MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mbunge Ndoinyo Asema Imani ya Wananchi kwa Rais Samia Yazidi Kuimarika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mbunge Ndoinyo Asema Imani ya Wananchi kwa Rais Samia Yazidi Kuimarika
Habari

Mbunge Ndoinyo Asema Imani ya Wananchi kwa Rais Samia Yazidi Kuimarika

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Ngorongoro, Yannick Ndoinyo, amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameingilia kati changamoto zilizokuwepo katika wilaya hiyo, hali iliyosababisha mambo kuanza kutulia na kuleta matumaini mapya kwa wananchi.
Amesema wananchi wa Ngorongoro wana imani kubwa na Rais Samia na wanaamini uongozi wake utaendelea kuleta mabadiliko chanya na maendeleo makubwa zaidi.
Ndoinyo ameyasema hayo wakati akichangia hotuba ya Rais Samia katika uzinduzi wa Bunge la 13, kuelekea siku 100 za utekelezaji wa Awamu ya Sita, Kipindi cha Pili.
Habari Picha 10997
Ameeleza kuwa Wilaya ya Ngorongoro ni eneo la uhifadhi, utalii na ufugaji, ambapo shughuli hizo ndizo vyanzo vikuu vya mapato kwa wananchi.
Hata hivyo, kwa muda mrefu kumekuwepo na sintofahamu pamoja na minong’ono kati ya mamlaka za uhifadhi na wananchi kuhusu matumizi ya maeneo ya hifadhi.
Amesema wilaya hiyo ni kitovu cha uzalishaji kupitia ufugaji na utalii, na kwamba lengo la Rais Samia ni kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia milioni nane ndani ya kipindi cha miaka mitano.
Amesema ili kufanikisha azma hiyo, alisisitiza umuhimu wa kuboresha miundombinu, hususan barabara, kwani nyingi bado hazina lami.
Kwa mujibu wake, uboreshaji wa barabara utawezesha watalii kufika kirahisi katika vivutio vyote vilivyopo ndani ya wilaya hiyo, jambo litakaloongeza idadi ya watalii zaidi ya lengo lililowekwa.
Kwa sasa, watalii wengi hushindwa kufika katika maeneo nyeti kutokana na changamoto ya miundombinu mibovu, hususan maeneo ya Loliondo na Serengeti.
Ndoinyo aliongeza kuwa Rais Samia aliwahi kuahidi kutengeneza barabara hizo, na tayari dalili za utekelezaji wa ahadi hiyo zinaonekana kwa kuanza kwa kazi za ujenzi.
Kuhusu sekta ya ufugaji, amesema kuwa jamii ya wafugaji inataka kuona sekta hiyo ikiboreshwa ili iweze kuongeza tija na kuchangia zaidi katika pato la Taifa.
Aidha, alitoa pongezi kwa Rais Samia kwa kuchagua viongozi wasikivu, akieleza kuwa ana orodha ya Mawaziri sita ambao wameonesha nia ya kufika jimboni Ngorongoro kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Alitoa wito kwa Wakuu wa Mikoa, Wilaya pamoja na watendaji wa kata kuhakikisha wanachangamka na kufanya kazi kwa kasi ili kuendana na ari ya utendaji ya Rais Samia, kwa lengo la kufanikisha malengo ya maendeleo yaliyojiwekea taifa.

You Might Also Like

Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti

Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar

CPC chatambua juhudi za Rais Samia

Dar es Salaam Kuunda Kamati Ya Kupitia Majengo Chakavu

Wagombea Wa CCM Dodoma Mjini Waanza Kujinadi kwa Wajumbe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mtasingwa Aitaka Serikali Kuwatengea Eneo Wafanyabiashara wa Senene Bukoba
Next Article Hotuba ya Rais Samia Yachochea Miradi Mikubwa ya Viwanda na Bandari Bagamoyo – Mgalu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari February 2, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?