MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mgombea Urais wa CHAUMMA Atangaza Mpango wa Kunusuru Kilimo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mgombea Urais wa CHAUMMA Atangaza Mpango wa Kunusuru Kilimo
Habari

Mgombea Urais wa CHAUMMA Atangaza Mpango wa Kunusuru Kilimo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
 TUNDUMA: MGOMBEA urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu ametaja hatua mbalimbali ambazo chama chake kitaweka mbele iwapo kitapata ridhaa ya kuongoza nchi, kwa lengo la kunusuru sekta ya kilimo nchini Tanzania.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika mjini Tunduma, mgombea huyo amesema moja ya hatua ni kufungamanisha kilimo na viwanda ili kuhakikisha kuwa mazao ya wakulima yanapata soko la uhakika na kuongeza thamani ya mazao hayo kabla ya kuyasafirisha nje ya nchi.
Habari Picha 9608
Ameeleza pia kuwa serikali yao itaacha kuuza malighafi za kilimo na badala yake kuweka mkazo katika usindikaji wa bidhaa hizo ndani ya nchi.
Kadhalika, ameeleza kuwa serikali yake itaongeza ukubwa wa eneo la kilimo hadi kufikia ekari milioni tatu hadi tano, kwa lengo la kuongeza uzalishaji kwa matumizi ya ndani na viwandani.
Katika kuboresha mazingira ya uzalishaji, mgombea huyo ameahidi kuongeza bajeti ya kilimo kutoka asilimia nne ya sasa hadi kufikia kati ya asilimia saba hadi nane ndani ya miaka mitano, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuipa sekta hiyo uzito unaostahili katika ajenda ya maendeleo ya taifa.
Akizungumza kuhusu mfumo wa masoko ya mazao, ameahidi kuweka uhuru wa soko kwa kufuta utaratibu wa stakabadhi ghalani na mfumo wa kilimo cha mkataba kupitia vyama vya ushirika kama Chama cha Ushirika wa Masoko ya Mazao ya Kilimo (AMCOS), hatua ambayo inalenga kumuwezesha mkulima kupata faida stahiki kutokana na jasho lake.
Hatua nyingine alizozitaja ni kuanzishwa kwa Mamlaka ya Kilimo itakayoshughulikia masoko, utafiti, mahitaji ya kiufundi katika kilimo pamoja na kusimamia hifadhi ya taifa ya chakula.
Amesema mamlaka hiyo itakuwa nguzo muhimu katika kupanga na kuratibu maendeleo ya sekta hiyo kwa njia ya kisasa na endelevu.
Aidha, amesema serikali yake itaweka mkazo katika uboreshaji wa miundombinu ya barabara, umwagiliaji na ujenzi wa maghala kwenye maeneo ya kilimo makubwa kama vile Mabonde ya Magugu, Bahi, Igunga, Tanganyika, Bonde la Kilombero, Ziwa Rukwa na Kyela, ili kuongeza ufanisi katika uzalishaji na usambazaji wa mazao.
Vilevile, ameahidi kuanzisha Mfuko wa Kudhibiti Bei utakaosaidia kukabiliana na mabadiliko ya bei ya mazao sokoni, pamoja na kuanzisha na kuimarisha vyuo vya kilimo nchini ili kuongeza ujuzi na maarifa kwa wakulima na wataalamu wa sekta hiyo.
Kwa mujibu wa mgombea huyo, hatua hizo zinalenga kuifanya sekta ya kilimo kuwa na tija, endelevu, na yenye mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

You Might Also Like

Posta Yaleta   Usafiri Wa Kitalii Ndani Ya Sabasaba

Thamani ya Fedha Ionekane Kwenye Utekelezaji wa Miradi-Nyamoga

Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88

Tanzania Ipo Tayari Kwa Mazungumzo Ya Urejeshwaji Malikale

Wakulima Wa Zabibu Wakiri Bidhaa Zilizoongezwa Thamani Zina Soko

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kingalame Aitaka Sekta Binafsi Kushirikiana na TBA Kukamilisha Mradi wa Makazi Geita
Next Article REA Kivutio Kikubwa Uuzaji Wa Majiko Banifu Kwa Bei Ya Ruzuku
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Dkt Natu Mwamba Ashuhudia Utiaji Saini CRDB Na Taasisi Tatu Za Fedha Kimataifa
Habari October 21, 2025
Tanzania Na Africa50 Wazidi Kuimarisha Ushirikiano
Habari October 21, 2025
Madaktari Kutoka Ireland Watoa Matibabu Ya Mifupa Kwa Watoto MOI
Habari October 20, 2025
Mwalim: Nikichaguliwa urais, Kigaila atakuwa Waziri Mkuu wangu
Habari October 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?