MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Maziwa Kukuza Uchumi Wa Wafugaji
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Maziwa Kukuza Uchumi Wa Wafugaji
Habari

Maziwa Kukuza Uchumi Wa Wafugaji

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
IRINGA: WAFUGAJI wa ng’ombe wa maziwa katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga, mkoani Iringa, wanatarajia  kukuza uchumi wao kupitia uzalishaji wa maziwa yaliyo bora na salama, baada ya kupatiwa elimu ya kitaalamu kuhusu usafi, uhifadhi na usindikaji wake.
 Elimu hiyo imetolewa mkoani Iringa,  na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA),  kuhusu afya ya mifugo, hususani ugonjwa wa homa ya kiwele, pamoja na athari za usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa.
Katika mafunzo hayo, wafugaji wameelekezwa namna sahihi ya kuzalisha maziwa salama na yenye kukidhi viwango vya ubora, jambo ambalo litaongeza kipato, kupanua masoko, ikiwa ni pamoja na kubadili maisha ya familia nyingi.
Akizungumza kwa niaba ya wafugaji wenzake baada ya mafunzo, Uneiy Chaula kutoka Mafinga amesema elimu waliyoipata imewaongezea maarifa ya kufuga kwa tija na kibiashara.
“Sasa tunaweza kutambua ugonjwa wa kiwele mapema, kutumia vifaa sahihi kama California Mastitis Test (CMT), na kutengeneza bidhaa kama mtindi.
Hii ni fursa ya kuongeza kipato chetu na kuvutia wateja zaidi,” amesema Oscar Ngimba, mfugaji kutoka Mafinga.
 Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ambaye pia ni Mtafiti wa Mradi wa NANO COM, Dkt. Nuria Majaliwa, amesema maziwa ni rasilimali ya thamani yenye mchango mkubwa katika lishe na uchumi wa mfugaji.
Amesema mchango huu unaweza kuonekana kikamilifu endapo tu maziwa hayo yatazalishwa, na kuhifadhiwa kwa kuzingatia kanuni bora za uzalishaji na usalama wa chakula.
Amesema kwa kufanya hivyo maziwa yatakuwa salama kwa mlaji, kukidhi viwango vya ubora vinavyotambulika kitaifa na kimataifa, hivyo kufungua fursa zaidi za kibiashara kwa wafugaji na wajasiriamali wa bidhaa za maziwa.
“Maziwa yanaweza kuwa chanzo cha lishe bora au chanzo cha maradhi endapo hayatazalishwa, kuhifadhiwa na kusindikwa kwa viwango vinavyokubalika. Elimu hii inalenga kuongeza thamani ya maziwa na kukuza kipato,” amesema.
Nqye Daktari wa wanyama wa  Halmashauri ya Halmashauri ya wilaya ya Mufind,
Innocent  Nguluma amesema elimu hiyo imekuwa msaada mkubwa kwa wafugaji kutambua mbinu bora za usindikaji, usafi wa mazingira na namna bora ya kuzuia magonjwa ya mifugo ambayo huathiri moja kwa moja uzalishaji wa maziwa.
“Kujua namna ya kudhibiti ugonjwa wa kiwele na kutunza maziwa kwa usafi kunafanya uzalishaji wa bidhaa bora sokoni, kipato zaidi kwa mfugaji, na afya bora kwa mlaji,” amesema
Mradi wa  NANO COM unaoendeshwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ambao unafadhiliwa na Kituo cha Kimataifa cha Maendeleo ya Utafiti cha Canada (IDRC), unalenga kuimarisha usalama wa chakula, lishe na kipato cha wafugaji kupitia mnyororo wa thamani wa maziwa

You Might Also Like

Ridhiwani, Waziri Wa Kazi, Ajira UAE Waweka mkakati

Matumizi Mabaya Ya Dawa Husababisha Usugu Wa Vimelea Kwa Wanyama – Dkt. Kitimu

Wanawake Taasisi za Kitafiti Watoa Furaha Kwa Waliojifungua, Madaktari, Manesi Kawe Kituo Cha Afya

Mgahawa unaotembea fursa kwa vijana, kutoa huduma ya unywaji wa kahawa

Vyuo vya Kilimo vishirikishwe mradi wa BBT

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti
Next Article Madaktari Toka China Waleta Matumaini Barani Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Madaktari Toka China Waleta Matumaini Barani Afrika
Makala May 16, 2025
Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti
Habari May 15, 2025
Serikali Kupeleka Umeme Maeneo Ya Kimkakati
Habari May 15, 2025
Jaffo Aagiza Kufufuliwa Vilivyokuwa Viwanda Vya Serikali
Habari May 15, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?