MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Kuanzisha Kituo Maalum Cha Kuwezesha Wawekezaji Vijana
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Kuanzisha Kituo Maalum Cha Kuwezesha Wawekezaji Vijana
Habari

Serikali Kuanzisha Kituo Maalum Cha Kuwezesha Wawekezaji Vijana

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu

KATIKA kuchochea uwekezaji unaoleta tija zaidi na kutoa fursa kwa vijana serikali ina mpango wa kuanzisha kituo maalum cha kuhudumia na kuwezesha  wawekezaji vijana.

Aidha itaanzisha program maalum ya kuwezesha wawekezaji vijana kubuni na kuanzisha uwekezaji wa viwanda nchini kote.

Waziri kutoka Ofisi Ya Rais, Mipango Na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema hay oleo Dar es Salaam wakati akieleza vipaumbele na fursa kwa vijana katika miaka mitano ijayo na kuongeza kuwa programhiyo itazinduliwa kabla ya mwisho wa mwaka.

Amesema katika kuwezesha mipango hiyo kwa kuanzia watatenga maeneo ambayo vijana waliomaliza vyuo vikuu na vyuo vyuo vya ufundi kupewa  ili kuweza kuwekeza kwenye viwanda.

Profesa Kitila amesema program hiyo itahusisha mafunzo, uwezeshaji wa kupewa ardhi, kuunganishwa na wauzaji wa mitambo na  malighafi na pia kuunganisha na benki ambazo zina ushirikiano na TISEZA.

“Tutatenga maeneo yafuatayo maalum kwa uwekezaji utakaofanywa na vijana,” amesema na kuyataja maeneo  hayo na  ardhi itakayotumika kuwa ni pamoja na Dodoma eneo la Nala lenye ekari 100.

Ameyataja maeneo mengine kuwa ni Pwani eneo la Kwala ekari 20, Mara (Bunda) ekari 100, Ruvuma (Songea) ekari 100 na Bagamoyo ekari 20 .

Mbali na kuanzisha program hiyo, Profesa  Kitila amesema serikali ina mpango wa kusogeza huduma za Mamlaka ya uwekezaji na maeneo maalum ya kiuchumi kufikia kila mkoa ifikapo mwaka 2028.

Amesema kila mkoa utakuwa na kituo maalum cha kutangaza na kuwezesha wawekezaji Pamoja na agizo la Rais Dkr Samia Suluhu Hassan la  kusogeza huduma kwa wananchi wote.

“Tutashirikiana na TAMISEMI kuratibu na kuwezesha huduma hizi kuwafikia  wote nchini,” amesema Profesa Kitila an kuongeza pia kwa kushirikiana na sekta binafsi kujenga miundombinu ya uwekezaji wa viwanda nchi nzima.

Amesema kwenye eneo hilo TISEZA ataingia ubi ana wenye mitaji ili kujenga majengo ya  viwanda ambayo yatakodishwa kwa gharama nafuu kwa mtanzania yoyote anayetaka kuwekeza kwenye viwanda.

Amesema mpango utapunguza gharama za watanzania kuwekeza na kunufaika na mageuzi ya kiuchumi yanayotokea nchini kote, hatua hiyo itaongeza fursa za kiuchumi na kukuza  kipato cha mtanzania mmojammoja.

Profesa Kitila amesema  pia serikali itabuni na kuanzisha vituo vipyavya kiuwekezaji mara kwa mara ili kuongeza uimara wa uwekezaji nchinina mvuto wa Tanzania kwa wote wenye mitaji huko duniani.

“ Katika kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, serikali inakamilisha maadalizi ya mkakati mpya wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini utakaozinduliwa kabla ya kuanza utekelezaji wa dira 2050 Julai mosi 2026.

Amesema ni matarajio ya serikali ifikapo mwaka 2030 hatua kubwa zitakuwa zimepigwa na mfanikio makubwa kupatikana ikiwemo kuongezeka miradi ya uwekezaji, fursa za ajira kupanuka na mitaji ya uwekezaji kukua.

Amesema matarajio ni kuzalisha ajira milioni nane na kuvutia mtaji wenye jumla yad ola za Kimarekani angalau bilioni 50 ifikapo 2030.

You Might Also Like

MOI Yazindua Mfumo Mpya Wa Kielektroniki Wa Kupanga Miadi Na Madaktari

MWALIM: Njaa na Ukosefu wa Ajira Ni Matokeo ya Uongozi wa CCM

Heshima ya Udaktari Ni Mwito wa Kulitumikia Taifa: Dkt Ikomba

Watafiti, Wabunifu Waendelezwe Wasivunjwe Moyo- Biteko

TARURA Yatenga Milioni 580 Kuboresha Barabara Zinazohudumia Sekta ya Madini Geita

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Next Article TPDC na PURA Hakikisheni Watanzania Wananufaika na Rasilimali za Mafuta na Gesi- Salome
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPDC na PURA Hakikisheni Watanzania Wananufaika na Rasilimali za Mafuta na Gesi- Salome
Habari December 8, 2025
Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Habari December 5, 2025
DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Habari December 5, 2025
Msama Aipongeza Hotuba Ya Samia, Atoa Neno Kwa Vijana, Wazee, Wanaharakati
Habari December 4, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?