MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.
Habari

SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi wetu
RAIS Samia Suluhu Hassan amezindua Soko la Madini ya Vito na Dhahabu Wilayani Tunduru ikiwa ni moja ya shughuli alizofanya akiwa katika ziara ya kikazi ya siku sita Mkoani Ruvuma.
Katika uzinduzi huo Samia ameipongeza
Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa utekelezaji wa Sera ya kushirikiana na sekta binafsi kwa vitendo.
“Ni dhahiri kwamba ujenzi wa soko hili kubwa na la kisasa utarahisisha biashara ya madini Wilayani hapa na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji maduhuli ya Serikali sambamba na kudhibiti udanganyifu na utoroshaji wa madini”, amesema.
Pia Rais Samia amepongeza ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali katika Mkoa wa Ruvuma ambapo alieleza kwamba kwa kipindi cha Julai na Agosti mwaka huu, zaidi ya Sh. Bilioni 6.5 zimekusanywa, hali inayoonyesha taswira nzuri ya makusanyo kadri muda unavyoendelea.
Vile vile Rais Samia amesisitiza kutambua mchango wa wachimbaji wadogo katika uchumi wa Taifa, na kumwelekeza Waziri wa Madini kuhakikisha STAMICO inawasimamia ipasavyo kuwaendeleza ili wanufaike na rasilimali hiyo.
Naye Waziri wa Madini Anthony Mavunde amesema mwaka wa fedha uliopita sekta ya madini ilikusanya na kuchangia kwenye mfuko mkuu wa Serikali Sh. Bilioni 753 ilhali kwa mwaka 2015/2016 Sh. Bilioni 161 pekee zilikusanywa.
“Maelekezo yako Rais ndiyo yamepelekea kwa mwaka 2023/2024 zaidi ya Sh. Trilioni 1.7 zizunguke kwenye masoko 43 na vituo vya ununuzi 102 nchi nzima kwenye biashara ya madini.
“Pamoja na mzunguko huo, sekta ya madini inaendelea kukua kwa kasi na kuchangia ukuaji wa vipato vya wananchi katika maeneo mbalimbali.
“Katika kipindi cha siku 84 za mwaka huu wa fedha yaani 2024/2025 tayari sekta ya madini imekusanya jumla ya Sh. Bilioni 225 na kuchangia katika mfuko mkuu wa Serikali, hii ni hatua kubwa katika maendeleo ya sekta ya madini na ukuaji wa uchumi wa Taifa letu” amesema.

You Might Also Like

ICGLR Yajipanga Kujiimarisha Amani Katika Kanda

MOI Yaokoa Bilioni 150 Matibabu Ya Kibingwa

VETA Mtwara Watua Na Mwani Maadhimishilo Ya Miaka 30

Spika Tulia Kufungua Kongamano La Uhuru Wa Wanataaluma Afrika UDSM

Wanawake Wang’aa Mchakato Uchaguzi Mkuu 2025

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article REA Yatoa Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi, Shule ya Samia
Next Article Profesa Mutembei apongeza serikali kuruhusu mchepuo lugha ya kichina
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?