MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Maadhimisho Ya VETA Ya Miaka 30 Kuhitimishwa Machi 18 Hadi 21, DSM
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Maadhimisho Ya VETA Ya Miaka 30 Kuhitimishwa Machi 18 Hadi 21, DSM
Habari

Maadhimisho Ya VETA Ya Miaka 30 Kuhitimishwa Machi 18 Hadi 21, DSM

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Mwandishi Wetu

SINGIDA: MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Elim una Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Anthony Kasore amesema kuwa mamlaka hiyo inaadhimisha miaka 30 tangu ilipoanzishwa mwaka 1995.

Kasore amesema hayo katika Chuo cha VETA, mkoani Singida kwa maelezo kuwa maadhimisho hayo yataangazia mafanikio, changamoto na mustakabali wa elimu ya elimu ya ufundi stadi nchini.

Amesema katika kipindi cha maadhimisho vyuo vya VETA vilivyopo kwenye mikoa na wilaya nchini kote vitatoa huduma ya ufundi ya ukarabati wa miundombinu ya Serikali bure ikiwemo majengo ya hospitali, zahanati, shule, ofisi za umma pamoja na kwa watu wasiojiweza, ili kuonyesha mchango wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwenye jami.

“Wanafunzi, walimu na wahitimu watatoa huduma za kiufundi kama kupaka rangi majengo yaliyochakaa, kurekebisha mifumo ya umeme, mifumo ya mabomba ya maji, milango na samani,”amesema.

Amesema maadhimisho hayo yataimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo ya elimu ya ufundi.

Amesema kilele cha maadhimisho hayo kitafanyika kwa siku nne, kuanzia Machi 18 hadi 21, 2025, katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, ambapo kutakuwa na maonesho ya kazi na ubunifu wa wanafunzi, mashindano ya ujuzi, kongamano la wadau, na utoaji wa tuzo kwa taasisi na watu binafsi waliochangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya sekta ya ufundi stadi nchini.

“Miaka 30 ya VETA ni ushuhuda wa dhamira ya Serikali ya kuhakikisha vijana wa Tanzania wanapata ujuzi bora wa ufundi stadi unaowawezesha kujiajiri na kuajiriwa. Katika miaka hii, tumeweza kuzalisha wahitimu wenye uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya Taifa,” amesema.

Amesema, kwa miaka 30, VETA imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwa kujenga vyuo vipya, kupanua fursa za mafunzo kwa makundi maalum, na kushirikiana na sekta binafsi ili kuhakikisha wahitimu wanapata ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Amesema idadi ya vyuo vinavyomilikiwa na VETA imeongezeka kutoka 14 mwaka 1995 hadi 80 mwaka 2025, huku vyuo vingine 65 vikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Pia sekta za mafunzo zimeongezeka kutoka 10 mwaka 1995 hadi 13 mwaka 2025, zikihusisha fani 89 zinazohitajika katika maendeleo ya viwanda na uchumi wa kisasa.

You Might Also Like

CMA yawataka wafanyakazi walioachishwa kazi kuwasilisha mgogoro ndani ya muda

UDOM yashauri matumizi ya green house kupata tija

Kikwete: Waambieni Tunataka Maendeleo Sio Maneno

Matukio Mbalimbali Katika Picha Baada Ya Waziri Mkuu Kuwasilisha Makadirio Ya Mapato Ya Bajeti

NIT Yajivunia Uanzishwaji Chuo Cha Marubani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Lugendo Awataka Wananchi Kujenga Tabia Ya Kufanya Usafi
Next Article Ridhiwani Kikwete Kuzindua Miradi ya Maendeleo Songwe
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?