Na Lucy Lyatuu
BALOZI wa Italia nchini Tanzania Giuseppe Sean Coppola amesema ubunifu wa bidhaa mbalimbali ni jambo muhimu linalohusisha urithi, utamaduni na historia ya Taifa.
Amesema ubunifu ni sehemu ya kuoneshwa uzuri wa bidhaa zinazozalishwa nchini lakini pia huleta faraja.
Balozi Coppola amesema hayo Dar es Salaam wakati Italia ikiadhimisha miaka 10 ya ubunifu ambayo imetumika kuzindua na kuonesha bidhaa mbalimbali za kibunifu za vioo zinazozalishwa na kampuni ya Rangi Gallery ya jijini Arusha.

Amesema mpango wa maonesho hayo ya kibunifu umekuzwa na viongozi wa Italia lengo likiwa ni kuonesha muundo wa nchi hiyo na bidhaa zinazozalishwa.
“Bila shaka, Italia ni nchi muhimu sana katika suala la uzalishaji na asili ya usanifu, haswa ikiwa na mkusanyiko maalum katika mji wa Milan, ambao ni Maalum Kwa usanifu barani Ulaya” amesema

,Amesema maadhimisho hayo Yana kauli mbinu ya kubuni upya, kuunda upya na kubuni mawazo up ya , nafasi na uhusiano na vitu.
Kuhusu Rangi Gallery amesema wameingia makubaliano kuonesha uzalishaji wa mradi huo wa bidhaa za viooambao ujuzi umechukuliwa kutoka Murano.

“Tuna watu, watu mahiri, mafundi wanaotengeneza vioo ambao walikuja hapa Novemba jijini Arusha wakiwafundisha watu huko jinsi ya kuunda vitu zaidi na ufundi mzuri zaidi wa mikono kwa kutumia mbinu maalum ikihusisha takataka,” amesema na kuongeza kuwa Italia inaunga mkono mradi huo kwa sababu ni muhimu sana kutoka kwa mtazamo wa mazingira na kijamii.
Mkurugenzi wa Rangi Gallery,Nona Mashiba wanashirikiano na WA Italiano kutengeneza bidhaa hizo zitokanazo na takataka za vioo na chupa na kuunda vitu vizuri na vya kitofauti.

Amewataka wabunifu na wasanii wa aina mbalimbali kujitokeza na kushiriki kuunda bidhaa hizo ambazo ni za kipekee .

