MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini
Habari

PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Nishati,  Deogratius John Ndejembi ameutaka Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuhakikisha kuwa maghala yote makubwa ya usambazaji wa mafuta yanapata bidhaa hiyo kwa wakati, ili kuimarisha upatikanaji wake nchini.
Hayo yamesemwa  leo Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa kikao chake na viongozi wa PBPA, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na kampuni ya TIPER kwa lengo la kujadili hali ya upokeaji wa mafuta yanayoingia nchini.
Habari Picha 11594
Akizungumza katika kikao hicho,  Ndejembi ameielekeza PBPA kuweka mfumo madhubuti wa upangaji wa ratiba ya ushushaji wa mafuta (sequencing) ili kuhakikisha maghala yote makubwa yanayohusika na usambazaji yanapata mafuta kwa usawa na kwa wakati.
 Amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto za upatikanaji wa mafuta katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Habari Picha 11595
Aidha, ameeleza kuwa Serikali imekubaliana kuharakisha ushushaji wa meli za mafuta zinazoingia nchini, hususan kwa ajili ya matumizi ya ndani, ili kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unaendelea kuwa wa uhakika na salama.
Ameongeza kuwa Serikali imefanya mazungumzo na Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER), na kuelekeza kuwepo kwa utaratibu mzuri wa kupanga ushushaji wa mafuta ili wasambazaji wote wapate huduma kwa usawa.
Waziri Ndejembi amewaasa Watanzania kutokuwa na taharuki kuhusu upatikanaji wa mafuta, akisisitiza kuwa nchi ina akiba ya kutosha.
Vilevile,  Ndejembi,  ameitaka EWURA kuhakikisha kuwa mafuta yote yanayotoka kwenye maghala yanafika kwa walengwa na kutumika ipasavyo, huku vituo vya mafuta vikihimizwa kuuza bidhaa kulingana na mahitaji halisi ya soko.
Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia, Dkt. James Mataragio,  Mtendaji Mkuu wa PBPA,  Erasto Simon, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa TIPER,  Mohamed Mohamed na wataalam mbalimbali wa sekta ya mafuta.

You Might Also Like

Ridhiwani akutana na Mtendaji Mkuu ATE

TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar

Huduma ya Mahakama ya Mwanzo yasogezwa Wilaya ya Ubungo

Ridhiwani, Mlao na wanachama wa CCM Kata ya Bwilingu wakinadi chama chao dakika za lala salama

Tanzania yashiriki Kongamano la Afya Duniani jijini Berlin

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article UNFPA,Wadau Washauri Kuimarisha Usalama Wa Kidigitali Kukabiliana na Ukatili Wa Jinsia Mtandaoni
Next Article Randama Ya Maji 2026/27 Yaidhinishwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii
Habari March 28, 2026
Italia Yahimiza Ubunifu Wa Bidhaa Za  Sanaa Za Vioo
Habari March 28, 2026
Randama Ya Maji 2026/27 Yaidhinishwa
Habari March 27, 2026
UNFPA,Wadau Washauri Kuimarisha Usalama Wa Kidigitali Kukabiliana na Ukatili Wa Jinsia Mtandaoni
Habari March 26, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?