MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari

Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MAKAMU wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua za makusudi kuimarisha uhuru wa Mahakama, ikitambua umuhimu wake katika ujenzi wa Taifa, ustawi wa wananchi na maendeleo endelevu.
Dkt. Nchimbi alisema hayo alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini, yaliyofanyika Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tambukareli jijini Dodoma.
Alisema Serikali itaendelea kushirikiana na Mahakama katika ujenzi wa miundombinu ya Mahakama, kuimarisha rasilimali watu, kuboresha maslahi ya watumishi wa Mahakama na kusogeza huduma za utoaji haki karibu zaidi na wananchi.
Habari Picha 11049
Alibainisha kuwa juhudi hizo zitatekelezwa hususan kupitia mpango wa ujenzi wa Mahakama za Mwanzo katika kata zote nchini ambazo bado hazina mahakama hizo.
Aidha, Makamu wa Rais alisisitiza kuwa uhuru wa Mahakama usitumike kuficha uzembe, upendeleo au vitendo visivyo vya haki.
Habari Picha 11050
Alisema uhuru huo ni dhamana ya kutenda haki kwa uadilifu, uwazi na kwa kuzingatia Katiba na Sheria za nchi.
Aliongeza kuwa Mahakama ina wajibu mkubwa wa kulinda utawala wa sheria, kusimamia utekelezaji wa mikataba, kulinda rasilimali za Taifa na kuhakikisha maendeleo yanayopatikana yanawanufaisha Watanzania wote kwa usawa.
Dkt. Nchimbi alisema Mahakama ina mchango muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050 kwa kuendelea kulinda haki na misingi ya Katiba, kuhakikisha migogoro ya kiuchumi, kibiashara na kijamii inatatuliwa kwa haraka na kwa haki, kujenga imani ya wananchi na wawekezaji katika mfumo wa kisheria, kukuza uwajibikaji na nidhamu katika sekta za umma na binafsi, pamoja na kudumisha amani na mshikamano wa kitaifa.
Habari Picha 11051
Aidha, alisema Mahakama ina wajibu wa kuzuia migogoro inayoweza kusababisha migawanyiko ya kijamii au kisiasa, kuharakisha utekelezaji wa sera na mipango ya maendeleo kwa kutoa tafsiri za kisheria zilizo wazi, kujenga utamaduni wa kuheshimu sheria na taasisi za umma, kupambana na rushwa na matumizi mabaya ya madaraka, pamoja na kuwezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa kwa kuhakikishiwa ulinzi wa haki zao za kisheria.
Katika hatua nyingine, Makamu wa Rais aliwaasa viongozi, wanasiasa, wanaharakati na wananchi kuheshimu tume iliyoundwa na Rais kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, kwa kuacha kuyajadili masuala hayo nje ya mfumo wa kisheria.
Kauli hiyo ilitolewa kufuatia ombi la Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi, aliyeomba viongozi kuacha kuzungumzia suala hilo kwa namna inayowaumiza wananchi.
Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania, George Masaju, alisema Mahakama inaendelea kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi wa utendaji.
Alisema Mahakama ipo katika hatua za mwisho za kujenga mfumo unaotumia Akili Unde (AI) kwa ajili ya kurekodi mwenendo wa mashauri na hukumu mahakamani.
Alifafanua kuwa kupitia mfumo huo, Jaji, Hakimu, Wakili na Shahidi wanapozungumza, mfumo utatafsiri na kuandika mazungumzo hayo kwa lugha iliyochaguliwa kwa wakati halisi.
Aliongeza kuwa matumizi ya mfumo huo yataondoa changamoto za ucheleweshaji na upotoshaji unaoweza kujitokeza wakati wa kuchukua kumbukumbu kwa kuandika kwa mkono au kutumia kompyuta.
Habari Picha 11052

You Might Also Like

Biteko Amwakilisha Rais Samia Harambee Ujenzi Kanisa Katoliki

China Inaongoza Sekta ya Miundombinu na Ujenzi Tanzania

Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari

TPHPA Yaelekeza Wakulima Kutumia Viuatilifu Kwa Usahihi

TARI Mlingano Yaleta Mapinduzi ya Mkonge, Viungo na Sayansi ya Udongo Tanzania

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbarawa Aitaka Jamii Kulinda Miundombinu ya Uchukuzi
Next Article Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Mbarawa Aitaka Jamii Kulinda Miundombinu ya Uchukuzi
Habari February 1, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?