MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: JOWUTA Yapokea Cheti Kwenye Uzinduzi Wa Jengo La Biashara TUCTA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > JOWUTA Yapokea Cheti Kwenye Uzinduzi Wa Jengo La Biashara TUCTA
Habari

JOWUTA Yapokea Cheti Kwenye Uzinduzi Wa Jengo La Biashara TUCTA

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
ARUSHA: SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) limezindua jengo lake jipya la biashara jijini Arusha, katika hafla iliyoambatana na utoaji wa vyeti kwa vyama wanachama wake, ikiwa ni ishara ya kuimarika kwa mshikamano na upanuzi wa ushirikiano ndani ya shirikisho hilo.
Miongoni mwa vyama 16 vilivyotunukiwa vyeti ni Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA). Cheti hicho kilikabidhiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete, kwa Mwenyekiti wa JOWUTA, Mussa Juma.
Habari Picha 9013
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais wa TUCTA, Tumaini Nyamhokya, amesema kujiunga kwa JOWUTA kunafanya idadi ya vyama ndani ya TUCTA kufikia 16, kutoka 13 vilivyokuwepo awali.
Ametoa wito kwa waandishi wa habari kujiunga na JOWUTA ili kufurahia fursa mbalimbali, ikiwemo kutetewa kwa maslahi yao na kupewa elimu kuhusu haki na wajibu kazini.
Habari Picha 9014
Mbali na JOWUTA, vyama vipya vilivyopokea vyeti ni Chama cha Wafanyakazi Sekta ya Ulinzi Binafsi (TUPSE) na Chama cha Wafanyakazi wa Huduma za Viwandani Tanzania (TASIWU).
Kwa upande wake, Mussa Juma, Mwenyekiti wa JOWUTA, ameshukuru TUCTA kwa kutambua mchango wao na kuwapokea rasmi.
Amesema jukumu kubwa walilonalo sasa ni kuhakikisha wanahabari wanatetea maslahi yao na kufanya kazi katika mazingira bora.
Habari Picha 9015
“Tutaendelea kushirikiana na TUCTA kuhakikisha wanahabari wanafanya kazi kwa kuzingatia sheria, wakiwa na mikataba rasmi na ajira zinazotambulika kisheria,” amesena.
Akihutubia katika uzinduzi huo, Waziri Ridhiwani amesema TUCTA lina mchango mkubwa katika historia ya nchi kabla na baada ya uhuru, na kwamba mafanikio mengi ya taifa hayawezi kutajwa bila kuwahusisha wafanyakazi.
“Asiyeona umuhimu wa shirikisho hili si mzalendo wa kweli. Serikali haitasahau wala kuwadharau wafanyakazi, kwani wao ndio chimbuko la mafanikio mengi ikiwemo elimu, miundombinu na huduma mbalimbali,” amesema Waziri Ridhiwani.

You Might Also Like

Kanisa lakabidhi jengo la watoto la milioni 595 kwa serikali

Tunatekeleza Azma YA Rais Samia Kuwafikia Wananchi Waliojiajiri

JAB Yaanza Rasmi Kutoa Vitambulisho Kwa Waandishi Wa Habari

Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 

Shirikianeni kutekeleza majukumu- Possi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waomba Kuondolewa Vikwazo Vya Biashara Ya Mazao Ya Kilimo Ikolojia Mipakani
Next Article Vyama Vya Wafanyakazi Himizeni Na Kufundisha  Amani Ya Nchi Kuelekea Uchaguzi Mkuu -Ridhiwan
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mbarawa Aagiza Adhabu Kali kwa Madereva, Makondakta Wanaonyanyasa Wanafunzi
Habari February 4, 2026
Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?