MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kingalame Asisitiza Umuhimu wa Wachimbaji Kuuza Dhahabu Serikalini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kingalame Asisitiza Umuhimu wa Wachimbaji Kuuza Dhahabu Serikalini
Habari

Kingalame Asisitiza Umuhimu wa Wachimbaji Kuuza Dhahabu Serikalini

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: MKUU wa Wilaya ya Nyang’hwale, Grace Kingalame, amesema Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeendelea kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji, na hadi sasa taifa lina akiba ya takribani tani 10 za dhahabu.
Amesema hayo katika Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Sekta ya Madini, yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili, mkoani Geita alipofanya ziara.
Habari Picha 9591
Kingalame amesema hatua hiyo ni matokeo ya juhudi za serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha wananchi wote.
“BoT imepiga hatua kubwa. Watu wanaendelea kuleta dhahabu na serikali inanunua. Hili linaonyesha dhamira ya kweli ya kuhakikisha Tanzania inakuwa miongoni mwa nchi tano bora barani Afrika kwa uzalishaji wa dhahabu,” amesema.
Ameongeza kuwa serikali haijawabana wachimbaji, bali imeweka mazingira rafiki yanayowawezesha kuuza dhahabu ndani na hata nje ya mipaka ya Tanzania, kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.
Habari Picha 9592
“Ni muhimu wachimbaji wa Nyang’hwale na maeneo mengine waelewe kuwa kuuza dhahabu kwa serikali kunasaidia taifa kuwa na akiba ya kutosha. Lakini pia, kila mmoja anafaidika mjasiriamali na taifa kwa ujumla,” amesema.
Katika hatua nyingine, amewataka wananchi kufika katika maonesho hayo kujifunza kuhusu teknolojia mbalimbali zinazotumika katika sekta ya madini ikiwemo uchimbaji, uchenjuaji na uchorongaji wa dhahabu, akisisitiza kuwa elimu hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya sekta.
Pia amepongeza juhudi za wajasiriamali waliopo kwenye maonesho hayo kwa kuonesha ubunifu na bidii katika kukuza uchumi wa nchi kupitia shughuli zao mbalimbali.
“Wajasiriamali wanafanya kazi kubwa. Nimefurahishwa na namna wanavyojishughulisha na kujipambanua katika utafutaji wa kipato na kuchangia ukuaji wa uchumi wetu,” amesema.

You Might Also Like

Sekta Binafsi Zazuia Wafanyakazi Kujiunga Na Vyama Vya Wafanyakazi

Soko La Kisasa La Nyamachoma Lazinduliwa Vingunguti

CCCC Yakutana na Wanahabari, Yapanga Mikakati Mipya 2025

Wapongeza Nyongeza Ya Likizo Kwa Aliyejifungua Mtoto Njiti

Kilimo Yaomba Trilioni 1.24 Mwaka Wa Fedha 2025/26

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Fursa za Uwekezaji Kanda ya Ziwa: Buzwagi na Maeneo Mengine ya Kimkakati
Next Article TARURA Yatenga Milioni 580 Kuboresha Barabara Zinazohudumia Sekta ya Madini Geita
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Katoro Yapata Gari Jipya la Zimamoto, Kuwasili Februari 9
Habari February 4, 2026
Waziri Mbarawa Aagiza Adhabu Kali kwa Madereva, Makondakta Wanaonyanyasa Wanafunzi
Habari February 4, 2026
Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?