MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rais Wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Mgeni Rasmi Mkutano Wa THRAPA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rais Wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Mgeni Rasmi Mkutano Wa THRAPA
Habari

Rais Wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Mgeni Rasmi Mkutano Wa THRAPA

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHAMA cha  Wataalam wa Rasilimali Watu na Utawala Tanzania (THRAPA), kimeandaa Mkutano wa wataalaam kutoka sekta mbalimbali nchini, kujadili na kubadilishana uzoefu wa kitaaluma mahala pa kazi kulingana na mabadiliko ya teknolojia duniani.

Mwenyekiti wa THRAPA, Christopher Mwansasu amesema hayo Mkoani Dar es Salaam leo, Mei 13, 2025 alipozungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mkutano huo utakaofanyia katika Hoteli ya New Amaan Visiwani Zanzibar, kuanzia Mei 20 hadi 22 mwaka huu 2023.

Mwansasu amesema mkutano huo utaambatana na maadhimisho ya siku ya Rasilimali Watu Duniani na Mkutano Mkuu wa Mwaka.

Ametaja kauli mbiu ya siku hiyo ni, ‘Uwezo wa Nguvukazi ya Baadaye, Inayoendeshwa na Akili Bandia’.

Amesema Mgeni Rasmi atakuwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ally Mwinyi.

“Njoo tujifunze teknolojia mpya za kitaaluma na viwango vya ubora mahala pa kazi. Tukuze taaluma na kujenga mtandao wa kitaaluma,” amesema.

Naye Katibu Mkuu wa chama hicho, Denis Derua amesema kuwa changamoto za taaluma zinasababishwa na mazingira kulingaa na nyakati.

“Hata changamoto za ajira namna ya kusimamia watu. Kwa kuwa tunapambana kuona namna gani tunashauri watu, tunashauri mwajiri, tunaishauri serikali na tumekuwa sehemu ya kushirikiana na serikali,” amesema.

Kwa upande wake mjumbe wa chama hicho, Bruno Daniel amesema kitaalam kuna mazingira ya kazi yanahitaji uzoefu wa utendaji.

Amewataka waajiri kuchukua wanafunzi na kuwajengea uzoefu.

“Rai yetu ni kuwahamasisha wanachama kukumbusha waajiri wawe na mipango thabiti kufundisha ili wawe na uwezo wa kuajirika,” amesema.

Pia amesema wana taasisi ya kutoa mafunzo na mitihani ya ithibati, pia watakuwa na mafunzo kuhakikisha wataalamu wao wanapikwa vizuri.

You Might Also Like

Kongamano  La Kimataifa La Jotoardhi Laanza Kwa Mafanikio

Ridhiwani, Waziri Wa Kazi, Ajira UAE Waweka mkakati

Wanaodaiwa Kumuua Ofisa TRA Washikiliwa na Polisi

TARI Yawapa Elimu Wakulima, Maofisa Ugani 165 Kilimo Cha Matunda

TUCTA Yakutana Na Mkuu Wa Mkoa Mbeya, Maandalizi Mei Mosi kitaifa 2025.

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kenya, Tanzania Zashirikiana na China Kukabiliana na Changamoto za Ushuru wa Marekani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Kenya, Tanzania Zashirikiana na China Kukabiliana na Changamoto za Ushuru wa Marekani
Makala May 13, 2025
SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele
Habari May 12, 2025
Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina
Habari May 12, 2025
Uchaguzi Mkuu 2025: Majimbo Mapya Nane Yaanzishwa, 12 Yabadilishwa Majina
Habari May 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?