MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.
Habari

SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi wetu
RAIS Samia Suluhu Hassan amezindua Soko la Madini ya Vito na Dhahabu Wilayani Tunduru ikiwa ni moja ya shughuli alizofanya akiwa katika ziara ya kikazi ya siku sita Mkoani Ruvuma.
Katika uzinduzi huo Samia ameipongeza
Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa utekelezaji wa Sera ya kushirikiana na sekta binafsi kwa vitendo.
“Ni dhahiri kwamba ujenzi wa soko hili kubwa na la kisasa utarahisisha biashara ya madini Wilayani hapa na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji maduhuli ya Serikali sambamba na kudhibiti udanganyifu na utoroshaji wa madini”, amesema.
Pia Rais Samia amepongeza ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali katika Mkoa wa Ruvuma ambapo alieleza kwamba kwa kipindi cha Julai na Agosti mwaka huu, zaidi ya Sh. Bilioni 6.5 zimekusanywa, hali inayoonyesha taswira nzuri ya makusanyo kadri muda unavyoendelea.
Vile vile Rais Samia amesisitiza kutambua mchango wa wachimbaji wadogo katika uchumi wa Taifa, na kumwelekeza Waziri wa Madini kuhakikisha STAMICO inawasimamia ipasavyo kuwaendeleza ili wanufaike na rasilimali hiyo.
Naye Waziri wa Madini Anthony Mavunde amesema mwaka wa fedha uliopita sekta ya madini ilikusanya na kuchangia kwenye mfuko mkuu wa Serikali Sh. Bilioni 753 ilhali kwa mwaka 2015/2016 Sh. Bilioni 161 pekee zilikusanywa.
“Maelekezo yako Rais ndiyo yamepelekea kwa mwaka 2023/2024 zaidi ya Sh. Trilioni 1.7 zizunguke kwenye masoko 43 na vituo vya ununuzi 102 nchi nzima kwenye biashara ya madini.
“Pamoja na mzunguko huo, sekta ya madini inaendelea kukua kwa kasi na kuchangia ukuaji wa vipato vya wananchi katika maeneo mbalimbali.
“Katika kipindi cha siku 84 za mwaka huu wa fedha yaani 2024/2025 tayari sekta ya madini imekusanya jumla ya Sh. Bilioni 225 na kuchangia katika mfuko mkuu wa Serikali, hii ni hatua kubwa katika maendeleo ya sekta ya madini na ukuaji wa uchumi wa Taifa letu” amesema.

You Might Also Like

Dkt. Komba: Mfumo wa kidijitali utaleta tija kwa mkulima

China Inaongoza Sekta ya Miundombinu na Ujenzi Tanzania

Biteko – Asisitiza Umuhimu Wa Mifumo Thabiti Ya Nishati Jadidifu Kukidhi Mahitaji Ya Nishati

Kassim Majaliwa Mgeni Rasmi Miaka 30 VETA

Majaliwa Ataka Yatolewe Mafunzo Yanayozingatia Soko La Ajira

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article REA Yatoa Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi, Shule ya Samia
Next Article Profesa Mutembei apongeza serikali kuruhusu mchepuo lugha ya kichina
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?