MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kwelea Kwelea, Nzige, Viwavi Jeshi Kudhibitiwa Kwa Haraka
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > Kwelea Kwelea, Nzige, Viwavi Jeshi Kudhibitiwa Kwa Haraka
Makala

Kwelea Kwelea, Nzige, Viwavi Jeshi Kudhibitiwa Kwa Haraka

Author
By Author
Share
13 Min Read
– Ni Baada Ya TPHPA Kupokea Ndege Ya Kisasa 

– Profesa Ndunguru Amshukuru Rais Samia Kwa Kuleta Mageuzi Sekta Ya Kilimo

 

Na Lucy Ngowi

 

DODOMA: MEI 30 Mwaka huu 2025, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Kilimo iliandika historia katika Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), baada ya kupokea ndege ya kisasa aina ya Thrush 510P2+.

 

Ndege hiyo imenunuliwa kwa ajili ya kudhibiti Visumbufu vya mazao ambavyo ni magonjwa na wadudu waharibifu ambavyo vingeathiri uzalishaji wa mazao ya wakulima.

 

 

Akizungumza kwenye hafla ya mapokezi ya ndege hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Profesa Joseph Ndunguru anamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za dhati za kutaka kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo yenye malengo ya kuongeza tija, ajira, kupanua na kuimarisha masoko.

 

Vile vile kuimarisha hali ya chakula na kuimarisha ushirika.

 

Anaeleza umuhimu wa ndege hiyo ya kisasa katika kuimarisha usalama wa chakula hapa nchini kwa kusema kuwa, kilimo kimekuwa nguzo ya uchumi kikiwapa mamilioni ya Watanzania riziki na ajira.

 

“Hata hivyo, changamoto tunazokutana nazo katika kuhakikisha upatikanaji wa chakula wa kudumu ni nyingi.

 

Mojawapo ni vitisho vikubwa kwa mazao yetu ya nafaka hasa mpunga, mtama na uwele kuvamiwa na ndege waharibifu aina ya kwelea kwelea nzige na viwavi jeshi.

 

“Kwa miaka mingi, ndege hawa wamekuwa tishio kubwa kwa uzalishaji wa kilimo, hasa kwa wakulima wa vijijini wanaotegemea sana mavuno ya mazao haya.

 

“Katika msimu wa hivi karibuni, idadi ya ndege wa kwelea imeongezeka, na kufanya kuwa vigumu kwa wakulima kuyalinda mazao yao kwa kutumia mbinu za kizamani,” anasema.

 

 

Anaongeza kwamba, matokeo ya kuongezeka kwa ndege hao ni tishio la kupoteza mazao jambo ambalo limekuwa ni changamoto kubwa, na kuathiri usalama wa chakula na maisha ya wakulima.

 

Profesa Ndunguru anasema kwa kutumia ndege hiyo mamlaka itakuwa na uwezo wa kufikia maeneo mapana kwa muda mfupi zaidi kuliko ilivyokuwa ikutumia mbinu za kizamani, kuhakikisha kwamba athari za ndege wa kwelea zinapunguzwa,

 

Hivyo kulinda mazao ya wakulima na hatimaye, kuhakikisha upatikanaji wa chakula kwa taifa.

 

“Kwa uwezo wake wa kufanya kazi katika maeneo magumu, kufikia maeneo ya mbali, na kunyunyiza kiuatilifu kwa usahihi, kitatekeleza jitihada zetu za kudhibiti ndege hao kwa kiwango cha juu.

 

“Hii haitayalinda tu mazao yetu, bali pia itaboresha maisha ya wakulima wanaotegemea mavuno bora ili kuhudumia familia zao, kuwapeleka watoto shule, na kujenga maisha bora kwao na kwa jamii zao.

 

“Zaidi ya kulinda mazao, ndege hii pia itachangia katika kuongeza tija ya kilimo. Kama tunavyofahamu, usalama wa chakula hauhusu tu kiasi, pia unahusisha ubora.

 

“Kwa kuhakikisha kwamba mashamba yetu yanalindwa dhidi ya uvamizi wa kwelea kwelea, tunaweza kuhakikisha kuwa chakula tunachozalisha ni salama, cha afya, na cha kutosha. Hii itachangia sana katika kupungua kwa bei za mazao muhimu na kupunguza hatari ya njaa katika nyakati za ukame au changamoto nyingine za kimazingira,” anasema.

 

 

Anasema wakulima wamekuwa wakipambana na visumbufu kwa kutumi nyezo duni za asili kama mitego, mawe, udongo, sanamu na kelele, lakini ufanisi wake mara zote umekuwa mdogo sana.

 

Anasema visumbufu hivyo hutokea kwa wingi sana na huweza kuvamia maelfu ya ekari, na kuharibu kiasi kikubwa cha mazao kwa muda wa siku chache.

 

Anatolea mfano kuwa, kundi moja la ndege waharibifu wa kwelea kwelea hujuimuisha ndege kati ya maelfu hadi zaidi ya milioni kumi.

 

“Makundi ya ndege waharibifu hawa yana uwezo wa kula na kuharibu nafaka zote kwenye mashamba yenye zaidi ya ekari 2000 ndani ya siku moja.

 

“Kwa mfano kundi lenye ndege waharibifu wa Kwelea kwelea milioni mbili linaweza kula na kuharibu zaidi ya tani ishirini za nafaka kwa siku moja. Kundi dogo la nzige lenye nzige milioni 80 linaweza kula chakula sawa na kile kinacholiwa na watu 35,000 kwa siku moja,” anasema.

 

Profesa Ndunguru anasema, milipuko ya ndege waharibifu wa Kwelea kwelea hutokea kila msimu wa kilimo, hususan katika kipindi cha kiangazi kwenye maeneo yanayoendesha kilimo cha umwagiliaji hasa katika zao la mpunga.

 

 

Kwamba, Kwa kipindi cha msimu wa kilimo, takribani Halmashauri za Wilaya arobaini nchini huvamiwa na ndege waharibifu wa Kwelea kwelea wanaokadiriwa kufikia milioni 200 kila mwaka wenye uwezo wa kuharibu takribani tani 450,000 za nafaka

 

Vile vile kwa kipindi cha kiangazi jumla ya skimu za umwagiliaji za zao la mpunga 38 zimekuwa zikivamiwa na ndege waharibifu aina ya Kwelea kwelea wapatao takribani milioni 100 kila mwaka wenye uwezo wa kula na kuharibu karibu tani 225,000.

 

Anasema ndege hao waharibifu wa Kwelea kwelea sio tu wamekuwa wakisababisha upotevu mkubwa wa chakula mashambani lakini pia wakulima wamekuwa wakipoteza muda mwingi kuwepo shambani ili kuwafukuza.

 

Ndege hii itasaidia kuongeza ufanisi katika udhibiti wa kwelea kwelea hivyo kutoa nafasi kwa wanachi Wakulima kufanya kazi nyingine za kiuchumi na watoto kutokusimamisha masomo yao.

 

Kuhusu ndege hiyo, imenunuliwa kwa fedha za serikali takribani bilioni sita, ikiwa ni juhudi za serikali ya Awamu ya Sita kupitia Wizara ya Kilimo katika kulinda usalama wa chakula nchini na pia wakulima kupata ziada ya mazao kwa ajili ya kuuza na kujipatia kipato.

 

Kwamba ndege hiyo  maalum aina yaThrush 510P2+ itatumika katika kudhibiti Visumbufu vya mimea na mazao kwa njia ya anga.

 

Kwani Kwa kipindi kirefu Tanzania imekuwa ikikabiliana na uvamizi wa ndege aina ya kwelea kwelea kwenye mashamba ya wakulima kwa kutumia ndege za shirika la DLCO-EC toka nchini Kenya.

 

“Moja ya changamoto tulizokuwa tunakumbana nazo ni kuchelewa kufika kwa ndege hizo kutokana na sababu za kiutendaji, na pale milipuko inapotokea kwa wakati mmoja katika nchi wanachama zinashindwa kukidhi mahitaji.

 

“Hivyo ujio wa ndege hii ni ukombozi mkubwa kwa wakulima wa Tanzania katika maeneo ya Mbarali, Kapunga, Igunga, Singida, Magu, Simiyu, Manyara, Kondoa, Mvomero, Kilosa na maeneo mengine, kwani inawahakikishia mavuno na usalama wa mazao yao.

 

“Ndege hii pia inaweza kutumia kuzima moto kwenye maeneo makubwa pale unapotokea.

 

Ndege hii ina utendakazi wa hali ya juu na imeundwa kwa ajili ya matumizi ya shughuli za kilimo ikiwa ni pamoja na kunyunyizia Viuatilifu na mbolea shambani kwa njia ya anga,” anasema.

 

Anataja sifa nyingine za ndege hiyo kuwa ina tenki la mafuta lenye ujazo wa lita 863 hali inayopelekea ndege kuweza kukaa angani takribani saa nne.

 

Pia ina tenki la Viuatilifu lenye ujazo wa lita 1,930. Kwa uwezo huu, ndege hii inaweza kudhibiti ndege waharibifu wa Kwelea kwelea, viwavijeshi na nzige kwenye eneo lenye ukubwa wa ekari 2400 kwa mara moja.

 

Ina vifaa vya kisasa vya redio “Avionics” vinavyoipa uwezo wa kutumika kufanya uchunguzi wa maeneo yenye viashiria vya uwepo wa Visumbufu na taarifa hizo kuaminika na kuwekwa kwenye Mpango waUnyunyiziaji wa kudhibiti wa Visumbufu katika eneo husika.

 

Maelezo ya Mkurugenzi Mkuu huyo wa TPHPA, ndege hii imekusudiwa kuongeza ufanisi na wigo katika uchunguzi na udhibiti wa Visumbufu vya mimea nchini.

 

“Ndege hii imekuja wakati muaafaka wakati Tanzania inahimiza kilimo cha umwagiliaji kinachoenda kufungua mashamba mapya na mengi ya mpunga ambayo moja ya changamoto yake kubwa ni uvamizi wa ndege aina ya kwelea kwelea.

 

“Visumbufu vya mimea hususani ndege waharibifu aina ya Kwelea kwelea, nzige na viwavi jeshi vamizi huchangia kwa kiasi kikubwa katika upotevu wa chakula mashambani hivyo kuhatarisha usalama wa chakula nchini na kupunguza tija katika uzalishaji wa mazao,” anasema.

 

Ndunguru anasema, ndege hii pia itakuwa nyezo muhimu katika udhibiti wa majanga ya nzige ambayo huikumba Tanzania mara kwa mara na kuhatarisha usalama wa chakula na malisho ya mifugo.

 

Anasema Tanzania imekuwa ikivamiwa na nzige wa aina tatu ambao ni nzige Wekundu, Jangwani na Miti. Ndani ya Tanzania kuna maeneo makuu matano ambayo ni mazalia ya Nzige Wekundu yenye ukubwa wa jumla ya kilomita za mraba 8000. sawa na ekari 1,976,843.

 

Maeneo haya ni pamoja na Mabonde ya Wembele, Malagarasi, Uwanda wa Iku-Katavi,

 

Uwanda wa Bahi na Bonde la Rukwa. hivyo ndege hii maalum itasaidia kufanya uchunguzi na udhibiti wa Nzige kwenye maeneo hayo.

 

Anasema ufanisi katika operesheni za ndege hiyo utategemea ushirikiano mkubwa utakaowezeshwa na wadau wote katika tasnia ya kilimo nchini Tanzania.

 

Ndege hiyo ni chombo kama vyombo vingine vya udhibiti wa Visumbufu, kama vile ndege nyuki na mabomba.

 

Kuendelea kuwa katika hali bora kiutendaji itategemea sana mazingira bora na utashi wa kisiasa katika utekekelezaji wa majukumu yake.

 

“Mathalan, hili linajumuisha kuweka viwanja vidogo katika hali bora ya kimatumizi, eneo ambalo Halmashauri mbalimbali nchini ni wadau wa msingi.

 

“Lakini, vile vile mazingira bora ya Kisera yatakayowezesha ndege hiyo kufanya kazi bila matatizo katika anga la mikoa mbalimbali,” anasema.

 

Anasema mategemeo ni kwamba mamlaka nyingine za serikali  na sekta binafsi zikiwemo Ofisi ya Raisi – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyama Pori Tanzania (TAWA), Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI), Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA).

 

Vile Vile Taasisi ya Kilimo cha Mboga Mboga na Matunda nchini (TAHA),  Shirika la Kudhibiti Nzige wa Jangwani (DLCO-EA) na IRLCO CSA zitaendelea kushirikiana na TPHPA katika kutumia ndege hii hususani kwenye kunyunyiza Viuatilifu ambavyo ni viuadudu, viuakuvu na viuagugu na mbolea mashambani.

 

 

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Hussein Bashe baada ya kupokea ndege hiyo mpya, ameagiza kuanza  mara moja kwa mchakato wa ununuzi wa ndege nyingine nchini..

 

Bashe ametoa maelekezo kwa Mamlaka hiyo kuhakikisha katika vituo vinne vya Kilimo nchini kuwe na Kilimo anga  vikiwa na ndege pamoja na ndege nyuki.

 

Maelekezo ya Bashe ni kwamba, mchakato wa ununuzi wa ndege hizo  uanze akiwa bado madarakanu kabla ya kwenda kwenye Uchaguzi Mkuu kwa kuwa bajeti ya Kilimo imeshapita.

 

“Ni lazima kama nchi tujitegemee, dunia ya kubebana haipo,wadau Wa maendeleo tunawashukuru sana,” amesema Bashe akitaja vituo vinne vya Kilimo kuwa ni Arusha, Dodoma,Mwanza na Mbeya.

 

Anasema  nchi imeshaanza kununua ndege nyuki  kwa ajili ya ufuatiliaji na sasa inanunua kwa ajili ya kunyunyiza na hivyo lazima watanzania wajue hilo.

 

“Hivyo kelele za kwelea kwelea ni nchi nzima na kwamba Ilani  ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyozinduliwa inazungumzia Kuwekeza kwenye  Kilimo Cha umwagiliaji,” anasema na kuongeza kuwa ndio maana Kuna Mradi mkubwa Wa umwagiliaji kwa ziwa Viktoria na Tanganyika wenye hekta milioni tatu.

 

Anasema hivyo lazima kujiandaa, na kutambua kuwa  Tanzania ina maeneo yenye mazalia ya nzige wekundu ambayo ni Dodoma,Katavi na Rukwa.

You Might Also Like

MATUKIO YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI SASA DISEMBA 2024:

BAADHI YA MATUKIO MAKUBWA YA UKATILI YALIYOFANYIKA MWAKA 2024

BAADHI YA MATUKIO YA KISIASA YALIYORIPOTIWA KUANZIA JANUARI 2024 HADI DISEMBA 2024;

Shen Zhiying: Mkongwe Aliyeanzisha Kozi Ya Kiswahili Nchini China

Daraja La Magufuli Laimarisha Uhusiano Wa Jumuiya Ya China,Tanzania Yenye Mustakabali Wa Pamoja

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanafunzi 431, Watumishi 52 Watembelea TARI kujifunza Kilimo
Next Article Mdemu Azindua Utafiti Uliofanywa na FES Kwa Kushirikiana Na COTWU – T
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?