MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yaimarisha Mafunzo Ya Vitendo Kupitia Ushirikiano, Viwanda
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yaimarisha Mafunzo Ya Vitendo Kupitia Ushirikiano, Viwanda
Habari

Serikali Yaimarisha Mafunzo Ya Vitendo Kupitia Ushirikiano, Viwanda

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kujenga ushirikiano thabiti na endelevu kati ya taasisi za elimu na sekta za uzalishaji, kwa lengo la kuzalisha rasilimali watu wenye ujuzi, tija na ubunifu ili kuchochea maendeleo ya uchumi jumuishi.
Profesa Mkenda ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa ahadi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mafanikio yaliyopatikana ndani ya siku 100 za Serikali ya Awamu ya Sita, muhula wa pili.
Amesema miongoni mwa hatua zilizotekelezwa ni kuandaa na kutekeleza mpango wa pamoja kati ya Waajiri, Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA), vyuo vya kati na vyuo vikuu, unaolenga kulinganisha mafunzo yanayotolewa na mahitaji ya sekta za kipaumbele ikiwemo nishati, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na viwanda vya kuongeza thamani.
Ameeleza kuwa mpango huo umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi na umejengwa katika mfumo wa kiunzi, ambacho kitazinduliwa rasmi Februari 9, 2026 jijini Dar es Salaam.
Kupitia kiunzi hicho, wanafunzi wa VETA na vyuo vikuu watapata fursa ya kupata mafunzo kwa vitendo viwandani, hatua itakayosaidia kuziba pengo kati ya nadharia ya darasani na mahitaji halisi ya soko la ajira.
Profesa Mkenda amesema kiunzi hicho kimeoanishwa na sera na mikakati ya kitaifa ikiwemo Dira ya Taifa 2050.
Ameongeza kuwa kupitia miradi ya Mradi wa Kuboresha Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) na Mradi wa Kukuza Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ya Kikanda (EASTRIP), pamoja na ushirikiano na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Amali (NACTVET), tayari zimeanzishwa kamati za ushauri wa viwanda na mikataba ya ushirikiano kati ya vyuo na viwanda katika sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, ujenzi, utalii, madini, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) pamoja na huduma za biashara
Akizungumzia mafanikio mengine ndani ya siku 100, amesema Serikali imeongeza mikopo ya elimu ya juu na kati kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kwa wanafunzi zaidi ya 276,000, sambamba na utekelezaji wa Mpango wa Samia Scholarship uliowanufaisha zaidi ya wanafunzi 3,000 katika fani za sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati.
Aidha, ameongeza kuwa ujenzi wa shule maalum za sayansi kwa wasichana na shule za vipaji unaendelea, huku kampasi za vyuo vikuu zikijengwa na kukamilishwa katika mikoa mbalimbali nchini, hatua inayopanua fursa za elimu na mafunzo ya ujuzi kwa vijana.

You Might Also Like

DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda

Walimu Kupatiwa Mafunzo ya Tehama

CCM Kuwezesha Wananchi Kufuatilia Mkutano Mkuu Maeneo Ya Wazi

Mwigulu: Wavivu, Wazembe, Wala Rushwa Serikalini Jiandaeni Na Fyekeo

Madaktari Bingwa, Wauguzi Wabobevu Wa Mama Samia Watoa Mafunzo Ya Huduma Kwa Mama Na Mtoto, Hospitali Ya Wilaya Ya Singida

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanafunzi 571 watunukiwa Stashahada Na Astashaha Za Vyuo Vya Polisi
Next Article Serikali Kuwasilisha Bungeni Nyenzo Kuu Tatu Zitakazowezesha Utekelezaji Dira 2050
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari February 2, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?