochochea wajasiriamali kuibua bidhaa mpya sokoni huku wakulima wakinufaika kwa kuuza mazao yenye thamani zaidi.
Ametoa wito kwa wajasiriamali na wakulima kutembelea taasisi hiyo na kujifunza teknolojia mbalimbali zinazoweza kuwapatia fursa za biashara na kukuza kipato.
“Lengo letu ni kuhakikisha matokeo ya utafiti hayabaki makaratasi; tunataka yawe suluhisho la maisha ya Watanzania,” amesema.

You Might Also Like

TASU yaiomba serikali inunue kutoa ajira kwa mabaharia

RC Serukamba Aiunga Mkono REAUgawaji Wa Mitungi Ya Gesi Iringa

Asali inayozalishwa nchini kukidhi ubora wa kimataifa

SGR Kipande Cha Saba Na Nane kuanza kujengwa

Dar Sasa Kufanya Biashara Saa 24, Kuanza Februari 22 Mwaka Huu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article ‘Jichunge’ Programu Ya Simu Yenye Mafanikio Katika Kuboresha Matumizi Ya Dawa Kinga Dhidi Ya VVU
Next Article Wizara Ya Kilimo Yajipanga Vema Maonesho ya Kimataifa Ya Biashara
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?