MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mikataba ya Bilioni 50.9 Yasainiwa kuwezesha nishati safi ya kupikia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mikataba ya Bilioni 50.9 Yasainiwa kuwezesha nishati safi ya kupikia
Habari

Mikataba ya Bilioni 50.9 Yasainiwa kuwezesha nishati safi ya kupikia

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema Serikali inafanya kila jitihada kuhakikisha kunakuwa na unafuu katika upatikanaji wa bidhaa za nishati safi ya kupikia ili kumwezesha kila mwananchi kutumia nishati iliyo safi na salama.
Biteko amesema hayo Septemba 13, 2024 Jijini Dodoma wakati wa hafla ya kusaini mikataba ya ushirikiano ya utekelezaji wa nishati safi ya Kupikia yenye thamani ya Sh. Bilioni 50.98 kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Jeshi la Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Wasambazaji wa Gesi ya kupikia.
Hafla hiyo imeenda  sambamba na uzinduzi wa jengo la REA.
“Namshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maono yake yanayowezesha sekta ya nishati kuendeshwa kwa mafanikio kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuokoa maisha ya watanzania.
“Pia kuiwezesha Wizara ya Nishati kutatua changamoto zinazojitokeza lengo likiwa ni kutoa huduma iliyo bora kwa wananchi,” amesema.
Kuhusu usambazaji nishati vijijini ikiwemo umeme, Biteko ameipongeza Bodi na Menejimenti ya REA kwa kusimamia ipasavyo miradi kwa kuwahimiza wakandarasi kukamilisha kazi kwa wakati.
Kwa upande wa jengo lililozinduliwa la ghorofa tano lenye thamani ya Sh. Bilioni 9.8, Biteko amesema litawawezesha watumishi kutoa huduma kwa wananchi.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo amesema tukio hilo ni alama ya ushirikiano kati ya REA na Taasisi za Jeshi.
Ameishukuru serikali kwa jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, udhibiti wa rasilimali za misitu na kutengeneza fursa za ajira kupitia Nishati Safi ya Kupikia.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameishukuru serikali kwa kutoa Sh. Bilioni 214 kwa ajili ya shughuli za umeme mijini na vijijini ambapo mkoani Dodoma asilimia 92.2 ya vijiji vimefikiwa na umeme huku kazi hiyo usambazaji umeme ikiendelea.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba amesema kusainiwa kwa mikataba hiyo ni utekelezaji wa agizo la Rais Samia  alilolitoa wakati akizindua mjadala wa kitaifa wa Nishati Safi ya kupikia.
Na kutilia mkazo wakati akizindua Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia hivyo Wizara ya Nishati ina wajibu wa kutekeleza agizo hilo, ndio maana taasisi yake ya REA imesaini mikataba
Awali Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA),  Hassan Saidy amesema Wakala kuhamia kwenye jengo lake kumewezesha kuokoa Sh. Milioni 650 zilizokuwa zikitumika kwa mwaka kulipia kodi ya pango ambazo sasa zinaelekezwa kwenye maendeleo ya huduma zinazotolewa na Wakala.
Saidy amesema kwa upande wa JKT mikataba iliyosainiwa ina thamani ya Shilingii Bilioni 5.75 ambapo kati ya fedha hizo asilimia 76 ambayo ni sawa na Sh. Bilioni 4.37 itatolewa na REA na huku asilimia 24 sawa na Sh. Bilioni 1.39 itatolewa na JKT.

You Might Also Like

Kampuni ya Kichina CCCC yatoa msaada wa vitabu UDSM

Bajeti ya TUGHE 2025 Yaidhinishwa

TPHPA yafundisha namna sahihi ya utumiaji wa viuatilifu

Ridhiwani Awataka Wananchi Kuboresha Taarifa Zao Tayari Kwa Uchaguzi Mkuu

Askari Wawili wa JWTZ Wafariki, Wanne Wajeruhiwa DRC

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TRA Kuzindua Boti Za Kisasa Kudhibiti Bidhaa Hatarishi
Next Article WCF yapongezwa kwa Ithibati ya ISO, utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?