MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu
Habari

Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) imeendelea kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali wa elimu katika juhudi za kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia, kwa lengo la kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata elimu bora katika mazingira salama na rafiki.
Kupitia ushirikiano na Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF) na kwa ufadhili wa Serikali ya Canada, TEA inatekeleza jumla ya miradi 48 ya ujenzi, ukarabati na umaliziaji wa miundombinu ya elimu katika mikoa ya Tabora, Kigoma na Songwe.
Habari Picha 9881
Atugonza David Ofisa Miradi kutoka TEA akiwa na Mwalimu Maisha Masabile Makamu Mkuu wa shule ya Nyakitonto alipokuwa akikagua hali ya ukarabati wa maabara tatu za Sayansi shuleni hapo.
Ofisa Miradi kutoka TEA, Atugonza David, ameeleza hayo wakati wa ziara ya kukagua miradi hiyo na kuweka vibao vya ufadhili.
Amesema miradi mingi imekamilika na ipo tayari kutumika, huku akisisitiza kuwa maeneo mengi yamelenga ukarabati na uboreshaji wa maabara za sayansi kama sehemu ya kuunga mkono mkakati wa Serikali wa kuongeza ushawishi kwa wanafunzi katika masomo ya sayansi.
Habari Picha 9875

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyakitonto iliyopo Wilayani Kasulu wakifanya mazoezi ya somo la Fizikia kwa vitendo kwenye maabara iliyokarabatiwa na UNICEF, kwa ufadhili wa Serikali ya Canada na kusimamiwa na TEA

Miongoni mwa shule zilizofaidika ni Shule ya Sekondari Nyakitonto, iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma. Shule hiyo ilipokea takriban Sh. Milioni 60 kwa ajili ya ukarabati wa maabara tatu za sayansi.
Makamu Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Maisha Masabile, amesema mradi huo umeleta mageuzi chanya katika ufaulu.
Habari Picha 9873

Mwalimu Maisha Masabile Makamu Mkuu wa shule ya Nyakitonto akifafanua jambo kwa Ofisa Miradi kutoka TEA, Atugonza David alipokuwa akikagua hali ya ukarabati wa maabara tatu za Sayansi shuleni hapo.

“Awali tulikosa maabara kabisa na tulikuwa tukifanya mazoezi ya vitendo darasani. Sasa tuna vyumba vitatu vya maabara vilivyokarabatiwa. Mwaka 2024 ufaulu ulikuwa asilimia 100, huku wanafunzi 43 kati ya 150 wakichagua masomo ya sayansi. Mwaka huu 2025, idadi imeongezeka hadi wanafunzi 68 kati ya 210,” amesema Mwalimu Masabile.
Habari Picha 9876
Kwa sasa, TEA kwa kushirikiana na UNICEF, inaendelea kutekeleza miradi yenye thamani ya takriban shilingi bilioni 2.5 katika mikoa hiyo mitatu, kwa lengo la kuinua ubora wa elimu, kuongeza fursa za ujifunzaji na kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bora na jumuishi.
Habari Picha 9877

Monekano wa kibao cha ufadhili wa maabara tatu za sayansi Shule ya Sekondari Nyakitonto iliyopo Wilayani Kasulu.

Habari Picha 9878

Monekano wa jengo la maabara tatu za sayansi zilizofanyiwa ukarabati na UNICEF, kwa ufadhili wa Serikali ya Canada na kusimamiwa na TEA Shule ya Sekondari Nyakitonto iliyopo Wilayani Kasulu.

You Might Also Like

Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika

Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba

TUICO Arusha Yapongezwa Na AUWSA

Dhibitini Magonjwa ya Mlipuko-Mchengerwa

Ulega : Nimeridhisha Na Hatua Iliyofikiwa, Ongezeni Kasi Zaidi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa Afurahishwa Na Ustadi Wa Vijana Wenye Ulemavu Veta
Next Article VETA Yawasilisha Teknolojia ya Hybrid Katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?