MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Elimu ya Ufundi Yachangia Maendeleo ya Taifa – VETA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Elimu ya Ufundi Yachangia Maendeleo ya Taifa – VETA
Habari

Elimu ya Ufundi Yachangia Maendeleo ya Taifa – VETA

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA:  MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), imesema ushiriki wa VETA katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana ni fursa muhimu ya kuonesha namna taasisi hiyo inavyowawezesha vijana kupitia mafunzo ya ufundi stadi yanayoendana na mahitaji ya soko la ajira.
Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Anthony Kasore amesema hayo alipotembelea banda la VETA katika maadhimisho ya Wiki ya Vijana yanayoenda sambamba na Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Kasore amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo vijana kugundua vipaji vyao na kuvitumia kwa maendeleo yao na ya jamii.
Habari Picha 9971
Katika maonyesho hayo, VETA imeonyesha bidhaa mbalimbali za ubunifu kutoka kwa wanafunzi na wakufunzi wake, zikiwemo kazi za watu wenye mahitaji maalum kama ishara ya matokeo chanya ya elimu jumuishi inayotolewa na taasisi hiyo.
“Tumekuja na mifano halisi ya bidhaa na bunifu mbalimbali zinazotengenezwa na wanafunzi wetu ili kuonesha matokeo chanya ya mafunzo tunayotoa,” amesema.
Amesema wanawake wengi pia wamenufaika kwa kupata ujuzi wa ziada unaowawezesha kuendesha shughuli zao kwa ufanisi zaidi, kupitia programu mbalimbali za uwezeshaji zinazoshirikisha VETA.
Kasore amesema  VETA inatekeleza mkakati wa kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa lengo la kutoa mafunzo ya ufundi stadi kwa wananchi kupitia programu shirikishi.
Amesema kupitia ushirikiano huo, zaidi ya wanawake 15,000 nchini kote wamepatiwa mafunzo kupitia mpango wa ‘Wanawake na Samia”, uliolenga kuwawezesha kiuchumi na kijamii.
Aidha, amewahimiza wazazi wenye watoto wenye mahitaji maalum kuwapeleka katika vyuo vya VETA badala ya kuwaficha majumbani, akisema taasisi hiyo ina miundombinu na walimu waliobobea katika kutoa mafunzo kwa makundi hayo.
Kasore amesema VETA ni taasisi pekee nchini yenye mamlaka ya kuandaa mitaala ya mafunzo ya ufundi stadi, hivyo kuhakikisha mafunzo yanayotolewa yanalingana na mahitaji ya soko na mabadiliko ya teknolojia kwa ngazi ya kitaifa na kimataifa.

You Might Also Like

DIT kudhibiti nzi wa maembe kisasa

Mikoa mitatu kuanzishwa vituo vya gesi asilia

KARIBU ESCAPE LODGE SERENGETI – NYUMBA YAKO YA KIFAHARI KATIKATI YA UFALME WA WANYAMAPORI

Tanzania Yapongeza China Kwa Kuimarisha Uhusiano Wa Kidiplomasia Kupitia Lugha, Utamaduni

Chatanda: Rais Ametuletea Kiongozi Bora Atakayetusaidia Kutekeleza Ilani Ya CCM

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article VETA Yajipanga Kutoa Mafunzo Yanayoendana na Teknolojia ya Kisasa
Next Article Uongozi OUT Waahidi Kuboresha Mazingira ya Kazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

VETA kumpa nafasi Igobeko kuongeza ujuzi na kuwawezesha wengine
Habari August 23, 2026
Airtel Yajenga Darasa La Fursa Katika Shule Ya Sekondari Magaoni,Tanga
Habari August 23, 2026
Bunifu ya dawa ya mayai yapunguza hasara kwa wafugaji wa kuku
Makala August 22, 2026
Dkt Yonaz Awakumbusha Vijana Kulinda Afya Zao Katika Mapambano Dhidi Ya Ukimwi
Habari August 22, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?