MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Sekta Binafsi Kuimarisha Huduma Za Fedha Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Sekta Binafsi Kuimarisha Huduma Za Fedha Nchini
Habari

Serikali Sekta Binafsi Kuimarisha Huduma Za Fedha Nchini

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI  imekuwa ikihimiza taasisi za fedha kuipeperusha bendera ya Tanzania nje ya nchi kwa kufanya uwekezaji wa kimkakati.

Hayo yameelezwa leo Februari 25, 2025 Kahama mkoani Shinyanga na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,Dkt. Doto Biteko wakati akizindua tawi la Benki ya Exim katika eneo hilo.

“ Eneo hili ni kitovu kikubwa cha shughuli za kiuchumi, hasa sekta ya madini ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kwenye pato la Taifa.

Mbali  ya madini, mji huu pia ni maarufu katika sekta ya kilimo na biashara. Ni wazi kuwa ufanisi wa sekta hizi unategemea upatikanaji wa huduma za kifedha imara na zinazokidhi mahitaji ya wajasiriamali na wafanyabiashara,” amesema Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko ametaja manufaa ya kufungua tawi eneo hilo kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa fursa za uchumi kwa kuongeza ajira, kuongeza mapato ya benki na hivyo kutumia sehemu ya faida yake kuchangia maendeleo ya jamii ikiwemo kusaidia makundi maalum kadhaa yenye uhitaj.

Aidha,amesema manufaa mengine ni kuongezeka kwa mapato ya kodi Serikalini na kuongezeka kwa ushindani wa huduma za kibenki.

Pia, Dkt. Biteko ameipongeza benki hiyo kwa hatua kubwa na kwa jitihada zake za kuiwakilisha Tanzania  katika nchi za Comoros, Uganda, Djibouti, pamoja na Ethiopia.

Amesema  Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuimarisha huduma za kifedha na kuhakikisha kuwa zinapatikana kwa urahisi na kwa ufanisi kwa kila Mtanzania.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,  Anamringi Macha amesema kuwa ufunguzi wa tawi la benki hiyo ni kielelezo kuwa shughuli za uchumi ni nyingi na zitaendelea kuimarishwa.

Ameongeza kuwa Mkoa huo una matawi ya benki 11 ambayo yote pia yapo Kahama hivyo  ni kiashiria kuwa Kahama ipo kibiashara na kuwa Mkoa huo uko tayari kushirikiana na benki hiyo.

Naye, Kamishna wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Dkt. Charles Mwamwaja amesema kuwa Serikali imeendelea kuweka mazingira mazuri ya kifedha na kuwa dira iliyopo imekuwa ikiwaongoza na ni mpango mkuu wa sekta ya fedha ulioandaliwa na Serikali umeweka mazingira wezeshi na moja ya manufaa yake ni kufunguliwa kwa tawi hilo la benki.

Pamoja na hayo, amesema kuwa kumekuwepo na changamoto ya watoa huduma wasio waaminifu na mikopo chechefu, hivyo Wizara kupitia Benki Kuu imeendelea  kukabiliana na changamoto hizo kwa kutoa elimu ya masuala ya fedha mijini na vijijini ili wananchi waelewe na kutumia fursa za fedha zilizopo.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu amesema benki hiyo si tu imesaidia katika sekta ya afya bali hata elimu, ubunifu na kuwezesha wajasiriamali wanawake.

 

 

You Might Also Like

Stamico Yapewa Tuzo Na FDH Kujali Wenye Ulemavu

Serikali Yatumia Zaidi Ya Bilioni 100 Kupeleka Umeme Simiyu

TAFIRI Wakabiliana Na Mabadiliko Ya Tabianchi

Kongamano la Kahawa Bora Afrika kufanyika Tanzania Februari mwakani

OUT Yawapiga Msasa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mafanikio Ya TEA Kwa Serikali Awamu Ya Sita;Miradi Ya Elimu 3,768 Yatekelezwa, Bil. 49.5 Zatumika
Next Article Watafiti Wa Mimea Vamizi Watua Serengeti
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?