MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wambali: Vyama Vya Wafanyakazi Muhimili wa Uchumi, Ustawi Wa Jamii
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wambali: Vyama Vya Wafanyakazi Muhimili wa Uchumi, Ustawi Wa Jamii
Habari

Wambali: Vyama Vya Wafanyakazi Muhimili wa Uchumi, Ustawi Wa Jamii

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi 
DODOMA: Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri, Vallensi Wambali amesema vyama vya wafanyakazi ni mhimili muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii.
Pia amesisitiza umuhimu wa uongozi bora, katiba shirikishi, na ushirikiano thabiti kati ya vyama, serikali na waajiri.
Amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa habari hii ofisini kwake jijini Dodoma.
Amesema ofisi yake inaratibu shughuli zote kuanzia usajili wa vyama, usimamizi hadi hatua ya mwisho kama chama kinataka kujitoa au kushindwa kutimiza masharti ya kisheria.
Habari Picha 9137
“Kwa mujibu wa Sheria ya Taasisi za Kazi Na. 7 ya mwaka 2019, kifungu cha 43 kinampa mamlaka Msajili wa Vyama kutekeleza majukumu haya,” amesema.
Pia amesema vyama vya wafanyakazi ni kiungo muhimu kati ya wafanyakazi na waajiri katika kuhakikisha kuwepo kwa mahusiano mazuri, uzalishaji wenye tija, na mazingira bora ya kazi.
“Huwezi kuzungumzia uchumi bila nguvu kazi, na huwezi kuzungumzia nguvu kazi bila kuzungumzia wanachama wa vyama vya wafanyakazi. Wanachama ndio uti wa mgongo wa taifa,” amesema Wambali.
Kwa mujibu wa Wambali, ili chama cha wafanyakazi kiwe imara, ni lazima kiwe na uongozi wenye dira, maono na uwezo wa kuwahudumia wanachama wake kwa mujibu wa katiba.
Amebainisha kuwa sheria inaruhusu watu wasiopungua 20 kuanzisha chama, lakini mara tu kinapoanzishwa, lazima kiwe na katiba inayoandaliwa kwa kushirikisha wanachama siyo viongozi peke yao.
Habari Picha 9136
“Katiba inapaswa kuakisi matarajio ya wanachama. Inapotungwa na viongozi bila ushirikiano, inakosa uhalali na kuibua migogoro isiyo ya lazima,” ameonya.
Aidha, amehimiza kwamba pamoja na katiba, chama kinapaswa kuwa na kanuni zinazoelezea utekelezaji wake.
“Endapo katiba na kanuni havilingani, huibua changamoto kubwa katika uendeshaji wa chama,” amesema.
Msajili amegusia changamoto zinazotokana na uchaguzi wa viongozi bila kufanya uchunguzi wa kina, kwamba baadhi ya vyama hujikuta na viongozi wasiokuwa na sifa au hata raia wa nchi nyingine, jambo ambalo linaathiri utendaji na kuibua migogoro.
“Ni muhimu kuzingatia mchakato wa uchunguzi wa wagombea ili kuhakikisha kuwa wana sifa stahiki za kuongoza,” amesema.
Wambali amesisitiza kuwa vyama lazima viendeshwe kwa misingi ya vikao, si kwa maamuzi ya mtu mmoja, na kuelekeza kila chama kuwa na mpango kazi wa mwaka, mpango mkakati wa muda mrefu kama wa miaka mitano, pamoja na taarifa za mapato na matumizi.
“Utawala bora unaleta uwazi kwa wanachama na huongeza imani yao kwa uongozi. Hii huongeza ufanisi na kuleta tija katika maeneo ya kazi,” amesema.
Ameongeza kuwa matumizi mabaya ya fedha na migogoro ya kiuongozi huathiri moja kwa moja maslahi ya wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na mishahara, mafao, na mazingira bora ya kazi.
Katika maelezo yake, Wambali ametoa rai kwa vyama vya wafanyakazi kuachana na uanaharakati wa zamani na kuingia katika majadiliano ya wazi na waajiri kuhusu maslahi ya wafanyakazi.
“Vyama vitambue kuwa kazi yao kubwa ni kulinda maslahi ya wafanyakazi, si ya viongozi,” amesema.
Amesisitiza pia umuhimu wa utatu baina ya serikali, waajiri, na vyama vya wafanyakazi katika kujenga uchumi imara na jamii yenye ustawi.
Amesema vyama vya wafanyakazi vina mchango mkubwa si tu katika kukuza uchumi, bali pia katika kuweka mazingira bora ya kazi, mshikamano, na maisha bora kwa wafanyakazi.
“Tusijenge vyama kwa ajili ya viongozi. Tuyajenge kwa ajili ya wafanyakazi na maendeleo ya taifa,” amesisitiza Wambali.

You Might Also Like

eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi

Profesa Ndunguru: Mabadiliko Sekta ya Kilimo Yanaenda Sambamba na Uwekezaji Katika Utafiti

Silaa: Akili Mnemba, Roboti kuongeza ufanisi,ubunifu 

Watafiti Mataifa 10 Kujadili ElimuMsingi Nchini

Serikali Kuendelea Kutenga Fedha Kwa ajili ya Ukamilishaji wa Maboma ya Vituo vya Afya

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa Ataka Wafanyakazi Waandaliwe Kwa Mabadiliko Ya Teknolojia
Next Article Bodi Ya  Bima Ya Amana Yapata Mkurugenzi  Mkuu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?