MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mafunzo ya Ufundi Sasa Kupatikana Popote Kupitia Programu ya VSOMO”
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mafunzo ya Ufundi Sasa Kupatikana Popote Kupitia Programu ya VSOMO”
Habari

Mafunzo ya Ufundi Sasa Kupatikana Popote Kupitia Programu ya VSOMO”

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeendelea kutumia teknolojia ya kisasa kutoa mafunzo kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa VSOMO, unaowawezesha wanafunzi kujifunza kwa kutumia simu janja (smartphone) wakiwa mahali popote nchini.

Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Vijana yanayoendelea mkoani Mbeya, Ofisa Habari na Uhusiano wa VETA, David Mpondyo, alisema mfumo huo utasaidia kutoa fursa kwa watu wengi kupata mafunzo ya ufundi stadi bila kulazimika kuwepo darasani.

“Mwanafunzi anapakua programu ya VSOMO kupitia Play Store, kisha anaanza kujifunza kwa nadharia kupitia simu yake janja. Baada ya kukamilisha sehemu ya nadharia, hufanya mafunzo kwa vitendo (practical) katika chuo cha VETA kilicho karibu na anapomaliza hupewa cheti kinachotambulika sawa na wale waliopo darasani,” alisema Mpondyo.

Alibainisha kuwa mfumo huo umetumika kwa zaidi ya miaka tisa na umeendelea kuboreshwa ili kuendana na mahitaji ya soko la ajira, huku jitihada zikiendelea kuhakikisha hata sehemu ya vitendo inaweza kufanyika kwa kutumia simu janja.

Aidha, Mpondyo alisema VETA inatumia mfumo mwingine wa elimu kwa masafa uitwao Open and Distance e-Learning (ODeL), unaotumia TEHAMA kuwafikia wanafunzi walioko mbali na vyuo. Alisema mfumo huo unahusisha matumizi ya teknolojia mbalimbali za kisasa kama Uhalisia Pepe (Virtual Reality), Vifaa vya kuiga mazingira halisi ya kazi (Simulators), Mechatronics, Roboti (Robotics), Akili Bandia (Artificial Intelligence – AI) na Mtandao wa Vitu (Internet of Things – IoT).

Kwa mujibu wa Mpondyo, Serikali imetumia Shilingi milioni 273 kununua vifaa vya kufundishia vya kuiga mazingira halisi ya kazi (simulators) kwa ajili ya mafunzo ya uchomeleaji na uungaji vyuma, ili kuongeza ujuzi wa vitendo kwa wanafunzi.

Alisema kuwa mafanikio ya matumizi ya teknolojia hizo yameongeza ubunifu wa kisayansi na kiteknolojia miongoni mwa wakufunzi, wanafunzi na wahitimu wa vyuo vya VETA, ambao wamekuwa wakibuni suluhisho la changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi kupitia maarifa waliyojifunza.

“Lengo letu ni kuhakikisha vijana wanapata ujuzi unaokidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye ya soko la ajira. Tunaendelea kuboresha mazingira ya mafunzo ili kufikia vijana wengi zaidi na kuwapa maarifa ya kisasa,” alisisitiza Mpondyo.

You Might Also Like

Rais TUCTA Apongeza Mfuko Wa NSSF Kwa Ongezeko La Thamani Hadi Trilioni 9

Ripoti Ya Bodadoda Yazinduliwa

Dkt. Bwana: Tunafanya utafiti wa mbegu kutatua changamoto za wakulima

TUCTA Yakutana Na Mkuu Wa Mkoa Mbeya, Maandalizi Mei Mosi kitaifa 2025.

Mradi Wa Thamini Uzazi Salama Wakabidhiwa Vitendeakazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Profesa Ndunguru: Teknolojia ya Vinasaba Yafungua Ukurasa Mpya Katika Kilimo
Next Article Tanzania yashiriki Kongamano la Afya Duniani jijini Berlin
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?