MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yang’ara Sabasaba
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yang’ara Sabasaba
Habari

VETA Yang’ara Sabasaba

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeendelea kuthibitisha dhamira yake ya kubadilisha maisha ya Watanzania kupitia utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi, ubunifu na ujasiriamali katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea mkoanii Dar es Salaam.

Akizungumza katika maonesho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Antony Kasore amesema mamlaka hiyo inashiriki maonesho hayo kwa lengo la kuonesha mchango wake mkubwa katika kuwapatia Watanzania ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira na pia kuwawezesha kujiajiri kupitia fani mbalimbali za ufundi.

“Tunachokifanya kama VETA si tu kutoa elimu ya ufundi stadi, bali ni kuhakikisha kila mwanafunzi anayeondoka kwetu amejiandaa kivitendo kuingia kwenye soko la ajira ama kujiajiri.

“Ujuzi huu unawafanya vijana kuwa wabunifu, waaminifu na wachapakazi katika sekta mbalimbali,” amesema.

Katika banda lao la maonesho, VETA wameonesha mafanikio ya mafunzo yao kupitia bidhaa na huduma mbalimbali walizozibuni wanafunzi kwa kushirikiana na wakufunzi wao.

Ametaja miongoni mwa bidhaa hizo ni mashine ndogondogo za kusaidia wakulima na wafugaji, kama vile mashine za kupukuchua mahindi, mashine za kutengeneza chakula cha mifugo, na incubator zinazotumia umeme pamoja na sola kwa ajili ya kutotolesha vifaranga.

Aidha, VETA imetambulisha bidhaa za usafi na urembo zinazotengenezwa na wanafunzi kama sabuni, mafuta ya kujipaka, na bidhaa nyingine za matumizi ya nyumbani.

“Tunataka kila mwanafunzi wetu aweze kubuni bidhaa, kuijaribu, na kuiingiza sokoni. Tumefungua kampuni tanzu ya VETA ili kusaidia usambazaji na uuzaji wa bidhaa hizi,” amesema.

Amesena Mwaka huu 2025 mamlaka hiyo pia imekuja na suluhisho kwa changamoto za nishati safi, kwa kuonesha aina mpya ya majiko rafiki kwa mazingira, yanayotumia teknolojia ya kisasa kuokoa nishati na kupunguza moshi.

Katika kuunga mkono mabadiliko ya sera ya elimu ya mwaka 2023, ambayo inalenga kukuza ujuzi wa vitendo kuanzia elimu ya msingi hadi sekondari, VETA wametenga eneo maalum kwenye maonesho hayo kwa ajili ya kuwaelimisha watoto wadogo umuhimu wa kupata ujuzi wa mapema.

“Watoto wanajifunza masuala ya ushonaji, urembo na hata useremala. Wengine tayari wanaonesha vipaji vikubwa. Tunataka Watanzania waanze kutambua fursa hizi wakiwa bado wadogo,” amesema.

Amesema kuna baadhi ya wahitimu wa vyuo vikuu ambao wamejiunga na VETA baada ya masomo yao, tayari wameanzisha kampuni zao kutokana na ujuzi waliopata. Hii inaonesha wazi kuwa elimu ya ufundi stadi ni chachu ya maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

Kupitia ushiriki wake katika Sabasaba, VETA imeonesha kuwa mwelekeo wa nchi katika kukuza ujuzi na ujasiriamali unazidi kuimarika. Kwa mujibu wa Kasore, lengo kuu ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya kujifunza, kubuni na kujiendeleza kiuchumi kupitia ujuzi wa vitendo.

You Might Also Like

Wanafunzi Shule Ya Anlex, Walimu Wao Watinga Bungeni

SUA Chatumia Ngamia Mafunzo Ya Vitendo Kwa Wanafunzi

Ridhiwan Kikwete aitaka LESCO kushirikiana na serikali

Aprili 2025 Matokeo Awamu Ya Kwanza, Maoni Dira Ya Taifa Na Maendeleo 2050 Kutolewa

TPDC  Yaibuka Mshindi Sabasaba Yapata Tuzo Ya Tano

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mashine Kusaidia Uuzaji Vinywaji Bila Muuzaji
Next Article Taasisi Za Umma Zasisitizwa Kuzingatia ubora Wa Mikataba Katika Utekelezaji Wa Majukumu Yao
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

  Tanesco Yagawa Zawadi Ya Majiko Sabasaba Kuhimiza Matumizi Nishati Safi
Habari July 8, 2025
Bahari  Ina Fursa Nyingi Zisizofahamika-Tasac
Habari July 8, 2025
VETA Yafanya Mageuzi Makubwa Yaliyowezesha Wengi Kuajiriwa
Habari July 8, 2025
DIT Mwanza   Kutoa Kozi Ya Kuchakata Ngozi
Habari July 8, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?