MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Habari

Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 

Author
By Author
Share
3 Min Read
– TARI Yatangaza Mbegu 22 Mpya Za Kisasa
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: NYANYA aina ya cheri zile ndogo ndogo tamu zenye rangi nyekundu na virutubisho vingi, ambazo zilipotea kwenye soko kwa muda mrefu, sasa zimerejea baada ya kufanyiwa utafiti na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI).
Mtafiti Mwandamizi kutoka Kituo cha TARI Tengeru, Emmanuel Laswai amesema Kituo hicho kinachojihusisha na utafiti wa mazao ya mbogamboga, matunda, viungo na vikolezo, kimefika na mbegu mpya aina 22, katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba mkoani Dar es Salaam.
Amesema mbegu hizo zinalenga kuboresha uzalishaji wa mazao na kukidhi mahitaji ya wakulima pamoja na masoko ya ndani na nje ya nchi.
Laswai amesema mbegu hizo mpya ni matokeo ya kazi ya miaka kadhaa ya utafiti, zikilenga kustahimili changamoto za mabadiliko ya tabianchi, magonjwa, na kuongeza tija.
“Katika nyanya, tumezalisha aina sita mpya, mojawapo ikiwa nyanya ya cheri ile ndogo iliyokuwa imepotea kwa muda mrefu.
“Tumeboresha mbegu hiyo, sasa ina mavuno mengi, haishambuliwi sana na magonjwa, na inawavutia watumiaji hususan kwenye hoteli na migahawa ya kisasa jijini Arusha na Dar es Salaam,” amesema.
Amesema pia wana aina mpya za pilipili hoho za rangi nyekundu na ya njano ambazo sasa zinaweza kulimwa nje ya kitalu nyumba, tofauti na ilivyozoeleka.
“Aina mpya za pilipili aina ya abanero  maarufu kwa ladha na harufu yake  zimeboreshwa kwa uwezo mkubwa wa kuhimili magonjwa ya virusi na bakteria, na kuleta chaguo la rangi mbalimbali kama njano, machungwa na nyekundu,,” amesema.
Amesema pia wametafiti ngogwe chungu iambayo ni mboga maarufu ya asili ilikuwa imeadimika sokoni.
Laswai anasema wamezalisha aina tatu mpya za ngogwe, mojawapo ikiwa ile ya muundo wa mshumaa, maarufu sokoni, lakini sasa ikiwa na ladha ya uchungu zaidi kama ilivyokuwa asili yake.
“Hii ngogwe chungu ni mahsusi kwa wale waliokuwa wanaikumbuka na kuhitaji ladha ya asili. Tuliboresha lakini hatukuondoa uchungu wake ambao ndio sifa kuu ya nyanyachungu,” amesema.
TARI Tengeru inawaalika wakulima na wadau wote wa kilimo cha mbogamboga kujipatia mbegu hizo mpya kwa lengo la kuongeza tija, ubora wa bidhaa, na kuongeza kipato kupitia kilimo cha kisasa chenye tija.

You Might Also Like

FAJ Yataka Wahamiaji Wa Kazi Wa Afrka, Wanaokwenda Maeneo Mengine Walindwe

Vijana Wahimizwa Kushiriki Kikamilifu Soko Huru la Afrika

Mramba Afungua Mafunzo Ya Teknolojia Ya Nishati Jua Kwa Watalaam

NIT Yajivunia Uanzishwaji Chuo Cha Marubani

Dar Yaidhinishiwa Bil. 68 Ukarabati, Matengenezo Ya Barabara

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article NFRA Yawaalika Wadau Kununua Nafaka kwa Masoko ya Ndani na Nje
Next Article Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?