MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba
Habari

Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: RAIS mpya wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mwalimu Suleiman Ikomba, ameweka wazi mafanikio aliyoyashuhudia pamoja na viongozi wenzake katika kipindi cha mwaka 2023 hadi 2025, wakati akihudumu kama Makamu wa Rais wa chama hicho kikubwa cha wafanyakazi nchini.
Ikomba ameeleza hayo alipozungumza na Mfanyakazi Tanzania baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa chama hicho.
Pia amesema kwa kipindi hicho walifanikiwa kuimarisha utulivu na mshikamano ndani ya chama, pamoja na kupeleka huduma bora kwa walimu kupitia miradi ya maendeleo ya kijamii.
Amesema nafasi yake ya makamu wa rais ilipatikana baada ya kikao cha chama kuazimia kutangazwa kwa nafasi hiyo, hivyo Uchaguzi mkuu uliofanyika Machi 2023 katika Ukumbi wa Naivera, mkoani Tanga, na kupatiwa dhamana hiyo kupitia kura za wajumbe wa mkutano mkuu.
“Nilikuwa miongoni mwa wagombea wengi waliowania nafasi hiyo, na kwa heshima kubwa, wajumbe walinichagua. Nilitumikia nafasi hiyo kuanzia mwaka 2023 hadi 2025,” amesema Ikomba.
Vile vile Ikomba amesema kuwa moja ya mafanikio makubwa ya uongozi wao ilikuwa ni kurejesha utulivu ndani ya chama, jambo ambalo lilikuwa changamoto kubwa kwa kipindi cha nyuma.
“Tulihakikisha chama kinakuwa na utulivu wa kutosha. Zamani kulikuwa na sintofahamu na migogoro ya mara kwa mara, lakini tumeweza kutuliza hali hiyo kwa kutumia busara, kusikiliza wanachama wetu, na kushughulikia changamoto zao kwa wakati,” amesema.
Kwa upande mwingine amesema,  mradi wa ‘Samia Teachers Mobile Clinic’ ni moja ya mafanikio ya kipekee ambayo yanajivuniwa na uongozi wake, Kwa kuwa kupitia mpango huo, changamoto mbalimbali za walimu zilitatuliwa.
 “Tumefanikisha ziara ya kitaifa kupitia Samia Teachers Mobile Clinic, nimefika karibu kila mkoa nchini kasoro mikoa mitatu tu. Hii ni hatua kubwa katika kuhakikisha walimu wanatatuliwa changamoto zao pale walipo,” amesema.
 Kwa upande mwingine amesema kwamba, baada ya kupewa jukumu la kuwa Rais wa CWT, kwa kushirikiana na viongozi wenzake pamoja na wanachama, ataendeleza mafanikio hayo.
“Ninaamini katika uongozi wa pamoja. Tumejifunza mengi, tumeona ni nini kinachowezekana tukifanya kazi kwa umoja. Sasa tupo tayari kuijenga CWT imara zaidi, inayosikiliza, inayohudumia, na kulinda haki za walimu wa Tanzania,” amesema.

You Might Also Like

TEA Mshindi wa Kwanza Maonyesho Ya Mfuko wa Utamaduni

Jisajilini mapema mpate mbolea ya ruzuku

Mpogolo Aipongeza Halmashauri Maandalizi Mikopo Asilimia 10

Watuhumiwa 25 Wa Makosa Ya Mtandao Wakamatwa Na Polisi

Ulega : Nimeridhisha Na Hatua Iliyofikiwa, Ongezeni Kasi Zaidi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Afya Bora Yachochea Ustawi wa Wananchi Kigoma
Next Article Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ikomba: Aliishi Na Watoto Wiki Sita Akiwafundisha Kabla Ya Mtihani WaTaifa
Habari July 21, 2025
Samia Aleta Mapinduzi Arusha
Habari July 21, 2025
Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Habari July 20, 2025
Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Habari July 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?