MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: ‘Jichunge’ Programu Ya Simu Yenye Mafanikio Katika Kuboresha Matumizi Ya Dawa Kinga Dhidi Ya VVU
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > ‘Jichunge’ Programu Ya Simu Yenye Mafanikio Katika Kuboresha Matumizi Ya Dawa Kinga Dhidi Ya VVU
Habari

‘Jichunge’ Programu Ya Simu Yenye Mafanikio Katika Kuboresha Matumizi Ya Dawa Kinga Dhidi Ya VVU

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WATAFITI kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kupitia Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi iliyopo Mbeya,  Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), na Chuo Kikuu cha Oslo  (Norway) wamebuni programu ya simu janja iitwayo ‘Jichunge’, ambayo inalenga kuboresha matumizi ya dawa za kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi (PrEP).

Mradi huu unaendeshwa kwa usimamizi wa Dkt. Christopher Mbotwa, Mhadhiri wa Takwimu, Baiolojia na Epidemiolojia chuoni hapo.

Dkt. Mbotwa amesema programu hiyo ni sehemu ya utafiti mpana unaojulikana kama Jaribio la Programu za Simu katika Kuboresha Matumizi ya Dawa za Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Amesema lengo kuu la utafiti huo ni kuangalia namna teknolojia ya simu inaweza kutumika kuboresha afya ya umma na kusaidia kufikia malengo ya kimataifa ya kutokomeza UKIMWI kama tishio la kiafya kufikia mwaka 2030.

Amesema ingawa dawa za kinga (PrEP) zimeonekana kuwa na ufanisi mkubwa kwa watu walioko kwenye hatari ya kuambukizwa VVU, changamoto kubwa imekuwa ni ufahamu mdogo, kutotumia dawa kwa wakati, na kukosekana kwa ufuatiliaji wa karibu wa kitabibu.

Dkt. Mbotwa amesema, “Watu wengi wanaopewa dawa za kujikinga hushindwa kuzitumia ipasavyo. Wengine hawajui ni lini waache au waanze kuzitumia, wengine hawaelewi madhara au faida zake. Matumizi yasiyo sahihi yanaweza kupunguza kabisa ufanisi wa dawa hizo.”

Amesema Programu ya Jichunge, inayopatikana kwenye simu janja, imetengenezwa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Chuo Kikuu cha Oslo, Norway ina faida nne ambazo ni,

Kumkumbusha mtumiaji muda wa kutumia dawa kwa usahihi kila siku ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa njia rahisi kuhusu dawa hizo, faida, madhara, na namna bora ya kuzitumia.

Vile vile mtumiaji kuweza kuwasiliana moja kwa moja na mtaalamu wa afya kwa maswali au changamoto za kiafya.

Amesema pia Programu hiyo humuunganisha mtumiaji na mtu aliyepitia mafunzo kuhusu dawa hizo, anayetoa msaada wa kisaikolojia na kijamii kwa wanaotumia PrEP.

Amesema kwa ajili ya kuthibitisha ufanisi wa programu hiyo, utafiti ulifanyika katika mikoa miwili ya Dar es Salaam na Tanga ambapo washiriki wa Dar es Salaam walipewa programu ya Jichunge, huku wale wa Tanga waliendelea kutumia PrEP bila msaada wa programu.

Amesema matokeo ya awali yalionyesha kuwa idadi ya watu waliotumia dawa kwa usahihi Dar es Salaam ilikua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na wa Tanga.

“Hii inaashiria kwamba programu ya Jichunge inaongeza ufanisi wa matumizi ya PrEP na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika juhudi za kupunguza maambukizi ya VVU nchini,” amesema.

Kwa mujibu wa Dkt. Mbotwa, mafanikio haya yanatoa picha halisi kuwa ‘teknolojia ya afya ya kidijitali’ inaweza kuwa sehemu muhimu ya mikakati ya kiafya ya taifa, hasa kwa makundi yaliyo hatarini.

Mpango wa kupanua matumizi ya programu hii unatarajiwa kuendelea kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya ndani na nje ya nchi, huku matumaini yakiwa makubwa kwamba, kwa kutumia mbinu kama hizi, Tanzania inaweza kufanikisha lengo la kuwa na jamii isiyo na maambukizi mapya ya VVU ifikapo mwaka 2030.

You Might Also Like

Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais Samia Suluhu Hassan, kuongoza Kamati Kuu Maalum kesho

Waajiri Wathamini Taaluma Ya Uandishi Wa Habari – Dkt. Mkoko

Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika

Kimwaga Mwenyekiti Mpya DCPC, Ahimiza Nidhamu

Rais Samia Aongoza Waombolezaji Kutoa Heshima Za Mwisho Kwa Mbunge Ndungulile

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Toleo La Sheria Zilizotafsiriwa Kwa Kiswahili Kutoka Agosti
Next Article TARI Yabadilisha Kilimo kwa Teknolojia Mpya, Za Kisasa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?