MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kagera, Geita kuanza uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kagera, Geita kuanza uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura
Habari

Kagera, Geita kuanza uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura

Author
By Author
Share
2 Min Read
 Na Mwandishi Wetu
UBORESHAJI wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoani Geita na Kagera utafanyika kwa siku saba kuanzia Agosti tano hadi 11, mwaka huu.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Jacobs Mwambegele amesema hayo wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoani Geita leo.
Mkutano kama huo mkoani Kagera umefunguliwa na Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufaa Mstaafu, Mbarouk Salim Mbarouk ikiwa ni maandalizi ya uboreshaji wa Daftari kwenye mikoa hiyo.
“Mzunguko wa pili wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utajumuisha mkoa huu wa Geita na Kagera ambapo uboreshaji utaanza Agosti tano hadi 11, mwaka huu ” amesema Mwambegele.
 Maelezo yake ni kwamba, mikoa hiyo inafanya uboreshaji kwenye mzunguko wa pili baada ya mzunguko wa kwanza ambao umejumuisha mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora ambako ulianza Julai 20,  unatarajiwa kukamilika Julai 26 2024.
“Tume tayari imeanza uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,  uzinduzi ulifanyika mkoani Kigoma Julai 20 mwaka huu.
“Uzinduzi huo umeenda sambamba na kuanza kwa mzunguko wa kwanza wa uboreshaji kwenye mikoa mitatu ya Kigoma, Tabora na Katavi, utaendelea hadi Julai 26,” amesema.
Mkoani Kagera Jaji Mbarouk amesisitiza kadi za wapiga kura zilizotolewa 2015 na 2020, zitaendelea kutumika kwenye chaguzi zijazo.
Naye Mkurugenzi wa uchaguzi wa tume hiyo, Kailima Ramadhan amesisitiza kuwa
wapiga kura wanaoboresha taarifa zao wanaweza kuanza mchakato wa awali kwa kutumia simu janja, kiswaswadu na kompyuta kupitia mfumo ujulikanao kama Online Voters Registration System (OVRS) au kwa kubobya *152*00#, kisha namba 9 na kufuata maelekezo.

You Might Also Like

SPIKA asisitiza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 

Bunge lapitisha muswada marekebisho ya sheria za Hifadhi ya Jamii

Rais Samia atoa zaidi ya bil. 2.1 usimikaji wa mifumo, uendeshaji mashauri ya wafanyakazi

Mwanafunzi UDSM Aja Na Nyama Ya Mimea

BOT Yafungia Applications 69 Za Mikopo Mtandaoni

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali kuleta kicheko kwa TASU 
Next Article Bodi ya mkonge kutoa ajira kwa watu 10,000 ifukapo 2030
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari August 6, 2025
Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?