MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025
Habari

Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amekikabidhi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) tuzo ya ushindi wa kwanza katika kundi la Elimu ya Juu, Maendeleo ya Ujuzi na Taasisi za Utafiti, kwenye Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba.

Majaliwa alikabidhu tuzo hiyo wakati akifunga maonesho hayo jana Julai 13, 2025, yaliyofanyika mkoani Dar es Salaam.

Tuzo hiyo, iliyotolewa katika hafla ya kufunga maonesho hayo imejumuisha UDSM kama taasisi bora iliyoonesha mchango mkubwa katika kuendeleza ujuzi, maarifa na bunifu kwa maendeleo ya taifa.

Waziri Mkuu Majaliwa, ambaye pia ni mhitimu wa chuo hicho, alilisifu banda la UDSM kwa kuonesha ubunifu unaogusa jamii moja kwa moja, huku akisisitiza umuhimu wa kuunga mkono bidhaa na huduma za ndani.

“Maonesho haya siyo tu jukwaa la biashara, bali ni daraja muhimu la kuunganisha ubunifu, uwekezaji na maendeleo ya viwanda. Tunapaswa kuyachukulia kwa uzito kama mataifa yaliyopiga hatua kama Japan,” amesema. Majaliwa.

Amesisitiza azma ya serikali kujenga uchumi wa ndani unaotegemea uzalishaji wa ndani na maarifa ya Watanzania wenyewe.

“Tunapaswa kuenzi bidhaa, chapa na bunifu zetu za ndani. Taasisi kama UDSM zina nafasi muhimu katika kutimiza azma hii.” amesema.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa William Anangisye, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayesimamia Utafiti, Profesa Nelson Boniface amesema ushindi huo ni ishara ya mafanikio ya pamoja na wito wa kuendelea kuwa mstari wa mbele katika suluhisho la changamoto za kitaifa.

“Tuzo hii ni ya kila mwanafunzi, mhadhiri, mtafiti na mshirika aliyeshiriki kutufikisha hapa. Ni ushahidi kwamba tukishirikiana tunaweza kubadili jamii kupitia utafiti na bunifu zenye suluhisho,” amesema.

Banda la UDSM liliwavutia maelfu ya wageni wa ndani na nje kwa ubunifu wa hali ya juu, maonyesho ya kisayansi na teknolojia za kisasa.

Miongoni mwa bunifu zilizosisimua wengi ni kifaa cha kidijitali kinachopima damu bila sindano, kilichobuniwa na mwanafunzi wa kike kutoka Kitivo cha  waliotembelea banda hilo ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kikwete amepongeza ubunifu na umuhimu wa miradi iliyowasilishwa.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya UDSM Sabasaba na Mkuu wa Mawasiliano wa UDSM, Dkt. Dotto Kuhenga, amesema ushindi huo umetokana na maandalizi makini, kazi ya pamoja na kujituma kwa dhati.

“Huu ni ushindi wa kimkakati. UDSM imejipambanua siyo tu kwa kufundisha, bali kwa kubadilisha maarifa kuwa suluhisho linalogusa jamii. Tumejipanga kuendelea kuwa chachu ya maendeleo ya taifa,” amesema.

Ushindi huo unaiimarisha nafasi ya UDSM kama moja ya taasisi zinazoongoza barani Afrika katika elimu ya juu, utafiti na ubunifu. Kwa dhamira ya kulea vipaji, kuendeleza maendeleo jumuishi na kutumia maarifa kubadilisha maisha.

You Might Also Like

Naibu Waziri Katambi aagiza CMA kutoa mafunzo kwa njia ya mtandao

Wapongeza Nyongeza Ya Likizo Kwa Aliyejifungua Mtoto Njiti

Utafiti Wa Roketi UDOM Uko Mbioni Kukamilika

TFS Yawataka Wananchi Kufuga Nyuki Kuzuia Uharibifu Wa Mazingira

Rais Samia na maadhimisho ya miaka 60 ya JWTZ

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Habari July 13, 2025
NFRA Yawaalika Wadau Kununua Nafaka kwa Masoko ya Ndani na Nje
Habari July 13, 2025
Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma
Habari July 13, 2025
Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Habari July 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?