MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi
Habari

Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: WAUMINI wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), wamehimizwa kulipa kodi ili kuiwezesha nchi kupata maendeleo.
Askofu Mkuu wa KKKT Dkt. Alex Malasusa amehimiza hilo wakati Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Juma  Mwenda alipokwenda ofisini kwake kumsalimia.
Dkt. Malasusa amesema kwa kulipa kodi serikali itaweza kukamilisha malengo endelevu kwa munufaa ya watu wake.
“Hakuna nchi inayoendelea bila kodi. Ukiona Maendeleo ya nchi maisha bora ni sababu ya  kodi wala  hakuna muujiza hapo.
“Shida tunayopata ni wanaotoa  kodi ni wachache hivyo mzigo unakuwa  mkubwa, unawaelemea hao wachache walio waaminifu.
“Ili nchi iendelee lazima kuhakikisha binadamu anapata mahitaji muhimu ikuwemo chakula,” amesema.
Malasusa ameahidi kutoa elimu kanisani ili waumini waelewe na kıtımıza wajibu wao kama ilivyo kwenye maandiko matakatifu.
“Naahidi kushirikiana nanyi (TRA) kutoa elimu, kuwakumbusha kila siku pia kuwaambia kuwa maandiko yako wazi na  tuheshimu mamlaka.
“Sasa tutashirikiana na wachungaji tuzungumzie ndani ya kanisa maana suala la kodi liliachwa sana tukawa tunahamasisha masuala mengine kama ya afya na mengineyo.
“Sasa tunafungua milango ya kuelezea hili ‘damu ya Tanzania’(kodi). Kanisa na taasisi zake zote watakuwa mstari wa mbele,” amesema.
Amesema  elimu ya mlipa kodi ikipenyezwa makanisani watanzania watalipa kodi  bila kulazimishwa na kwa furaha.
Awali Kamishna Mwenda amesema amefika ofisini kwa Askofu Malasusa kuona namna gani ya kushirikiana ili kuweza kutoa elimu kwa mlipa kodi.
“Kwa kuwa kanisa lina waumini wengi na hao ndio walipa kodi ni vizuri wajue kodi ipi inalipwa na ni kwa wakati gani na analipa wapi,” amesema.
Amesema kwa nafasi na fursa aliyonayo askofu ni rahisi kuwabadilisha waumini wake.
Amemshukuru Malsusa kwa utayari wake wa kukubali kushirikiana na TRA  kuelimisha jamii.

You Might Also Like

Sekta ya Huduma Kuchangia Asilimia 45 Katika Uchumi Wa Nchi

THBUB Mdau Mkubwa Utekelezaji Wa Majukumu 

TPHPA, MUCE Wasaini Hati Ya Makubaliano Maeneo Yanayogusa Sayansi

Balozi wa Tanzania Nchini Italy Afurahishwa  Ubunifu wa TPHPA Maonesho ya Nanenane

Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Yapambana Kutokomeza Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele
Next Article Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Laleta Furaha Kwa Watoto
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
Viongozi Wa Dini Zote Wajifungie Kuomba,Kujadili Na Kutoa Mapendekezo-SAU
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?