MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa Ataka Wafanyakazi Waandaliwe Kwa Mabadiliko Ya Teknolojia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa Ataka Wafanyakazi Waandaliwe Kwa Mabadiliko Ya Teknolojia
Habari

Majaliwa Ataka Wafanyakazi Waandaliwe Kwa Mabadiliko Ya Teknolojia

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa vyama vya wafanyakazi barani Afrika kuweka mikakati madhubuti ya kukabiliana na mabadiliko ya teknolojia duniani ili kulinda ajira na kuimarisha ustawi wa wafanyakazi.
Majaliwa ametoa wito huo alipohutubia Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Afrika (OATUU) uliofanyika mkoani Dar es Salaam, alipomwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan.
Amesisitiza umuhimu wa mafunzo endelevu kwa wafanyakazi ili kukabiliana na changamoto zinazotokana na matumizi ya teknolojia mpya ikiwemo akili mnemba.
Habari Picha 9125
“Tunapaswa kuweka mpango wa kutoa mafunzo endelevu yanayoendana na mabadiliko ya teknolojia ili kuwandaa wafanyakazi kwa aina mpya za ajira zinazojitokeza. Teknolojia lazima ilinde utu wa binadamu na si kudhoofisha heshima ya kazi,” amesema.
Amesema mapinduzi ya teknolojia na utandawazi yameleta mabadiliko makubwa katika mazingira ya kazi, na kwamba mitambo na mifumo ya kisasa imeanza kuchukua nafasi ya kazi ambazo hapo awali zilitegemea nguvu kazi ya binadamu.
Waziri Mkuu ameeleza kuwa Serikali  imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha wafanyakazi wanajengewa uwezo wa kukabiliana na mabadiliko hayo, ikiwa ni pamoja na kuhamasisha matumizi sahihi ya teknolojia mpya na kulinda haki pamoja na faragha za wafanyakazi.
Habari Picha 9126
Amesisitiza kuwa serikali inaendelea kutambua na kuthamini mchango wa vyama vya wafanyakazi katika maendeleo ya taifa, na kwamba uhusiano mzuri uliopo baina ya serikali na vyama hivyo umechangia maboresho ya sera, sheria na mazingira ya kazi nchini.
“Serikali imevipa nafasi vyama vya wafanyakazi kufanya kazi kwa uhuru na bila kuingiliwa. Tunawasihi kuendelea kushirikiana nasi kwa lengo la kuboresha zaidi maslahi ya wafanyakazi,” amesema.
Naye Naibu Waziri wa Kazi, Vijana, na Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi, amesema serikali imeendelea kuimarisha ushirikiano na vyama vya wafanyakazi kwa kuhakikisha sera na sheria mbalimbali zinarekebishwa ili kulinda haki zao.
Habari Picha 9127
Makamu wa Rais wa OATUU, Joshua Ansah, ametoa wito kwa vyama vya wafanyakazi Afrika kuendelea kushikamana katika kutetea usawa na haki za wafanyakazi, huku akiishukuru Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo muhimu.
“Tuendelee kuunga mkono Shirikisho letu kwa maslahi mapana ya wafanyakazi barani Afrika. Tukiwa wamoja, tunaweza kusimamia na kupigania haki zao kwa mafanikio zaidi,” amesema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Kanda ya Afrika Mashariki, Caroline Mugalla, amebainisha kuwa ni muhimu kwa wafanyakazi kuhusishwa moja kwa moja katika kila mabadiliko ya kijamii na teknolojia yanayowahusu.
“Ni lazima wafanyakazi washirikishwe na waandaliwe kwa mabadiliko haya kwa kuwapatia mafunzo stahiki. Mafanikio ya maendeleo haya hayawezi kupatikana bila ustawi wa wafanyakazi,” amesema.
Habari Picha 9128
Naye Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhokya, ameeleza kuwa mafanikio yaliyopatikana katika kutetea haki za wafanyakazi nchini yametokana na mahusiano bora kati ya chama hicho na serikali.
“Tumetumia njia ya majadiliano na maridhiano kwa kiasi kikubwa. Serikali yetu imesikiliza changamoto za wafanyakazi na kutafuta suluhisho,” amesema Nyamhokya huku akifurahia Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa kihistoria.
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi wa Afrika (OATUU) lilianzishwa Aprili 1973 kwa juhudi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza wa Ghana, Kwame Nkrumah, kwa lengo la kuunganisha wafanyakazi wa Afrika na kutetea maslahi yao kwa pamoja.

You Might Also Like

Chalamila Atoa Wiki Mbili Wafanyabiashara Ndogo Ndogo Kufungua Njia Kariakoo

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni

ALAT Kujadili Ripoti Ya CAG

Kikwete: Waambieni Tunataka Maendeleo Sio Maneno

Rais Samia Kuzindua Mfuko wa Mikopo Wenye Kianzio Cha Sh. Bilioni 2.3

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa: Elimu Ya Watu Wazima, Silaha Ya Mapinduzi Ya Maendeleo
Next Article Wambali: Vyama Vya Wafanyakazi Muhimili wa Uchumi, Ustawi Wa Jamii
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?