MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Daraja La Magufuli Laimarisha Uhusiano Wa Jumuiya Ya China,Tanzania Yenye Mustakabali Wa Pamoja
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > Daraja La Magufuli Laimarisha Uhusiano Wa Jumuiya Ya China,Tanzania Yenye Mustakabali Wa Pamoja
Makala

Daraja La Magufuli Laimarisha Uhusiano Wa Jumuiya Ya China,Tanzania Yenye Mustakabali Wa Pamoja

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Waandishi Wetu

DARAJA la J.P. Magufuli nchini Tanzania, lililojengwa na Kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) ikishirikiana na Kampuni ya China Railway 15th Bureau Group Corporation Limited (CR15), liliunganishwa kwa mafanikio makubwa, Oktoba sita mwaka jana 2024.

Ikiwa ni mradi muhimu wa kitaifa nchini Tanzania, daraja hilo linalopita juu ya Ziwa Victoria na kuunganisha Mkoa wa Mwanza na Geita ndilo daraja la Sita kwa urefu Barani Afrika.

Uwepo wa daraja hilo utapunguza urefu wa safari kutoka saa mbili mpaka dakika 15.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua Daraja hilo jijini Mwanza Mei Mwaka huu 2025, na kwamba daraja hilo ni moja ya miradi mikubwa ya kimkakati ya serikali ya Awamu ya Sita anayoiongoza.

Daraja hilo (Kigongo–Busisi) lenye urefu wa kilomita tatu na barabara unganishi Kilomita 1.66, linaunganisha Barabara Kuu ya Usagara–Sengerema–Geita zenye urefu wa Kilomita 90, upana wake ni mita 28.45 unaojumuisha njia mbili za Magari zenye upana wa mita saba kila upande.

Njia ya maegesho ya dharura mita 2.5 kila upande, njia za watembea kwa miguu mita 2.5 kila upande, eneo la kati linalotenganisha uelekeo tofauti wa barabara mita 2.45, kingo za magari mita 0.5 kila upande,

Na kingo za watembea kwa miguu mita 0.5 kila upande. Na Usanifu wa daraja hilo umetumia teknolojia ya madaraja marefu inayoitwa ‘Extra Dosed Bridge’ ambapo kutakuwa na nguzo kuu tatu.

Wakati wa ujenzi, timu ya mradi ilizingatia kanuni ya ‘ujenzi wa kijani’, ikitafiti na kutumia teknolojia za ujenzi rafiki kwa mazingira ili kupunguza athari kwa ubora wa maji ya Ziwa Victoria na kuhifadhi mazingira.

Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo-Busisi)

Daraja la Magufuli limejengwa kwa gharama ya Sh. Bilioni 592.6.

Takwimu zinaonyesha kwamba, kwa ujumla mradi huo umetoa jumla ya ajira 29,211 tangu ulipoanza Februari 25, 2020 mpaka Julai 2024 ambapo asilimia 93.33 sawa na ajira 27,262 ni Wazawa, na hivyo umechochea sana ajira za ndani.

Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoani Mwanza, Paschal Ambrose amezitaja faida zitakazopatikana baada ya kukamilika kwa daraja hilo kuwa ni pamoja na kupunguza muda wa kusafiri na uwepo wa uhakika wa usafiri kwa saa 24.

Pia kuondoa msongamano wa magari uliokuwa unatokea kwenye feri.

Kwamba daraja hilo litakuwa kiungo muhimu kwa mkoa wa Mwanza na mikoa inayouzunguka pamoja na nchi jirani,  pia daraja hilo litakuwa kivutio muhimu kwa mkoa huo wa Mwanza, tena litatumika kama nembo kwa nchi ya Tanzania.

Daraja hilo ni moja kati ya madaraja makubwa zaidi Afrika Mashariki na Kati, pia ni alama ya ushirikiano wa China na Tanzania katika kujenga jumuiya ya ngazi ya juu ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja.

Kwamba kukamilika kwa Daraja hilo kutakuza kwa nguvu maendeleo ya kiuchumi ya mikoa ya Mwanza na Geita na kutoa msukumo mkubwa katika kuimarisha ushirikiano kivitendo kati ya China na Tanzania.

Mwandishi Zhou Li, mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Tianjin (TFSU)

Barua pepe: sylvanzhou@foxmail.com

Mwandishi Ning Yi, mwalimu wa Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai (SISU).

Barua pepe:02706@shisu.edu.cn

You Might Also Like

OSHA yaelimisha sheria mahala pa kazi kwa JOWUTA

Kitabu cha Utamaduni na Maendeleo Nchini Tanzania, Chaimarisha Mawasiliano ya Kitamaduni Baina ya China, Tanzania

Matukio ya Wafanyakazi Yaliyojiri kuanzia Januari 2024, Hadi Leo Disemba 31, 2024

Ndunguru: Mabadiliko Ya Tabianchi Yanachangia Kuwepo Kwa Magonjwa, Wadudu Kwenye Mazao

MATUKIO YA MISIBA KWA WATU MAARUFU YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI DISEMBA 2024

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Matumizi Mabaya Ya Dawa Husababisha Usugu Wa Vimelea Kwa Wanyama – Dkt. Kitimu
Next Article Profesa Ndunguru: Tumewezesha Usafirishaji wa Mazao Mbalimbali Yenye Thamani ya Trilioni 15.6
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Bodi Ya Wadhamini Ya NSSF Yaridhishwa Na Uwekezaji Wa Ubia Na Jeshi La Magereza
Habari May 14, 2025
TPHPA Yaelezea Vipaumbele Vyake
Habari May 14, 2025
TPHPA Tuna Mchango Mkubwa Katika Utoshelevu Wa Chakula – Ndunguru
Habari May 14, 2025
Profesa Ndunguru: Tumewezesha Usafirishaji wa Mazao Mbalimbali Yenye Thamani ya Trilioni 15.6
Habari May 14, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?